BOMU la LISSU jijini ARUSHA

BOMU la LISSU jijini ARUSHA

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Wakili Msomi Tundu Antipas Mughwai Lissu ameacha mwangwi kwenye Mkutano wa Mawakili-AICC Arusha. Ameonesha jinsi asivyotetereka na kusimamia anachokiamini. Amethubutu kusema na kuwaita Mawakili 'waoga' na watetezi wa vibovu.

Katika moja ya michango yake,Wakili Lissu alimuumbua Jaji Dr.Feuz Twaib(ambaye pia Mwalimu Shule ya Sheria ya Tanzania na Wakili) kwa kumwambia kuwa punde tu,miezi michache iliyopita,aliandika hukumu 'mbovu' na isiyostahili ambayo 'imechanwachanwa' na Majaji wa Mahakama wa Rufani na kutupiliwa mbali.Hukumu a Jaji Twaib ilikuwa ni kwenye kesi ya Yusuph Manji dhidi ya Kampuni moja ya Saudi Arabia.

Uchunguzi wa nyaraka za Wakili Tundu Lissu unaonesha kuwa katika kesi hiyo iliyokuwa mbele ya Jaji Rugazia wa Mahakama Kuu,pande husika za kesi zilikubaliana nje ya Mahakama( Settlement out of Court) na Jaji Rugazia akaridhia makubaliano hayo na kuyafanya Amri ya Mahakama. Ni utaratibu unaokubalika kisheria.

Siku si nyingi,Wakili Majura Magafu alijitokeza Mahakamani,kwa niaba ya Manji kuomba Marejeo(Review) ya Makubaliano hayo. Kisheria, Marejeo hufanywa na Jaji aliyeamua kesi husika.Jaji Twaib anajua hilo fika. Jaji Twaib,akiwa hausiki na Amri ya mwanzoni,alitengua Makubaliano ya pande za kesi. Akafanya 'blanda'. Akafanya jambo haramu kisheria.

Wakili Lissu hakuogopa uwepo wa Majaji na Mawakili Waandamizi kama vile Jaji Dr.Feuz Twaib,Prof. M.K.Wambali,Jaji Joseph Sinde Warioba,Jaji Mstaafu Thomas Mihayo,Jaji Victor Makaramba,Wakili na Rais wa Mawakili Tanganyika Francis Stolla na wengineo. Mkutano ukageuzwa Semina. Lissu akatoa mafunzo thabiti.

Aliposimama Jaji Twaib, ambaye alionekana mnyonge, aliwaomba Mawakili waende wakaisome hukumu husika na kujiridhisha na tuhuma za Lissu.Katika siku nilizojiona sina maana katika jamii hii,siku hii ya Lissu inaoongoza. Wakili Lissu akanifanya nirudi Dar kwa basi badala ya ndege kama nilivyopanga.
 
aisee kumbe majaji na mawakili wapo jando arusha eenh!
 
Ulikuwa ni Mkutano wa Mawakili.Umeshaisha.Kuna Majaji ambao pia ni Mawakili.Ndio maana wakawepo Mkutanoni
 
Wakili Msomi Tundu Antipas Mughwai Lissu ameacha mwangwi kwenye Mkutano wa Mawakili-AICC Arusha. Ameonesha jinsi asivyotetereka na kusimamia anachokiamini. Amethubutu kusema na kuwaita Mawakili 'waoga' na watetezi wa vibovu.

Katika moja ya michango yake,Wakili Lissu alimuumbua Jaji Dr.Feuz Twaib(ambaye pia Mwalimu Shule ya Sheria ya Tanzania na Wakili) kwa kumwambia kuwa punde tu,miezi michache iliyopita,aliandika hukumu 'mbovu' na isiyostahili ambayo 'imechanwachanwa' na Majaji wa Mahakama wa Rufani na kutupiliwa mbali.Hukumu a Jaji Twaib ilikuwa ni kwenye kesi ya Yusuph Manji dhidi ya Kampuni moja ya Saudi Arabia.

Uchunguzi wa nyaraka za Wakili Tundu Lissu unaonesha kuwa katika kesi hiyo iliyokuwa mbele ya Jaji Rugazia wa Mahakama Kuu,pande husika za kesi zilikubaliana nje ya Mahakama( Settlement out of Court) na Jaji Rugazia akaridhia makubaliano hayo na kuyafanya Amri ya Mahakama. Ni utaratibu unaokubalika kisheria.

Siku si nyingi,Wakili Majura Magafu alijitokeza Mahakamani,kwa niaba ya Manji kuomba Marejeo(Review) ya Makubaliano hayo. Kisheria, Marejeo hufanywa na Jaji aliyeamua kesi husika.Jaji Twaib anajua hilo fika. Jaji Twaib,akiwa hausiki na Amri ya mwanzoni,alitengua Makubaliano ya pande za kesi. Akafanya 'blanda'. Akafanya jambo haramu kisheria.

Wakili Lissu hakuogopa uwepo wa Majaji na Mawakili Waandamizi kama vile Jaji Dr.Feuz Twaib,Prof. M.K.Wambali,Jaji Joseph Sinde Warioba,Jaji Mstaafu Thomas Mihayo,Jaji Victor Makaramba,Wakili na Rais wa Mawakili Tanganyika Francis Stolla na wengineo. Mkutano ukageuzwa Semina. Lissu akatoa mafunzo thabiti.

Aliposimama Jaji Twaib, ambaye alionekana mnyonge, aliwaomba Mawakili waende wakaisome hukumu husika na kujiridhisha na tuhuma za Lissu.Katika siku nilizojiona sina maana katika jamii hii,siku hii ya Lissu inaoongoza. Wakili Lissu akanifanya nirudi Dar kwa basi badala ya ndege kama nilivyopanga.

Tuwekee hotuba nzima ya huyu mteule na mtetezi wa wanyonge
 
bravo lissu hajaogopa vituko vya majaji kama watamfanyia makusudi katika kesi zake
amekuwa mkweli na hajaogopa kwa vile yeye ni mtu wa haki na mkweli
muda wa kuwanyenyekea majaji wanaoandika hukumu 3 kwa mwaka umeisha
muda wa kuwanyenyekekea majaji wanaoahirisha kesi hata kama ni mention kwa miezi 4 umeisha
muda wa kuwanyenyekea majaji wanaopanga kesi kwa siku bila kuweka muda maalumu umeisha
kwani mawakili wanajikuta wanafika asbh mahakamani na kuondoka saa 10 kwa kusubiri
pawepo sasa tume ya kuratibu utendaji wa majaji na kuwawajibisha wazembe wanaopenda kuitwa waheshimiwa
lakini utendaji wao kazi ni zero.
 
Utamu ukiijua mizania ya sheria bwana, hivi kwanini tusiwe tunaiga vitu kama hivi vya msingi? Tuachane na mambo yasiokua na tija maishani, kama vile kumaliza mzinga wa konyagi, kula mbuzi mzima na mkia maini sijui kuku na mayai manyoya takataka kibao.
 
Kuna kitu hapa nimejifunza kumbe kuna Majaji ambao ni mawakili!! ok i read between the line learned Brothers.
 
dah kwakweli nimesikitika sana , jaji twaibu namheshimu sana pia kama mwalimu wangu, anauwezo mzuri sana, hili suala nalazimika kulifuatilia kiundani.
 
dah kwakweli nimesikitika sana , jaji twaibu namheshimu sana pia kama mwalimu wangu, anauwezo mzuri sana, hili suala nalazimika kulifuatilia kiundani.
Fanya hivyo kijana.Amekufundisha UDSM au Law School of Tanzania?
 
unadhani kuitwa jaji ni ujanja ujanja,wajibu sasa risasi za bwana lisu,ujanja hautakiwi jamani,sasa familia za hao majaji zinajifunza nini
 
..." Heri Dr Slaa awe Rais kuliko Tundu Lissu kuwa mbunge...." !

JK Campaign Rally 2010.
 
Kuna kitu hapa nimejifunza kumbe kuna Majaji ambao ni mawakili!! ok i read between the line learned Brothers.

Huwezi kuvaa kofia mbili kutakuwa na conflicts of interest walikuwaga mawakili kabla hawajateuliwa kuwa majaji so ile kofia ya uwakili wameivua kwenye mkutano wanaenda kama waalikwa
 
Mhe, Wakili Antipas Tundu Lissu (MB)-Huyu ndiye waziri wangu wa sheria na katiba,chezeya lissu wewe
 
unadhani kuitwa jaji ni ujanja ujanja,wajibu sasa risasi za bwana lisu,ujanja hautakiwi jamani,sasa familia za hao majaji zinajifunza nini
Baba kaenda kazini Arusha,kumbe wasijue lissu yuko anampiga makwenzi
 
Back
Top Bottom