Hata mimi sijaelewa maana ya heading yako Kuwa Mungu hakunyimi vyote. Maana kwa mtazamo wangu ni kuwa kutokana na heading yako ninaweza kunyongoloa kuwa au Imakulata na kasoro ya kimaumbile, au sura yake mbaya, au mapungufu yoyote katika mwili wake, hivyo basi pamoja na kuwa na kasoro hizo lakini bado alikuwa anafanya vizuri sana darasani hivyo kupelekea kuwa mwanafunzi bora katika mtihani yake ya kuhitimu.
Huu ni mtizamo wangu pengine mwenye mada atatufafanulia zaidi. kama hana ufafanuzi basi awe anaangali "heading" inayoendana na thread.
Pamoja na hayo Hongera sana IMACULATE Mungu akujalie na akutangulie katika safari mpya unayoianza ya elimu dunia.