Biashara ya Nguo za Mtumba: Ushauri na Muongozo wa Kuifanya kwa Mafanikio

Qsm

JF-Expert Member
Dec 11, 2008
445
251

Naomba msaada wenu nina duka la nguo la kawaida tu na lipo eneo zuri la biashara kinachonishangaza sipati faida kabisa je kuna yeyote kwenye biashara hiyo ambaye anaweza kunishauri jinsi ya kulisimamia? Mimi ni mfanyakazi kwa hiyo si mara kwa mara nakuwa dukani hapo.

Naombeni ushauri tafadhali.


WADAU WENGINE WANAOHITAJI KUELEWA BIASHARA HII
Ndg zangu wana JF naomba kusaidiwa mawazo katika biashara hii ya nguo za kike;

1. Mtazamo wako kama inalipa au hailipi
2. Location sahihi ni ipi?
3. Nitarajie changamoto zipi?

Pia, kama unaushauri mbadala nitaupokea na kuufanyia kazi.
Habari zenu wandugu;

Kwa wenye utaalamu wa biashara ya mitumba nahitaji elimu yenu. Wapi nitapata mabalo ya mitumba 1st grade? Ambapo hakuna kupigwa famba? Au jinsi ya kutambua grade nzuri?

Natanguliza shukrani!


MAONI, USHAURI WA WADAU KUHUSU BIASHARA HII
 
Qsm,

Nataka kukushauri ila kwanza naomba unijibu hili swali/maswali kwani sikuona kokote ulipoeleza kwenye post yako.

Je, unapata hasara na biashara/duka lako ina muda gani?
 
Ikiwa hakuna faida kwa miaka mitatu yote na labda pia huna hasara inawezekana ni usimamizi mbaya.

Hakikisha unajitahd baada ya muda wa kazi pita dukani angalia mauzo ya siku hiyo, weka kumbukumbu ya kila bidhaa inayoingia na kutoka dukani kuwa na daftari lenye kumbukumbu za vitu vyote naamni kama nguo zinatoka na unaingiza nyingine lazima kuwe na faida.
 
Acha kuuza nguo zilizotoka Uchina, Dubai etc zisizo na ubora, usifuate mkumbo, uza vitu bora, unique vitanunuliwa.
 
Acha kuuza nguo zilizotoka uchina, Dubai etc zisizo na ubora, usifuate mkumbo, uza vitu bora, unique vitanunuliwa

Kwani kasema anauza za Kichina? lakini pia sioni shida iwe ya kichina ama inatoka uk mradi ipate mteja, ni kuchagua tu zile zilizopo kwenye fashion kulingana na wakati uliopo.
 
lina miaka mitatu sasa

Miaka mitatu ni mingi kwa biashara kama hiyo yako ya nguo. Nadhani kuna mambo machache tu unahitaji kufanya ili uweze kuiona faida hiyo ya hicho unacho kifanya.

Kama biashara/Duka linajiendesha lenyewe kwa maana lina lipa kodi zote za nyumba,TRA na Mishahara au mshahara kwa kipindi chote cha miaka mitatu,basi hilo duka lako lina faida sana, tena sana.

Kama mchangiaji mmoja hapo juu alivyo shauri, fanya uwe unaangalia ana uwe na muda na biashara na hesabu zake zote, usiache kila kitu kwa mtu/watu bila ya uangalizi wako mwenye.
 
Pia angalia upande wa choice, labda hukidhi mahitaji ya wateja.
 
Acha kuuza nguo zilizotoka uchina, Dubai etc zisizo na ubora, usifuate mkumbo, uza vitu bora, unique vitanunuliwa

Sawa ila nguo hizo ndizo zinanunuliwa sana maeneo hayo, lakini nitalifanyia kazi wazo lako.
 
Dada huyu hajasema anauza nguo za China au Dubai, sasa kwanini ufikiri hivyo? Halafu JF ni The home of Great Thinkers?

Dada ni hivi

1. Nenda kwenye mipango ya awali uliyopanga kwa ajili ya duka hili.
2. Je, mipango inafuatwa?
3. Kwanini mipango inafuatwa na bado kuna hasara?
4. Je, kuna tofauti yoyote ya mauzo ya mwanzo na sasa?
5. Je, mtaji wako umeongezeka au umepungua tangu ulivyofungua?

Ninachoona hapa ni usimamizi hafifu, unajua unapoanza biashara changa ni kama mtoto mdogo anatakiwa atunzwe kwa karibu na usimamizi makini ndipo aweze kukua na kujisimamia mwenyewe.

Kwa biashara mpya unabidi usimamie kwa karibu ujue maendeleo ya mwanao (duka hili).

Usitumie pesa ya mtaji na ukumbuke kurudisha mtaji (kureinvest)

Mambo mengine je kuna ushindani mkubwa kutoka biashara za karibu,lazima zipo! Je duka au biashara yako inakidhi mahitaji ya wateja uliowalenga? Ubora wa bidhaa, bei nk.

Je, huduma kwa wateja inaridhisha? Au msimamizi ndiyo amekuwa kama ndiye mfalme wakati wafalme ni wateja!!!

Kwa ufupi unahitaji kwenda kwenye biashara yako na kuchunguza mambo madogo na ya msingi kama hayo juu ndipo utakapogundua pesa inaungulia wapi.

Yapo mengi ya kufanyia kazi lakini hayo hapo juu ni ya msingi ya kukuonyesha muelekeo.
 
Biashara ya nguo imekuwa ngumu sana kwa sasa kutokana na watu wengi kuivamia. Upinzani umekuwa mkubwa sana na ukiangalia kodi za flame zilivyokuwa juu ndio kabisaa.

Hii biashara nina experience nayo toka miaka ya 94 mpaka leo.miaka ya 94 na sasa tofauti ni kubwa sana kutokana na sababu hizo juu. Kutokana na ugumu huo wengi tunategemea wateja wetu wa siku zote miaka nenda rudi huku wao wakileta wenzao na wengine wachache. wapya.

Ningekushauri vitu viwili vitatu kama unataka kuendelea nayo manake sasa hivi kutokana na ugumu wake watu wengi wamekimbilia kwenye ukulima.

Cha kufanya unapoleta mzigo jaribu kutafuta soko mikoani.unaweza kutafuta watu wa mikoani ukawauzia kwa jumla wao kama unaleta mzigo mwingi.

Kitu kingine jaribu kuleta mzigo mkubwa karibu na sikukuu kubwa zote,lazima hujue kutime hizi sikukuu kwnai hapo ndio biashara huwa kubwa na watu wanapenda mzigo mpya wakati huo.

Kitu cha mwisho wajue wateja wako,nikimaanisha jaribu kuangalia nguo zipi zinatoka zaidi ya nyingine,nguo za watoto ndio zaidi sijui kwako wewe kwahio unatakiwa kununua mzigo mkubwa wa nguo ambazo zinatoka sana.

Endelea na hizo hizo nguo za China kwani unalenga watu wenye kipato cha chini sio kila mtu anaweza kununua nguo kutoka Marekani.

Nakutakia kila kheri kwenye biashara yako.
 
Newazz na Arsenal Wenger nawashukuru mno mno kwa mchango wenu nitafanyia kazi maoni hayo kwani nina uzembe mkubwa wa kusimamia na kufuatilia kwa karibu duka langu.
 
Wajua sasa biashara ya nguo imesambaa kila kona. Kama unaweza kubadrisha bidhaa katika duka lako au uwe unaenda na catalogue mpya mpya. Kuwa up todate kila siku.
 
Hebu pata likizo halafu simamia mwenyewe kwa muda ili uone mwelekeo.
 
Kama huwezi kukaa mwenyewe kwa muda mpe muuzaji likizo. Inawezekana anauza na kununua tana bidhaa bila wewe kujua, faida anachukua.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…