taffu69
JF-Expert Member
- Feb 26, 2007
- 2,094
- 538
Katika siku za hivi karibuni nimeshuhudia vifuniko ambavyo vinatumika kufunika bia za TBL vikiwa na kutu kwa kiwango kikubwa. Bia ambazo nimekumbana nazo binafsi ni Kilimanjaro na Ndovu ambapo mara inapofunguliwa unakumbana na layer kubwa ya kutu kwenye mdomo wa chupa na kifuniko chenyewe na wakati mwingine chupa ikiwa imelika kwa kiwango fulani.
Naomba kupata ufafanuzi kutoka kwa wahusika wa TBL kama tatizo hilo wameshaligundua na hatua ambazo wamechukua ili kukabiliana nalo. Jambo hili limenishtua sana kwani kwa wale wanywaji ambao hawatumii glass wanahatarisha afya zao kwa kiwango kikubwa kwani wanakuwa wanameza uchafu huo moja kwa moja. Kwa upande mwingine hata wale wanaotumia glass wanaweza kuwa hatarini pia pale wanapojimiminia kinywaji hicho bila kufuta chupa hiyo kwa makini ili kuondoa uchafu huo.
Swali la kujiuliza ni kuwa wahusika wa TBS hawajaona tatizo hili ama wanasubiri madhara yatakapotokea ndiyo waanze kuchukua hatua?. Nimezungumzia suala la bia kutoka TBL lakini inawezekana kwamba hata bia zinazozalishwa na makampuni mengine zina tatizo linalofanana na hilo pia.
Naomba kupata ufafanuzi kutoka kwa wahusika wa TBL kama tatizo hilo wameshaligundua na hatua ambazo wamechukua ili kukabiliana nalo. Jambo hili limenishtua sana kwani kwa wale wanywaji ambao hawatumii glass wanahatarisha afya zao kwa kiwango kikubwa kwani wanakuwa wanameza uchafu huo moja kwa moja. Kwa upande mwingine hata wale wanaotumia glass wanaweza kuwa hatarini pia pale wanapojimiminia kinywaji hicho bila kufuta chupa hiyo kwa makini ili kuondoa uchafu huo.
Swali la kujiuliza ni kuwa wahusika wa TBS hawajaona tatizo hili ama wanasubiri madhara yatakapotokea ndiyo waanze kuchukua hatua?. Nimezungumzia suala la bia kutoka TBL lakini inawezekana kwamba hata bia zinazozalishwa na makampuni mengine zina tatizo linalofanana na hilo pia.