BIASHARA YA NAFAKA ZA JUMLA

BIASHARA YA NAFAKA ZA JUMLA

political Engineer 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2014
Posts
296
Reaction score
794
Habari Wana JF

Nahitaji kununua mahindi Kwa wakulima mikoani na kuwa nasafirisha kuyaleta dar au mikoa yenye uhitaji zaidi.

Naomba kujua niwe na vibali gani na vinatolewa na Taasisi gani?

Sihitaji usumbufu wa njiani wakati mazao yanasafirishwa Ndo Maana nataka niwe na vibali vyote vinavyoniruhusu kusafirishamazao .

Tayari Nina kampuni iliyosajiriwa BRELA, Je nitafute vibali gani vya kampuni?

Asante in Advance
 
Unahitaji leseni ya biashara,
Ukifika Wilaya/Halmashauri unayonunulia nafaka waone maafisa wa kilimo watakupa utaratibu, kuna leseni pia.
Getini utalipia tzs 1,000 hadi 2,000 kwa kila gunia kama tozo ya Halmashauri.
 
Unahitaji leseni ya biashara,
Ukifika Wilaya/Halmashauri unayonunulia nafaka waone maafisa wa kilimo watakupa utaratibu, kuna leseni pia.
Getini utalipia tzs 1,000 hadi 2,000 kwa kila gunia kama tozo ya Halmashauri.
Kampuni nimefungulia Dar es salaam, nikapewa lessen ya kuuza mazao kutoka Manispaa ya hapa dar, je hii lessen haitoshi mpaka nitafute nyingine kule nakonunua? Kama ndo hivyo nitakuwa nazo ngapi maana nanunua mahindi wilaya mbali mbali
 
Back
Top Bottom