Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 2,439
- 6,692
Rais wa World Economic Forum (WEF), Borge Brende, amejiuzulu wadhifa baada ya kubainika kuwa alikuwa na urafiki na mahusiano na marehemu Jeffrey Epstein ambaye alikuwa na makosa ya unyanyasaji wa kingono.
WEF iliagiza uchunguzi huru kumchunguza Brende baada ya nyaraka zinazomhusu Epstein kutolewa na Wizara ya Sheria ya Marekani. Brende amekiri kuwa alikutana na kula chakula cha jioni na Epstein mara tatu kati ya mwaka 2018 na 2019, na pia waliwasiliana kupitia barua pepe na ujumbe mfupi, lakini amesema hakuwa na ufahamu wowote kuhusu historia ya uhalifu wa Epstein wakati huo.
Brende, ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, pia amesema anajutia kutofanya uchunguzi wa kina zaidi kuhusu Epstein wakati huo.
WEF huandaa mkutano wake mkubwa kila mwaka mjini Davos, Uswisi, unaowakutanisha viongozi wa kisiasa na wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali duniani.
Katika taarifa yake Alhamisi, Brende amesema ameamua kujiuzulu baada ya kulitumikia shirika hilo kwa zaidi ya miaka minane, akieleza kuwa amefikia uamuzi huo baada ya kufikiria kwa makini. Amesema anaamini huu ni wakati sahihi kwa WEF kuendelea na kazi zake muhimu bila usumbufu wowote.
Jeffrey Epstein alipatikana na hatia mwaka 2008 kwa kosa la kushawishi mtoto mdogo kujihusisha na ukahaba, na alisajiliwa rasmi kama mhalifu wa makosa ya ngono. Hata hivyo, kutajwa kwa jina la mtu katika nyaraka zinazomhusu Epstein haimaanishi moja kwa moja kuwa amefanya kosa, na Brende hajawahi kushtakiwa kwa kosa lolote.
Wenyeviti wenza wa WEF, Andre Hoffmann na Larry Fink, wamemshukuru Brende kwa mchango wake mkubwa katika shirika hilo na kusema wanaheshimu uamuzi wake wa kujiuzulu.
Wanasiasa, watu maarufu, wafanyabiashara na hata familia za kifalme kutoka nchi mbalimbali wamekuwa wakichunguzwa kutokana na uhusiano wao na Epstein baada ya kutolewa kwa sehemu mpya ya nyaraka za uchunguzi wa Marekani. Nyaraka hizo zinajumuisha mamilioni ya barua pepe binafsi, picha na taarifa za FBI kuhusu Epstein, aliyefariki mwaka 2019 akiwa gerezani akisubiri kushtakiwa kwa makosa ya biashara ya ngono.
Soma Pia Bill Gates akiri kuisaliti ndoa yake na Melinda pamoja na kushirikiana na Jeffrey Epstein. Aomba radhi wafanyakazi wake
Ikumbukwe pia siku kadhaa nyuma Mwanzilishi mwenza t, Bill Gates, alikiri kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanawake wawili wa Kirusi wakati akiwa bado ameoa aliyekuwa mke wake, Melinda French Gates, ambapo pia ameomba radhi kwa uhusiano wake na mfadhili wa kifedha aliyewahi kutiwa hatiani kwa makosa ya unyanyasaji wa kingono, Jeffrey Epstein.
Source: BBC News
WEF iliagiza uchunguzi huru kumchunguza Brende baada ya nyaraka zinazomhusu Epstein kutolewa na Wizara ya Sheria ya Marekani. Brende amekiri kuwa alikutana na kula chakula cha jioni na Epstein mara tatu kati ya mwaka 2018 na 2019, na pia waliwasiliana kupitia barua pepe na ujumbe mfupi, lakini amesema hakuwa na ufahamu wowote kuhusu historia ya uhalifu wa Epstein wakati huo.
Brende, ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, pia amesema anajutia kutofanya uchunguzi wa kina zaidi kuhusu Epstein wakati huo.
WEF huandaa mkutano wake mkubwa kila mwaka mjini Davos, Uswisi, unaowakutanisha viongozi wa kisiasa na wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali duniani.
Katika taarifa yake Alhamisi, Brende amesema ameamua kujiuzulu baada ya kulitumikia shirika hilo kwa zaidi ya miaka minane, akieleza kuwa amefikia uamuzi huo baada ya kufikiria kwa makini. Amesema anaamini huu ni wakati sahihi kwa WEF kuendelea na kazi zake muhimu bila usumbufu wowote.
Jeffrey Epstein alipatikana na hatia mwaka 2008 kwa kosa la kushawishi mtoto mdogo kujihusisha na ukahaba, na alisajiliwa rasmi kama mhalifu wa makosa ya ngono. Hata hivyo, kutajwa kwa jina la mtu katika nyaraka zinazomhusu Epstein haimaanishi moja kwa moja kuwa amefanya kosa, na Brende hajawahi kushtakiwa kwa kosa lolote.
Wenyeviti wenza wa WEF, Andre Hoffmann na Larry Fink, wamemshukuru Brende kwa mchango wake mkubwa katika shirika hilo na kusema wanaheshimu uamuzi wake wa kujiuzulu.
Wanasiasa, watu maarufu, wafanyabiashara na hata familia za kifalme kutoka nchi mbalimbali wamekuwa wakichunguzwa kutokana na uhusiano wao na Epstein baada ya kutolewa kwa sehemu mpya ya nyaraka za uchunguzi wa Marekani. Nyaraka hizo zinajumuisha mamilioni ya barua pepe binafsi, picha na taarifa za FBI kuhusu Epstein, aliyefariki mwaka 2019 akiwa gerezani akisubiri kushtakiwa kwa makosa ya biashara ya ngono.
Soma Pia Bill Gates akiri kuisaliti ndoa yake na Melinda pamoja na kushirikiana na Jeffrey Epstein. Aomba radhi wafanyakazi wake
Ikumbukwe pia siku kadhaa nyuma Mwanzilishi mwenza t, Bill Gates, alikiri kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanawake wawili wa Kirusi wakati akiwa bado ameoa aliyekuwa mke wake, Melinda French Gates, ambapo pia ameomba radhi kwa uhusiano wake na mfadhili wa kifedha aliyewahi kutiwa hatiani kwa makosa ya unyanyasaji wa kingono, Jeffrey Epstein.
Source: BBC News