Mara nyingi tumekuwa wagumu kuelewa somo. Umeambiwa pesa hizi zina ubora zaidi na zina security features ambazo haziwezi kughushiwa kiurahisi lakini hatuelewi. Au mtu akivaa sarawili ya kitambaa kizito ndo anakuwa amevaa nguo yenye ubora. Hizi hela niza kisasa zaidi isipokuwa matumizi yetu ndo mabaya. Mfano; mnaenda kanisani kutoa sadaka mmekunja noti, mnaficha noti sehemu za siri zinapata ukungu, wengine wanachimbia pesa chini ya shimo, wengine wanazikunja kwenye pembe za kanga, hatutumii wallet, mikono yetu inakuwa na unyevu wa maji na jasho lakini tunashika pesa. Hayo ni baadhi tu ya matumizi mabaya ya pesa zetu. Ukiangalia American Dollar---huwezi kuikunja kwa sababu unajua inaweza kukataliwa either na benki au ikagoma kupita kwenye mashine ndo maana mnazitunza vizuri.
Mie nakubaliana na Ndullu kabisa kuwa hizo noti ni bora kabisa kuliko zote zilizowahi kutoka hapa TZ.