Elections 2010 Beware, slow poison of religious bigotry is entering into Tanzania’s body politic!

wewe pia mdini. kwani mapdri sio pekee ndio wenye mamlaka nchi hii?

Hakika wewe ni kiboko, kila kitu unapinga bila kujadili hoja. Hebu jaribu kujadili hoja kwanza n kisha onesha msimamo wako. Je wewe unalishwa na rais kwa sababu ni wa dini yako. Ni muhimu kama wadau kubadilishana uelewa wa jambo linawekwa mezani kwa kujadili ubaya na uzuri bila kukimbilia kuunga mkono au kupinga hoja. Kwa ujumla masuala yoyote yanayohusu dini hayana faida kwa Taifa hili, na hakuna mtu ambaye atashinda nafasi ya Urais kwa kutegemea kundi la wanadini wenzake.

Nchi inhitaji kutafutia suluhisho tatizo la udini. Je kuna mtu anaweza kuwa hana imani yoyote katika maisha yake. Je tutamweka wapi mtu ambaye hana imani yoyote, je imani ya mtu ndiyo iwe sifa ya kuwa kiongozi wetu? Hebu tujadili kwa staili hii, je kwa kuwa muislamu, Mhindu, mpagani au mkristo inakufanya kuwa kiongozi mzuri kwa Taifa hili?

Taifa linakumbwa na matatizo mengi ambayo yanatuumiza wote bila kujali dini ya mtu. Je foleni ya magari Dar es Salaam inajali kwamba wewe ni muislam au Mkristo? Je ukosefu wa maji, barabara, huduma bora za afya,elimu bora zinachagua dini ya mtu? Ni muhimu tukawa tayari kujadili hoja kwa nia

1. kuelimisha wengine juu ya ufahamu wako kuhusu hoja iliyopo jukwaani,
2. kutushirikisha uelewa wako kuhusu tatizo na kupendekeza namna tunavyoweza kuliondoa tatizo husika
3. Tushirikishe msimamo wako kuhusiana na tatizo lililopo.

Kwa njia hii jukwaa linakuwa chanzo cha elimu na maarifa, pia tutajua namna ya kuchambua masuala mbalimbali kupitia michango ya wengine, lakini kwa staili ya Malaria Sugu hatoi fursa hiyo kwa wengine.

Lakini naamini anacheza kwenye sehemu yake ya kujidai "Uhuru wa kutoa maoni"
 
the important thing here is to pray mungu aepushe hali kama hii ili nchi yetu iwe ya amani
 
Malaria Sugu unafanana kabisa na jina lako....angalia hiyo malaria sugu isije ikakuchakachua akili!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Jaribu kujibu hoja kwa busara.....sawaeeee
 
Monday, 11 October 2010

dk%20slaa%2021.jpg

Dk Willibrod Slaa

Nora Damian na Aziza Masoud

JINA la Dk Willibrod Slaa jana lilitawala mjadala wa masheikh na maimamu katika semina ya elimu ya uraia na uchaguzi baada ya baadhi kudiriki kumtaja kwa jina na kueleza kuwa anafaa kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano, huku wengine wakitaka zitajwe sifa za mgombea anayefaa.

Wengine walipendekeza kuwa katibu huyo mkuu wa Chadema asipewe kura kwa kuwa hafai kuongoza na hivyo kupendekeza kuwa mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete au Prof Ibrahim Lipumba wa CUF ndio wapewe kura kwenye uchaguzi mkuu.

Pamoja na mjadala kuonekana ukitumia dini kama moja ya sifa za kiongozi anayefaa, masheikh hayo waliibuka na tamko linalowataka wananchi kuepuka kutumia udini wakati wa kuchagua viongozi kwenye uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 31.

Semina hiyo iliandaliwa na taasisi ya Kiislamu ya Imam Bukkary ikishirikiana masheikh na maimamu wa Dar es salaam.

Wakichangia kwenye semina hiyo, baadhi ya masheikh walisema kuwa Dk Slaa, ambaye anagombea urais kwa mara ya kwanza baada ya kuliongoza Jimbo la Karatu kwa miaka 10, anakubalika na wengi na ana uwezo wa kuongoza nchi.

Sheikh Said Mkalamba kutoka Magomeni Mapipa alisema anavyojua yeye Dk Slaa, ambaye anagombea urais kwa tiketi ya Chadema, anakubalika na anaweza kuwa rais.

Alisema kama itadhihirika kuwa kuna wagombea wengine ambao wana imani kama yake ambao wanaweza kuongoza, wampe aliyeanza ili amalizie vipindi vyake viwili.

Alisema kati ya wagombea wote wa urais wako Waislamu wengi, lakini wanaoonekana kuwa na nguvu ni wawili hivyo akawataka waumini wamchague mgombea mwenye nguvu zaidi ili wasije wakapoteza kura zao.

“Waislamu tumekuwa tukiambiwa hatujui kuongoza hivyo ni bora tumpe huyu aliyeanza amalize vipindi vyake vyote viwili kwasababu tukimpa mwingine itadhihirika rasmi kuwa hatujui kuongoza," alisema Sheikh Mkalamba.

Sheikh Hemed Majaliwa kutoka Kinondoni alitaka Dk Slaa asipewe kura kwa madai kuwa si mwadilifu na yeye akapendekeza apewe kura mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete au mgombea wa CUF, Profesa Lipumba.

Wachangiaji wengine katika mjadala huo ingawa walikuwa hawawataji majina wagombea wanaowataka, lakini namna walivyokuwa wakichangia walikuwa wakionekana dhahiri kumpigia debe mmojawapo kati ya Kikwete, Lipumba na Dk Slaa.

Sheikh mwingine kutoka Kinondoni, Abdul Mahede alitahadharisha dhidi ya matamko ya viongozi wa dini nyingine kwa kile alichodai kuwa yamekuwa yakipewa nafasi kubwa na kuaminiwa kuliko matamko yanayotolewa na viongozi wa Kiislamu.

Naye Sheikh Mkasi Mohamed kutoka Temeke alitaja mambo ambayo yanapaswa kuangaliwa kabla ya kuamua kuchagua kiongozi kuwa ni pamoja na kufanya mambo mazuri akisema watu wa namna hiyo wapo hata kabla ya kupewa madaraka.

Alisema pia watu wanapaswa kuepuka viongozi wasiotimiza ahadi, wanaosema uongo na wale ambao wameanza kufanya mambo mabaya kabla hawajaingia madarakani.

Kwa mujibu wa sheikh huyo sifa nyingine za kiongozi bora ni yule aliyeweza kupambana mafisadi na asiye dhaifu kwa sababu hatoweza kutetea haki yake.

Katika tamko la pamoja masheikh hao waliitahadharisha jamii kutoingiza udini katika siasa, hasa wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu kwa kuwa kufanya hivyo kunaweza kuhatarisha amani ya nchi.

Akisoma tamko hilo, mwenyekiti wa taasisi hiyo, Sheikh Khalifa Khamis alisema kauli na matendo yanayosababisha amani kuvunjika kama kufanya kampeni za kisiasa kwa misingi ya dini, kunaweza kuligawa taifa na kupoteza amani.

“Amani na utulivu ni tunu adhimu inayostahili kulindwa kwa nguvu zote tunalaani kwa nguvu zote wale wanaoeneza wito wa kuhamasisha chuki za kidini kwani jambo hilo ni hatarfi na halikubaliki kwa mujibu wa sheria za nchi yetu,”alisema Sheikh Khamisi na kuongeza kuwa:

“Kila chama kijihalalishe kwa misingi ya siasa zao na yale waliyoyafanya. Uamuzi wa kumchagua nani ni jukumu la wananchi wenyewe dini isitumike," alisema.

Alisema wapo watu ambao wamekuwa wakihamasisha chuki za kidini makanisani na kwenye mikutano ya hadhara pamoja na viongozi wa kisiasa wanaochochea wananchi kumwaga damu baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi.

Alisema suala la udini likiachwa liingizwe kwenye siasa lina athari kubwa kwani linaweza likasababisha watu kugawanyika na hivyo kutakuwa na taifa lisilokuwa na mwelekeo.

Viongozi hao wa dini pia walisema wanaunga mkono tamko lilitolewa na mnadhimu mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Abdurahamani Shimbo na kwamba wanalaani wale wanaolipinga.

Sheikh Khamisi alisema wanaamini wanaopinga kauli hiyo ndio walioandaa vurugu za uvunjifu wa amani na umwagaji damu na kuvitaka vyombo vya dola kuwadhibiti watu na viongozi wanaofanya ama kutoa matamshi ya kichochezi yanayoashiria uvunjifu wa amani.

Masheikh na Maimamu hao pia wamewataka viongozi wenzao kutumia fursa ya swala tano na mikusanyiko mbalimbali kuwahamasisha waumini wao kujitokeza kupiga kura siku ya Oktoba 31 na kuwachagua viongozi waadilifu, wasioendekeza udini na wasiokuwa na kauli au matendo yanayochochea uvunjifu wa amani.

Awali kabla ya kutolewa kwa tamko hilo masheikh na maimamu hao walionekana kutofautiana kuhusu kiongozi anayefaa kuchaguliwa kuwa rais wa nchi hii.


Source: Mwananchi



naomba kuwasilisha!!!
 
bado hujanijibu. mnamsema jk anapendelea waislam wenziwe. dk slaa ni padri, jee atapendelea waislam?

Ndiyo tunaanimini katika HAKI SAWA NA UTAWALA WA SHERIA NA AJIRA NI ON MERITS Siyo mambo ya huyu tunaoa nyumba moja, huyu ni shemeji, huyu ni mwana mtandao, huyu jina lake ni Ramadhan au ni mwanangu na hivyo mtoto wa mfalme! Fed up!!
 
Udini upo ingawa ni kwa chini chini kwani hata UDOM dini moja ndo inaqualify 75% -80% na wafanyakazi pia !!!!
 
Labda wakisema hivyo sawa ila siwaamini wale waislamu wanaosema tusiwachague wanaoingiza siasa kwenye dini kwa waislamu ndiyo wa kwanza kutuletea mambo ya dini kwani wako tayari kuilazimisha serikali iendelee kupoteza rasilimali kujadili mahakama ya kadhi ambapo ni kuchanganya siasa na dini.....

....wapo tayari hata kutishia kutoipa kura ccm kwa sababu tu ya mambo yao ya kiislamu......tukifikia hatua km hiyo kuwa kiongozi fulani anafaa itatusaidia kuliko kuwadanganya watz kuwa kuna watu wanatumia udini wkt wao waislamu ndio wako mstari wa mbele kuleta udini
 
Kweli Dr. Slaa anakubalika na wengi. Ni vyema wanaoitakia mema nchi hii wakamchagua Dr. Slaa la sivyo tutaendelea kuwa nchi ya 3 kutoka mwisho kwa umasikini duniani.
 
yes.kusema kweli ni democrasia ya kweli.mtu kama anafaa lazima tukubali,na pia tuwaambie watu wengine pia kwamba jamani fulani anafaa,siyo kutoa matokeo ya kura za maoni ambazo hazina mbele wala nyuma,tena nahisi kuna rushwa katika hilo la kura za maoni.
 
Anaogopwa kikwete kwani wengi wamemstukia kwa sababu anawakumbatia waislamu kwa kuiweka hata kwenye ilani mamnbo ya mahakama ya kadhi na oic ambayo ni mambo ya kiislamu...........kikwete amewatiliza waislamu wasiwe na wasi kwani atawaletea mambo hayo kwa gharama yoyote........hiyo ni kwa vitendo ila kwa maneno slaa ndiyo mdini...............wakristo wamestuka janja ya waislamu kuanza kulalamika uongo wkt wao ndiyo wanaongoza propaganda za kidini nchini
mbona uanpindisha. Wanumuogopa dk slaa, kwani waislam wengi wemeshtuka
 
Hongera viongozi wetu wa kislaam kwa kukemia udini. Tuchague kiongozi kwa uwezo wake wakuongoza na kuleta maendeleo kwa wananchi, si dini wala kabila!
 
Lakini waislau haohao si ndiyo wanatuletea udini kwa kuingiza mambo yao hadi kweneye ilani za vyama?........hivi kila dini ikiamua kuweka mambo yao kwenye chama cha siasa itakuwaje.............waache kuwapaka mafuta watz kwa mgongo wa chupa!
hongera viongozi wetu wa kislaam kwa kukemia udini. Tuchague kiongozi kwa uwezo wake wakuongoza na kuleta maendeleo kwa wananchi, si dini wala kabila!
 
tatizo lenu nyinyi msiokuwa waislam mnajiona mko juu ya wengine. kwani wapo madri wanompigia debe dk slaa waziwazi lkn hawaitwi wadini. akitokea kiongozi wa dini nyegine akipinga mnambwambia mdini. sasa nani mdini hapo?
Tuache ushabiki na uzandiki ndugu yangu ni mapadre gani wanaompigia debe Dr. Slaa waziwazi? Acha kuongea vitu vya kufikirika..naamini ya kwamba ukiniambie nikutajie masheikh wawili wanaompigania JK kwa nguvu zao zote nitaishia kukutajia mmoja tu yaani Prof Sheikh Yahya.
 
Jenerali+Ulimwengu.jpg

By JENERALI ULIMWENGU
October 10, 2010


Well, the only time I've heard a Catholic cleric say something politically incorrect - and pretty daft as well - he was saying that Kikwete, a Muslim, was God's own choice.

Slaa has never hidden the fact that he is a Catholic, a defrocked priest into the bargain.

In the past, we have had presidents who have worn their religiosity on their sleeve - Julius Nyerere and Ali Hassan Mwinyi - and both went on to assume confessional careers after retirement, the former inching toward canonisation, and the latter serving as part-time Imam. So where is the problem?

Too many Tanzanian politicians, especially in the ruling party, CCM (which has openly declared its aversion to debate), are simply incapable of engaging in dialogue on ideas and issues, and this renders them incapable of executing any campaign outside character assassination and identity politics.


Well thought!
 
tuache ushabiki na uzandiki ndugu yangu ni mapadre gani wanaompigia debe dr. Slaa waziwazi? acha kuongea vitu vya kufikirika..naamini ya kwamba ukiniambie nikutajie masheikh wawili wanaompigania jk kwa nguvu zao zote nitaishia kukutajia mmoja tu yaani prof sheikh yahya.

kakobe
 
Back
Top Bottom