BOOM Halitoshi Kununua Computer

Kwa wengi boom ni mtaji wa biashara wakiwa wanasoma. Kuna kijana alifanya chumba na kwenda kuchukua mchele mikoani a kawa anatumia mama bailie, sliketa kijana kutoka kijijini kwa shughuli hiyo.
alieelewa naomba anitagi
 
Labda sana unataka kujua nini? Specifically

Point ni kwamba Boom halitoshi kununua laptop, wewe ukasema linatosha kutegemeana na mtu, ukaorodhesha vitu ulivyofanya kwa kutumia boom.

Nimeuliza hayo maswali ili nione uhalisia wa kweli ulitumia Boom pekee au kuna kipato zaidi, na ni kwa mwaka ambao ulikuwa hujafungua salon.
 
Kwa wengi boom ni mtaji wa biashara wakiwa wanasoma. Kuna kijana alifanya chumba na kwenda kuchukua mchele mikoani a kawa anatumia mama bailie, sliketa kijana kutoka kijijini kwa shughuli hiyo.
Naona kuna somo hapa lakini....
 
Duh!, nakumbuka enzi zangu nilipata msoto sana. nikanunua tena ya bei rahisi tu 380,000tzs...duh, acha niyumbe haloo. pasi ndefu zikawa kwa wingi lohh!. Pesa za shule ukiwa unasaidia na nyumbani weeee, ukanunua na PC haloo utapiga sana miruzi chuoni hahaha
 

Wale wanaosemaga zinatosha ndo wanaoziba loan board kuongeza kiwango...
 
Kwa wewe halikutosha mie lilitosha. Boom la kuanza mwaka enzi zetu maana sasa sijui mnamabadiliko imeongezeka ilikuwa pesa ya kujikimu pamoja na stationary kwa pamoja ckumbuki vema ilikuwa laki 6 hv plus.

Nitashindwaje nunua laptop ya laki 460000/= nikabaki na laki 2. Utasema laki 2 utakulaje hapo ndio tunatofautiana budget

Udom chakula ilikuwa cheap, hostel cheap, mia tano kwa siku, hatukuwa na show za kusafiri mjini kwenye madaladala bila sababu mwezi mzima waweza usinione mjini.

Sikuwa ba tabia ya kununua handout notes. Nilijua nakozipata nakusoma. So mjini shule bana
 

Mkuu lengo ni kuelimishana, na kuwashauri wadogo zetu nini kifanyike ili waweze kuishi kwa kujibana na Boom hilo hilo, ungeweka mchanganuo vizuri ungesaidia sana.

Tupe mchanganuo kwa kipindi chenu hicho hicho, 600,000 - 460,000 = 140,000/= siyo 200,000.

Hostel 500 kwa siku, kwa semister ni 500*120 = 60,000/=, kwenye 140,000 tayari imebaki 80,000/=.

Umeongezea kitu umekiita Mjini Shule kwenye handouts.

Mkuu wewe tupe ufafanuzi mzuri ili tujue tunawashauri nini wadogo zetu.
 
Wale wanaosemaga zinatosha ndo wanaoziba loan board kuongeza kiwango...
WAWAONGEZE, PESA ZENYEWE ZA MKOPO. yaani kama mahitaji ya ziada hufanyi..inatosha, ila ukipiga hesabu vibaya na ukatumia kulala na demu gesti mkatanua...hakianani hiyo pesa haitoshi hahaha!. ila inapaswa kuongezwa sio km hivi sasa
 
WAWAONGEZE, PESA ZENYEWE ZA MKOPO. yaani kama mahitaji ya ziada hufanyi..inatosha, ila ukipiga hesabu vibaya na ukatumia kulala na demu gesti mkatanua...hakianani hiyo pesa haitoshi hahaha!. ila inapaswa kuongezwa sio km hivi sasa

Sijakuelewa utachotaka kusema!

Inatosha au haitoshi?
 
Nmekwambia laki 6 plus na hostel jua sio kila semister unalipa kuna vitu ukilipia mwanzo wa mwaka unamaliza maana yake semister ya pili waweza balance pesa. Nipo kazini saiz muda wa kuandika taratibu unabana badae nikipata nafasi siku njema mkuu
 
inatosha km utaamua kusoma kwa hali ya chini, haitoshi km utataka usome kwa raha ukiwa na vitendea kazi vyote uvitakavyo

Toa msimamo, je waongeze ili watu wasome kwa raha na vitendea kazi vyote au wanafunzi waendelee kusoma kwa hali ya chini?
 
Toa msimamo, je waongeze ili watu wasome kwa raha na vitendea kazi vyote au wanafunzi waendelee kusoma kwa hali ya chini?
hata wao wanaelewa haya, nadhani hawana hela. Inatakiwa iongezwe, hazina inasemaje kuhusu kuongeza?, ujue bado hawana uwezo wa kuhudumia wanafunzi wote wenye sifa huko vyuoni, je wataweza kustahimili kuongeza kwa hao wachache wanaowahudumia?
 
Nmekwambia laki 6 plus na hostel jua sio kila semister unalipa kuna vitu ukilipia mwanzo wa mwaka unamaliza maana yake semister ya pili waweza balance pesa. Nipo kazini saiz muda wa kuandika taratibu unabana badae nikipata nafasi siku njema mkuu

Shukrani mkuu, nitasubiri huo mchanganuo, na nitapenda kama utatumia correct figures.

Nina mdogo wangu ananipiga mizinga kila mara, nataka nimwoneshe hesabu ya jinsi anavyoweza kujibana.
 
Umeongea bila kufikiri mkuu uwezi kutumia pc miaka minne kwa kuifadhi notice pekee labda unataka kuwa msomi wa cheti usiye na maarifa ushauri mbaya sana kwa elimu yetu hapa tanzania kama unasoma civil engineering au electrical engineering na computer science uwezi kuwa na pc ya notice labda unatangaza biashara sema watanunua wasomaji wa notice
 
Kwa wengi boom ni mtaji wa biashara wakiwa wanasoma. Kuna kijana alipanga chumba na kwenda kuchukua mchele mikoani na Kuwaitis mama ntilie, alileta kijana kutoka kijijini kwa shughuli hiyo.
Chuo unasoma udaktari haya mambo ya biashara utayafanyaje??
 
inatosha km utaamua kusoma kwa hali ya chini, haitoshi km utataka usome kwa raha ukiwa na vitendea kazi vyote uvitakavyo
True mkuu,na inategemea unasoma nini,huwezi kuwa unasoma kozi za afya kisha unakula mlo mmoja,inabidi mazingira yawe mazuri..overall hela ni ya kujikimu
 
kwa udom ukiamua kujibana kwa kipindi nilichosoma unatumia tu 60,000 kwa mwezi kwenye kula, hio hela unampa mama ntilie, unakula tu kwake. Tena chakula kizuri kuliko cafeteria, unakula ugali na mboga saba.

Boom kipindi hiko lilikuwa 7500 kwa siku au 225,000 kwa mwezi au 900,000 kwa semester, plus 200,000 ya stationary inakuja 1.1m.

Fanya mahesabu sasa unajibana sana
-240,000 chakula
-60,000 malazi

hapo una laki 8 ipo mfukoni, sijui bei za mama ntilie/wajasi kwa sasa ila hazitatofautiana sana.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…