Bila Mungu taifa litaangamia

Bila Mungu taifa litaangamia

Wa Busiya

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
326
Reaction score
67
MUNGU ni neno linalomaanisha Hali ya UKUU na UWEZO usio na kikomo na ndani yake UUMBAJI wa vitu vyote.
MUNGU ANAAGIZA WANADAMU WAPENDANE WAO KWA WAO, WALA WASIUANE MAANA MUNGU hana radhi na wapumbavu. Tulipofika kama Taifa hatuna msaada tena zaidi ya kumlilia Mungu kwa kuwa sasa hivi ukisema ukweli utaitwa "Mchochezi" Haki na mawazo ya raia yanapozimwa kwa mtindo wa mwaka '47' ni kuliangamiza taifa. Maana haki huinua taifa lakini dhambi ni chukizo kwa kila mtu. Wacha Mungu tusimameni kuiombea nchi hii na kuchukua hatua za kusimama katika nafasi za uongozi bila kujali misingi ya dini. Naamini wapo watu wa madhehebu na dini mbalimbali wanaomcha Mungu wao kwa dhati
Mungu iepushe nchi hii na roho na mauti na machafuko ya kijamii
 
V.I.Lenin aliwahi kusema haya" Njia pekee ya kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii nilazma kufanya mapinduz dhid ya tabaka tawala dharimu lililokumbatia unyonyaji na unyanyasaji kwa wananchi wake. Wafanyakaz na wakulima wanapaswa kuungana na kulipindua tabaka dharimu" Huu mgogoro wa mtwara kiwe chanzo cha watanzania kujikomboa kutokana na unyonyaji,ubadhilifu wa mali ya umma,kunyanyaswa kwa wananchi na uöngozi mbaya tuelewe kitu kimoja kuwa nguvu ya umma ni imara kuliko nguvu ya dora. UNGANENI MKIZIPATA BUNDUKI
 
utambue Kuwa wanasiasa Ndio chanzo cha vurugu...
 
Kauli zinazotolewa na viongozi kuepusha uvunjaji wa amani hazina hata tone la kumwogopa na kumwomba MUNGU atuepushe na yanayotokea. Yamejaa ubabe mtupu na hayana Uzalendo.Ningependa kusikia tuunde tume ya kurudisha amani ya nchi inayopotea Kila kukicha mifano hai ya amani kupotea:- Polisi wakamatwa na bangi,Polisi wakutw na fuvu la kichwa,viongozi wa dini kuwawa, bomu lalipuka kanisani, nyumba za wanasiasa mtwara zachomwa, waandishi kutekwa na wengine kuwawa mikataba ya kutokuwa wazi,ajali za Kila kukicha Rushwa iliyokithiri na mengineyo mengi
 
Back
Top Bottom