Biashara ya Vifaa vya Ujenzi (Hardware Store): Ushauri wa Mtaji, Uendeshaji, Changamoto na Faida

Parachichi

JF-Expert Member
Jul 22, 2008
510
102


Wakuu poleni na shughuli!

Ee bana kuna ndugu yangu ameniahidi kunitoa kwenye umasikini,kaniahidi kunikopesha USD 15,000 ili nifungue biashara ya kuuza vifaa vya majenzi.

Sasa nauliza wakuu kwa kiasi hicho kinatosha kuanzia?au ntakua najitia pressure tuu manake hela ndogo?

Maeneo ninayotarajia ni tegeta,Boko,Bunju.

Naombeni ushauri tafadhali wenye ujuzi na hii kitu manake naamini JF ni zaidi ya mtandao.

NAWASILISHA WAKUU

WADAU WENGINE WANAOHITAJI UFAHAMU WA BIASHARA HII
Habari Wapendwa!

Nahitaji kupata ufahamu angalau kidogo kuhusu biashara ya vifaa vya ujenzi ninaweza kuanza na mtaji kiasi gani kwa kuanzia tu yaani kiwango cha mwanzo kabisa.

Niko maeneo ya Nzega Tabora.

USHAURI NA MAONI YA WADAU
 
Ukitaka kufanya biashara ya vifaa vya ujenzi kwa ufanisi mtafute mtu ambaye amefanikiwa katika biashara hiyo. Mimi ninaye rafiki yangu ambaye amefanikiwa sana katika biashara hiyo anaweza kukupa basics. Kama uko serious nipigie simu 0755394701 nikuunganishe naye.
CHARLES.
 
Mara nyingi mwanzo ni mgumu sana na hukatisha tamaa pia. Na hasa hii mifumo yetu ambayo unatakiwa ulipe mapato kabla ya kuanza biashara. Lakini kwa maoni yangu mimi naona 15,000,000 to 18M ambayo ndio makadirio ya pesa unayotegemea kuwa kama initial capital sio mbaya kwa sababu ukishaanza biashara ndipo utajua wateja wako wanahitaji bidhaa gani kwa wingi kwa hiyo uwingi wa bidhaa katika fani ya ujenzi kama alivyochangia mdau mmoja hapo juu isikutishe.

Pia ukishaanza biashara kuna kitu kinaitwa mali kauli (maana yake kwa kuaminiwa na mtu ambaye wewe hufanya whole buy kwake anaweza kuwa ana kukopesha mzigo kiasi fulani nje ya cash yako) hii husaidia sana watu wanaoanza shughuli kwani ghafla tu tutakuona una duka kuuubwa ajabu kumbe mali zingine ni ada ya uaminifu wako na sio lazima ziwe zako, ingawa faida ni yako na ndio itakayo kutoa mapema kwenye shughuli uliyo buni.

Kaza buti anza shughuli hakuna kisichowezekana chini ya jua, naamini utapiga bao hasa kwa maeneo uliyo yalenga kwa sababu bado ni endelevu ki ujenzi.
 
We jaribu tu bahati yako, biashara ni risk na ukitaka kufanikiwa lazima ukubali kurisk hiyo pesa kidogo utakayo azimwa anza na bidhaa ndogondogo then uongeze zile kubwa kadri mtaji unavyoongezeka! Nakutakia mwanzo mzuri.
 
Anahitajika mtu ambaye yupo tayari kuingia ubia katika kufanya biashara ya vifaa vya ujenzi kwa Dar es salaam.
 
That is great I am expecting to come to Dar Sept 06 will cantact you
 
Anahitajika mtu ambaye yupo tayari kuingia ubia katika kufanya biashara ya vifaa vya ujenzi kwa Dar es salaam.
Enny. just like the other guys, I'm more than interested. Ukija dar we need to talk seriously. Actually we can form a partnership and have a chain of stores for that. For you information, this is one of the niche areas in growing cities like Dar-es-salaam. Who knows we might even extend to other cities like Arusha, Mwanza etc. So ukija tuongeeni jamani kwa kina kabisa.
 
I am interested pia, nipo kwenye biz hii kwa muda sasa..... pls tuma details
 
Umeshapata Partners watano, mkiwa wengi sana haina tatizo? mie pia najiongeza kwenye List
 
Anahitajika mtu ambaye yupo tayari kuingia ubia katika kufanya biashara ya vifaa vya ujenzi kwa Dar es salaam.
Mkuu na mimi niko interested more than sana, tuwasiliane mkuu
 
Thank you for the interested parties we organize and find the convenient time and day.

Tunaweza kujipanga na kufuata taratibu zote zaa kisheria katika kuunda hii partnership business in Hardware.

Myself I am proposing Saturday 10th of September 2010.

Thank you,
 
Ni kweli kabisa umoja ni nguvu na hasa tukiwa serious na business na kufuata maadili ya biashara we can move further
 
Jamani nimepata soko la vifaa vya ujenzi huku DRC Lubumbashi naomba wale ambao wapo serious tujipange na nipate contact zenu kwa mawasiliano zaidi.

Asanteni sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…