Bomoabomoa Arusha: Wakazi 3,000 Arumeru kubomolewa makazi

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,311
3,341
arusha(3).jpg


Zoezi la kubomoa nyumba zilizojengwa kwenye maeneo yasiyo ruhusiwa kisheria linatarajiwa kuhamia mkoani Arusha wakati wowote kuanzia sasa na wananchi wakiwemo waliojenga kwenye vyanzo vya maji wameshaanza kupewa taarifa.

ITV imeshuhudia kazi ya kuweka alama kwenye nyumba zilizojengwa kwenye vyanzo vya maji katika wilaya ya Arumeru zikiwekewa alama na wananchi wakitakiwa kuanza kuzibomoa wenyewe ili kunusuru mali zao.

Hata hivyo baadhi ya wananchi hao wameiomba serikali kutumia vyombo vyake kuwawajibisha watendaji wa serikali waliochangia na kuruhusu maeneo yasiyoruhusiwa kisheria kujengwa na ikiwezekana walipe hasara inayojitokeza kwani wamefanya hivyo wakiwa wanajua wazi kuwa ni kosa.

Baadhi ya viongozi wa kata ikiwemo ya Kerai, Bw John Edward ambaye ni diwani pamoja na kukiri kuwepo kwa watendaji wanaoshiriki kuwasababishia wananchi hasara ameitaka serikali kuangalia namna ya kuwasaidia wananchi ambao walikuwepo kwenye maeneo hayo kabla ya sheria kupitishwa.

Arumeru ndio wilaya yenye vyanzo vya maji vinavyotegemewa na asilimia kubwa ya wananchi wa jiji la Arusha, na wilaya za jirani ikiwemo Monduli na Longido na ni miongoni mwa zinazokabiliwa na tatizo kubwa ya uharibifu wa mazingira.


================
Arusha. Zaidi ya wakazi 3,000 wa Kata ya Kiranyi Wilaya ya Arumeru mkoani hapa, wameamriwa na Mamlaka ya Bonde la Pangani kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji ya Mji Mdogo wa Ngaramtoni kubomoa nyumba zao kwa kujenga kwenye chanzo cha maji.

Meneja wa Mamlaka ya Maji Mji Mdogo wa Ngaramtoni (Ngauwsa), Clayson Kimaro alisema nyumba ambazo zimewekwa alama ya X zinazotakiwa kubomolewa kwa kuwa ziko ndani ya mita 60 kutoka kwenye chanzo hicho ambacho kwa mujibu wa sheria hazipaswi kuwapo.

Alisema wakazi hao wamekiuka Sheria ya Mazingira namba 20 ya mwaka 2004 na Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali Maji namba 11 ya mwaka 2009 inayozuia maendelezo ya ujenzi na kilimo kwenye eneo la mita 60 kutoka kingo za maji.

Ofisa wa Bonde la Pangani mkoani Arusha, Joel Lao alisema kulinda vyanzo vya maji ni wajibu wa kila mwananchi kama inavyotamkwa kwenye Sera ya Maji ya mwaka 2002 na kazi ya mamlaka ya bonde hilo ni usimamizi wa sheria.

Alisema athari za kuwapo kwa shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo vya maji zinaweza kuvikaviusha na kusababisha magonjwa ya milipuko yanayosababishwa na maji machafu kutiririkia kwenye vyanzo vya maji.

Baadhi ya wakazi hao, Hashim Kassimu na Mwanamkuu Shabani walisema unalenga kuwarejesha katika umaskini kutokana na kudunduliza fedha na kujenga makazi yao sehemu hiyo.

“Umaskini unatunyemelea upya. Tunaanza upya maisha,” alisema Kassimu.

Diwani wa Kata ya Kiranyi, John Seneu alisema wakazi hao wanaodaiwa kuvamia eneo hilo walinunua na kupata vibali kutoka Serikali za vijiji na wengine walizaliwa maeneo hayo, hivyo Serikali itumie busara kufanya uamuzi.

Chanzo: Mwananchi

 
Last edited by a moderator:
WanaJF,

Kama wote tujuavyo serikali ipo katika jitihada ya kuondoa wakazi wote waishio kinyume cha sheria za nchi hasa wale wakazi wa mabondeni, wanaoishi kwenye maeneo ya wazi na waliojenga kwenye fukwe na maeneo yasiyo ya kwao kihalali.

Zoezi hili lililoteka media kwa sasa linaelekezwa nguvu katika mkoa wa Arusha baada ya Dar kuonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wake.

Hadi sasa hatua ya kupiga alama ya 'BOMOA' au X ndio imeanza rasmi kwenye baadhi ya maeneo jijini Arusha, hali ambayo imepokelewa kwa vilio na majonzi kwa baadhi ya wananchi hao wanaojiita 'makamanda'.

Aidha, taarifa inasema mbunge wa Arusha mjini anatarajiwa kuitisha maandamano makubwa jijini Arusha kupinga hatua hiyo ya serikali kuwabomolea wananchi wake hao waishio mabondeni.

==============
Arusha
Zaidi ya wakazi 3,000 wa Kata ya Kiranyi Wilaya ya Arumeru mkoani hapa, wameamriwa na Mamlaka ya Bonde la Pangani kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji ya Mji Mdogo wa Ngaramtoni kubomoa nyumba zao kwa kujenga kwenye chanzo cha maji.

Meneja wa Mamlaka ya Maji Mji Mdogo wa Ngaramtoni (Ngauwsa), Clayson Kimaro alisema nyumba ambazo zimewekwa alama ya X zinazotakiwa kubomolewa kwa kuwa ziko ndani ya mita 60 kutoka kwenye chanzo hicho ambacho kwa mujibu wa sheria hazipaswi kuwapo.

Alisema wakazi hao wamekiuka Sheria ya Mazingira namba 20 ya mwaka 2004 na Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali Maji namba 11 ya mwaka 2009 inayozuia maendelezo ya ujenzi na kilimo kwenye eneo la mita 60 kutoka kingo za maji.

Ofisa wa Bonde la Pangani mkoani Arusha, Joel Lao alisema kulinda vyanzo vya maji ni wajibu wa kila mwananchi kama inavyotamkwa kwenye Sera ya Maji ya mwaka 2002 na kazi ya mamlaka ya bonde hilo ni usimamizi wa sheria.

Alisema athari za kuwapo kwa shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo vya maji zinaweza kuvikaviusha na kusababisha magonjwa ya milipuko yanayosababishwa na maji machafu kutiririkia kwenye vyanzo vya maji.

Baadhi ya wakazi hao, Hashim Kassimu na Mwanamkuu Shabani walisema unalenga kuwarejesha katika umaskini kutokana na kudunduliza fedha na kujenga makazi yao sehemu hiyo.

“Umaskini unatunyemelea upya. Tunaanza upya maisha,” alisema Kassimu.

Diwani wa Kata ya Kiranyi, John Seneu alisema wakazi hao wanaodaiwa kuvamia eneo hilo walinunua na kupata vibali kutoka Serikali za vijiji na wengine walizaliwa maeneo hayo, hivyo Serikali itumie busara kufanya uamuzi.

Chanzo: Mwananchi
 
Last edited by a moderator:
Wanataka waendelee kuishi mabondeni kama kenge na vyura??? (nimejiuliza mwenyewe)
 
WanaJF,

Kama wote tujuavyo serikali ipo katika jitihada ya kuondoa wakazi wote waishio kinyume cha sheria za nchi hasa wale wakazi wa mabondeni, wanaoishi kwenye maeneo ya wazi na waliojenga kwenye fukwe na maeneo yasiyo ya kwao kihalali.

Zoezi hili lililoteka media kwa sasa linaelekezwa nguvu katika mkoa wa Arusha baada ya Dar kuonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wake.

Hadi sasa hatua ya kupiga alama ya 'BOMOA' au X ndio imeanza rasmi kwenye baadhi ya maeneo jijini Arusha, hali ambayo imepokelewa kwa vilio na majonzi kwa baadhi ya wananchi hao wanaojiita 'makamanda'.

Aidha, taarifa inasema mbunge wa Arusha mjini anatarajiwa kuitisha maandamano makubwa jijini Arusha kupinga hatua hiyo ya serikali kuwabomolea wananchi wake hao waishio mabondeni.
Kwa akili yako ndogo lema anawajibika kwa wana arusha kuliko mkuu wa mkoa siyo?nyani we
 
WanaJF,

Kama wote tujuavyo serikali ipo katika jitihada ya kuondoa wakazi wote waishio kinyume cha sheria za nchi hasa wale wakazi wa mabondeni, wanaoishi kwenye maeneo ya wazi na waliojenga kwenye fukwe na maeneo yasiyo ya kwao kihalali.

Zoezi hili lililoteka media kwa sasa linaelekezwa nguvu katika mkoa wa Arusha baada ya Dar kuonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wake.

Hadi sasa hatua ya kupiga alama ya 'BOMOA' au X ndio imeanza rasmi kwenye baadhi ya maeneo jijini Arusha, hali ambayo imepokelewa kwa vilio na majonzi kwa baadhi ya wananchi hao wanaojiita 'makamanda'.

Aidha, taarifa inasema mbunge wa Arusha mjini anatarajiwa kuitisha maandamano makubwa jijini Arusha kupinga hatua hiyo ya serikali kuwabomolea wananchi wake hao waishio mabondeni.
Tunampongeza lema kwa kuwa karibu na wananchi wake kuliko hata marehemu rc
 
Kwani Lema si ni kamanda wa ukawa? Anapagawa nini wakati ILANI yao inatekelezwa?
 
habari imekaa kimipasho zaidi. Mbona husemi bomoa bomoa ya Dodoma ambayo mkoa mzima wabunge wake mmewachagua ni wa CCM na mmebomolewa? kweli ndio mana Mirembe ipo Dodoma kwa ajili ya watu kama nyinyi.
 
Ndio imeingia Arusha lakini si kwa wanaoishi mabondeni, Arusha hakuna sehemu inayoitwa mabondeni ila wanabomolewa waliojenga kwenye vyanzo vya maji, na kuhusu maandamano, hili neno limeshapitwa na wakati kama ilikuwa kashfa ya kumnyima Lema ubunge ilishindwa, Lema hajaitisha maandamano wala hata itisha maandamano kwa jambo la msingi, acha kukurupukia mambo kwa kuwa una chuki na MAKAMANDA wa Arusha wewe.
 
Sasa wanabomoa wakati manispaa viwanja vimepimwa eneo moja tu!



View attachment 315174

Zoezi la kubomoa nyumba zilizojengwa kwenye maeneo yasiyo ruhusiwa kisheria linatarajiwa kuhamia mkoani Arusha wakati wowote kuanzia sasa na wananchi wakiwemo waliojenga kwenye vyanzo vya maji wameshaanza kupewa taarifa.

ITV imeshuhudia kazi ya kuweka alama kwenye nyumba zilizojengwa kwenye vyanzo vya maji katika wilaya ya Arumeru zikiwekewa alama na wananchi wakitakiwa kuanza kuzibomoa wenyewe ili kunusuru mali zao.

Hata hivyo baadhi ya wananchi hao wameiomba serikali kutumia vyombo vyake kuwawajibisha watendaji wa serikali waliochangia na kuruhusu maeneo yasiyoruhusiwa kisheria kujengwa na ikiwezekana walipe hasara inayojitokeza kwani wamefanya hivyo wakiwa wanajua wazi kuwa ni kosa.

Baadhi ya viongozi wa kata ikiwemo ya Kerai, Bw John Edward ambaye ni diwani pamoja na kukiri kuwepo kwa watendaji wanaoshiriki kuwasababishia wananchi hasara ameitaka serikali kuangalia namna ya kuwasaidia wananchi ambao walikuwepo kwenye maeneo hayo kabla ya sheria kupitishwa.

Arumeru ndio wilaya yenye vyanzo vya maji vinavyotegemewa na asilimia kubwa ya wananchi wa jiji la Arusha, na wilaya za jirani ikiwemo Monduli na Longido na ni miongoni mwa zinazokabiliwa na tatizo kubwa ya uharibifu wa mazingira.




Vyanzo vya maji
 
WanaJF,

Kama wote tujuavyo serikali ipo katika jitihada ya kuondoa wakazi wote waishio kinyume cha sheria za nchi hasa wale wakazi wa mabondeni, wanaoishi kwenye maeneo ya wazi na waliojenga kwenye fukwe na maeneo yasiyo ya kwao kihalali.

Zoezi hili lililoteka media kwa sasa linaelekezwa nguvu katika mkoa wa Arusha baada ya Dar kuonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wake.

Hadi sasa hatua ya kupiga alama ya 'BOMOA' au X ndio imeanza rasmi kwenye baadhi ya maeneo jijini Arusha, hali ambayo imepokelewa kwa vilio na majonzi kwa baadhi ya wananchi hao wanaojiita 'makamanda'.

Aidha, taarifa inasema mbunge wa Arusha mjini anatarajiwa kuitisha maandamano makubwa jijini Arusha kupinga hatua hiyo ya serikali kuwabomolea wananchi wake hao waishio mabondeni.

==============


Chanzo: Mwananchi
Kata ya Kiranyi haipo kwenye Jimbo la Lema, ipo kwa Meseiyaki. Muda wa Propaganda ulishapita, jifunze kuendana na Muda. Update your Head.
 
Back
Top Bottom