Kwanza naomba samahani nafikiri mtandao uko chini nimeshindwa kuweka haya katika maandishi yangu lakini nadhani ujumbe utafika.
kwa mchakato wa katiba unavyoenda nawapongeza sana UKAWA ingawa nao siwaungi mkono kwa asilimia zote kuliko waliobaki wanaojaribu kupotosha mfumo wa utawala wa nchi ili watanzania wachache waendelee kuwa mafisadi na kupora rasilimali za nchi, ili viongozi waendelee kutokuwa na maadili, ili wananchi waendelee kukosa haki mbele ya vyombo vyao. wapo mafisadi wakuu wanaowadanganya wananchi kuwa hatuwezi kupoteza mda kujadili mihimili ya utawala wa nchi kwa na kudai ni kupoteza kodi za wananchi na kudai wananchi wanataka kusikia ardhi, kusikia uchumi na mengine yanayowagusa.
Jambo la msingi hapa ni kujua kuwa hata ukiwa na mipango mizuri ya kiuchumi, afya na mengine lakini kama mfumo wa utawala ni mbaya mwananchi hawezi kupata lolote. Kwa mfumo tulio nao wa raisi kuteua kila kitu unasababisha wahuni kuunda vikundi vya kuatafuta madaraka na kumchagua mmoja wao akawanie nafasi ya juu. Akipata anawaleta wahuni wenzake kwa kuwateua kushika nyadhifa muhimu zote na nchi inaendeshwa kihuni. bila kuondoa mifumo hii Tanzania hata tupate kiongozi gani mzuri hawezi kutuletea maendeleo kwani vikundi hivi vya kihuni vinavyojulikana kama mitandao na majina mengine vina nguvu kuliko mtu mmoja hata kama ni kiongozi wa nchi.
Vikundi hivi ndivyo vinavyovuruga katika yetu kwa kujaribu kuzuia mifumo ya uwajibikaji, usawa na mifumo ya viongozi kuwatumikia wananchi isiwekwe katika katiba. Mambo muhimu katika katiba yetu ni swala la muungano lazima tuangalie ni mfumo gani unaokubalika kwa watanzania wa muungano. Kiongozi asiye na busara ndiye anayeweza kuingiza nchi katika machafuko kisa ni kutetea kile anachokiamini yeye. kama wananchi hawapendi muungano hata kama muungano unafaida nyingi kiasi gani faida hizo haziwezi kupatikana kwa watu wasioukubali. lakini jambo la pili ni kutenganisha mihimili ya utawala wa nchi kwa maana mahakama, serikali na bunge na kisha ukimaliza kuvitenganisha kwa kuondoa ushawishi wa chombo kimoja katika chombo kingine kufanya kazi zake (ushawishi huu unaweza kupitia upatikanaji wa fedha za kuendesha chombo au upatikanaji wa watumimishi na mambo mengine ikiwemo maslahi binafsi).
Tunatakiwa kubalansi nguvu za vyombo vya usalama. hapa vipo vyombo ambavyo lazima vitoke katika mikono ya serikali vyombo kama takukuru, tume ya maadili ya watumishi wa umma na ikiwezekana uongozi wa jeshi usiwe unateuliwa na raisi bali raisi yeye anaweza kuwa anamuapisha tu lakini viongozi wa mihimili ya nchi wanakutana kujadili mapendekezo ambayo kila chombo kinajadili na kupeleka mapendekezo na kufikia maamuzi ya pamoja na hivyo mkuu wa majeshi kuwa anapatikana kwa kuteliwa na vyombo vyote na si mmoja hivyo kutumia nguvu ya jeshi kulinda kiongozi mmoja anayemteua hata kama anafanya maasi kwa wananchi. mimi nafikiri ukimchukua mtu mwenye uzoefu akutengenezee kitu anatengeneza kwa uzoefu wake na uzoefu unaweza kuwa umejikita katika "corruption" na hili ndilo linalowakumba watanzania walio wengi wana uzoefu lakini hawana uzoefu katika kulisaidia taifa bali uzoefu katika kutumia fitina kupata madaraka, uzoefu katika kutumia ujanja kupora rasilimali za taifa, uzoefu katika kufoji matokeo sasa unawachukua watu hawa wakutengenezee katiba mpya unafikiri watafanya nini kama sio kutumia uzoefu wao huo tena wakiangalia kujiandalia makao.
Wengi wao hawana sifa bali wameingizwa wengine kwa rushwa zisizo za fedha, wengine kwa kujuana na makundi na kuweka mifumo mizuri ya utawala na uwajibikaji ni sawa na kukata matawi waliyoyakalia je ni nani yuko tayari kujiondoa mwenyewe katika mrija anaoutumia kunyonya taifa kama siyo kuondolewa.
Hatuwezi kupata katiba kwa mfumo huu bali katiba inaweza kutengenezwa na wataalamu na sio wanasheria tu bali kundi la wataalamu wa fani zote kukaa pamoja kusikiliza matakwa ya wananchi na kuiandika katiba kitaalamu kuweka mifumo ya kuwasaidia wananchi kupata kile wanachokitaka. mfano wananchi wanaweza kudai maswala ya uchumi yaingie katika katiba, ukimchukua mbumbumbu atapendekeza kuwepo na kifungu kinachozungumzia uchumi katika katiba lakini kwa mtaalamu ataangalia jinsi gani mfumo wa serikali unaathili uchumi, ataangalia ushiriki wa wananchi na wataweka mifumo ya kuwezesha uchumi kukua bila hata kutaja uchumi katika katiba.
Mbumbumbu anaweza kuweka kifungu cha kuzungumzia uchumi huku mfumo wa utawala unamuweka fisadi katika kuongoza kitengo cha uchumi au vyombo vya usalama vinafungwa na mifumo ya kiutawala ukimkata kigogo unaletewa memo au kufukuzwa kazi na hakuna chombo hata kimoja kinaweza kunyanyua mdomo kuhoji sasa kinachotakiwa katika katiba ni kutaja neon uchumi au ni kuweka mifumo ya kumuwezesha hata yule mdogo katika chombo cha usalama anaweza kumninginiza kigogo kama ana hatia na hakuna mpuuzi anaweza kuandika vikaratsi kutishia wala kunyanyua mdomo wote wakiogopana kulingana na mfumo ulivyo. tusitegemee mafisadi walioshikilia mifumo (bila kujali upande walipo) watuwekee mifumo mizuri bali katiba mpya ni wakati sasa wa kuweka mifumo ya utawala ambayo inafanya vyombo kutumikia wananchi na si matajiri wanaowapa sapoti viongozi au nafsi zao au mitandao yao
kwa mchakato wa katiba unavyoenda nawapongeza sana UKAWA ingawa nao siwaungi mkono kwa asilimia zote kuliko waliobaki wanaojaribu kupotosha mfumo wa utawala wa nchi ili watanzania wachache waendelee kuwa mafisadi na kupora rasilimali za nchi, ili viongozi waendelee kutokuwa na maadili, ili wananchi waendelee kukosa haki mbele ya vyombo vyao. wapo mafisadi wakuu wanaowadanganya wananchi kuwa hatuwezi kupoteza mda kujadili mihimili ya utawala wa nchi kwa na kudai ni kupoteza kodi za wananchi na kudai wananchi wanataka kusikia ardhi, kusikia uchumi na mengine yanayowagusa.
Jambo la msingi hapa ni kujua kuwa hata ukiwa na mipango mizuri ya kiuchumi, afya na mengine lakini kama mfumo wa utawala ni mbaya mwananchi hawezi kupata lolote. Kwa mfumo tulio nao wa raisi kuteua kila kitu unasababisha wahuni kuunda vikundi vya kuatafuta madaraka na kumchagua mmoja wao akawanie nafasi ya juu. Akipata anawaleta wahuni wenzake kwa kuwateua kushika nyadhifa muhimu zote na nchi inaendeshwa kihuni. bila kuondoa mifumo hii Tanzania hata tupate kiongozi gani mzuri hawezi kutuletea maendeleo kwani vikundi hivi vya kihuni vinavyojulikana kama mitandao na majina mengine vina nguvu kuliko mtu mmoja hata kama ni kiongozi wa nchi.
Vikundi hivi ndivyo vinavyovuruga katika yetu kwa kujaribu kuzuia mifumo ya uwajibikaji, usawa na mifumo ya viongozi kuwatumikia wananchi isiwekwe katika katiba. Mambo muhimu katika katiba yetu ni swala la muungano lazima tuangalie ni mfumo gani unaokubalika kwa watanzania wa muungano. Kiongozi asiye na busara ndiye anayeweza kuingiza nchi katika machafuko kisa ni kutetea kile anachokiamini yeye. kama wananchi hawapendi muungano hata kama muungano unafaida nyingi kiasi gani faida hizo haziwezi kupatikana kwa watu wasioukubali. lakini jambo la pili ni kutenganisha mihimili ya utawala wa nchi kwa maana mahakama, serikali na bunge na kisha ukimaliza kuvitenganisha kwa kuondoa ushawishi wa chombo kimoja katika chombo kingine kufanya kazi zake (ushawishi huu unaweza kupitia upatikanaji wa fedha za kuendesha chombo au upatikanaji wa watumimishi na mambo mengine ikiwemo maslahi binafsi).
Tunatakiwa kubalansi nguvu za vyombo vya usalama. hapa vipo vyombo ambavyo lazima vitoke katika mikono ya serikali vyombo kama takukuru, tume ya maadili ya watumishi wa umma na ikiwezekana uongozi wa jeshi usiwe unateuliwa na raisi bali raisi yeye anaweza kuwa anamuapisha tu lakini viongozi wa mihimili ya nchi wanakutana kujadili mapendekezo ambayo kila chombo kinajadili na kupeleka mapendekezo na kufikia maamuzi ya pamoja na hivyo mkuu wa majeshi kuwa anapatikana kwa kuteliwa na vyombo vyote na si mmoja hivyo kutumia nguvu ya jeshi kulinda kiongozi mmoja anayemteua hata kama anafanya maasi kwa wananchi. mimi nafikiri ukimchukua mtu mwenye uzoefu akutengenezee kitu anatengeneza kwa uzoefu wake na uzoefu unaweza kuwa umejikita katika "corruption" na hili ndilo linalowakumba watanzania walio wengi wana uzoefu lakini hawana uzoefu katika kulisaidia taifa bali uzoefu katika kutumia fitina kupata madaraka, uzoefu katika kutumia ujanja kupora rasilimali za taifa, uzoefu katika kufoji matokeo sasa unawachukua watu hawa wakutengenezee katiba mpya unafikiri watafanya nini kama sio kutumia uzoefu wao huo tena wakiangalia kujiandalia makao.
Wengi wao hawana sifa bali wameingizwa wengine kwa rushwa zisizo za fedha, wengine kwa kujuana na makundi na kuweka mifumo mizuri ya utawala na uwajibikaji ni sawa na kukata matawi waliyoyakalia je ni nani yuko tayari kujiondoa mwenyewe katika mrija anaoutumia kunyonya taifa kama siyo kuondolewa.
Hatuwezi kupata katiba kwa mfumo huu bali katiba inaweza kutengenezwa na wataalamu na sio wanasheria tu bali kundi la wataalamu wa fani zote kukaa pamoja kusikiliza matakwa ya wananchi na kuiandika katiba kitaalamu kuweka mifumo ya kuwasaidia wananchi kupata kile wanachokitaka. mfano wananchi wanaweza kudai maswala ya uchumi yaingie katika katiba, ukimchukua mbumbumbu atapendekeza kuwepo na kifungu kinachozungumzia uchumi katika katiba lakini kwa mtaalamu ataangalia jinsi gani mfumo wa serikali unaathili uchumi, ataangalia ushiriki wa wananchi na wataweka mifumo ya kuwezesha uchumi kukua bila hata kutaja uchumi katika katiba.
Mbumbumbu anaweza kuweka kifungu cha kuzungumzia uchumi huku mfumo wa utawala unamuweka fisadi katika kuongoza kitengo cha uchumi au vyombo vya usalama vinafungwa na mifumo ya kiutawala ukimkata kigogo unaletewa memo au kufukuzwa kazi na hakuna chombo hata kimoja kinaweza kunyanyua mdomo kuhoji sasa kinachotakiwa katika katiba ni kutaja neon uchumi au ni kuweka mifumo ya kumuwezesha hata yule mdogo katika chombo cha usalama anaweza kumninginiza kigogo kama ana hatia na hakuna mpuuzi anaweza kuandika vikaratsi kutishia wala kunyanyua mdomo wote wakiogopana kulingana na mfumo ulivyo. tusitegemee mafisadi walioshikilia mifumo (bila kujali upande walipo) watuwekee mifumo mizuri bali katiba mpya ni wakati sasa wa kuweka mifumo ya utawala ambayo inafanya vyombo kutumikia wananchi na si matajiri wanaowapa sapoti viongozi au nafsi zao au mitandao yao