Bibi wa Deo Soka: Nashindwa kula nabaki kulia tu, waniletee hata maiti ya mjukuu wangu nikazike

Bibi wa Deo Soka: Nashindwa kula nabaki kulia tu, waniletee hata maiti ya mjukuu wangu nikazike

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Ukiyasikia maneno anayoyasema huyu bibi yake na Soka ambaye alimlea tangu mdogo hadi anakuwa inaumiza sana.

Soka amepotea imepita mwaka na miezi 2 ambapo alitekwa Agosti 18, 2024 familia yake haifahamu wapi amepelekwa mtoto wao. Nyie watekaji mliomteka Soka kumbukeni dunia ni duara ipo siku yenu itafika na mtalipa machozi na majozi ya hizi familia zote mlizopeleka misiba na maumivu makali sana.
==================

Poleni sana Familia na ukoo wa Deo Soka maumivu yenu yatalipwa tu na hawa wapuuzi na wajinga! watekaji

Nimemlea Deo Soka tangu akiwa na miaka mitatu mpaka akamaliza na shule na wakati amemaliza shule akaenda huko Dar Bibi wa Soka

Sikuchoka kulia Soka alikuwa ni mdogo wetu ndio kaka yetu ndio msaada kwetu, hatuchoki kulia nikiingia kwenye mtandao nabaki kulia tu Aunt wa Soka
 
Serikali ya ccm kamwe haiwezi kukwepa lawama za huu uonevu. ☹️
 
Duh!! Sad Bibi wa soka, Watoto wa Mwangosi,watoto wa mawazo, watoto wa Ben saanane,wazazi na ndugu wa Akwilina, watoto wa mdude,watoto wa ally kibao,watoto,Lissu,Heche,Mama wa pole pole na ndugu zao na wafuasi wa wao na Gwajima na wafuasi wake wakiingia tu barabarani hata nusu yao CCM inaanguka

Hii chain Ni kubwa Sana bado wafuasi wa kitima

Unajua tunachukulia Mambo pouw tu lakini kikinuka ndio tutaacha kuishi kwa mazoea
 
Ukiyasikia maneno anayoyasema huyu bibi yake na Soka ambaye alimlea tangu mdogo hadi anakuwa inaumiza sana.

Soka amepotea imepita mwaka na miezi 2 ambapo ilitekwa Agosti 18, 2024 familia yake haifahamu wapi amepelekwa mtoto wao. Nyie watekaji mliomteka Soka kumbukeni dunia ni duara ipo siku yenu itafika na mtalipa machozi na majozi ya hizi familia zote mlizopeleka misiba na maumivu makali sana.
==================

Poleni sana Familia na ukoo wa Deo Soka maumivu yenu yatalipwa tu na hawa wapuuzi na wajinga! watekaji

Nimemlea Deo Soka tangu akiwa na miaka mitatu mpaka akamaliza na shule na wakati amemaliza shule akaenda huko Dar Bibi wa Soka

Sikuchoka kulia Soka alikuwa ni mdogo wetu ndio kaka yetu ndio msaada kwetu, hatuchoki kulia nikiingia kwenye mtandao nabaki kulia tu Aunt wa Soka
Mungu Ibariki Tanzania
 
Back
Top Bottom