Honest urassa
Member
- Aug 21, 2013
- 13
- 1
Habari za humu, naomba kwa anayefahamu biashara ya Vito vya thamani Kama rubby na Tanzanite. Naomba muongozo nahitaji kufanya hii biashara. Natanguliza shukrani.
Mkuu kwa sasa bado sijafahamu bei sokoni. Ndio nimekuja hapa kufahamu naanzia wapi.Mkuu unafahamu vito na kuweza kujua thamani yake sokoni? Maana bila kuyajua madini ni rahisi kuingia mkenge kununua jiwe la thaman ndogo kwa bei kubwa
Nalenga soko la ndani, na ninataka kununua kutoka kwa wachimbajiBiashara ni ngumu sana unahitaji umakini wa hali ya juu, mi nimefanya for Leisure kwa muda wa Mwaka 1.
Nilikua nanunua Tanga nauza pale Arusha.
Unaweza nunua piece 1 kwa laki 1 ukitarajia kuuza kwa milioni au laki 6 mwishoni umefika sokoni unaambiwa unapata laki 1 na ishirini, ama wakati mwingine uambiwe unalipwa elfu themanini
1. Unataka kuchimba kwa kuweka man power?
Sometimes kuna ulaghai mwingi,
2. Unataka kununua kutoka kwa wachimbaji, let's Sapphire, Amethyst, Tourmaline, nk unawezapata Tanga kule Kigwasi na Ng'ombeni, Green garnets Arusha, nyingine wadau watakwambia zinapatikana wapi.
3. Unalenga kuuza soko la ndani au kuuza nje ya nchi?
Ainisha matakwa yako ili waje wanaoifahamu biashara hiyo wakujuze