Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 872
Wana JF salaam.Ningependa niwaulize wataalamu wetu juu ya suala hili ambalo limekuwa likijitokeza mara kadhaa hapa kiwanja cha ndege Songea.Bendera ya CCM inapeperushwa mbele ya ofisi hii kwenye jengo linaloitwa VIP ikiwa sambamba kabisa na bendera ya Taifa.Hili limekaeje jamani?Kwani ninafahamu siasa zimezuiliwa kwenye ofisi za umma na hata wafanyakazi wake wamezuiwa kufanya siasa eneo la kazi.Je hii bendera sio inaashilia siasa inafanyika hapa?Au kupeperusha bendera si tatizo?Meneja hafanyi siasa hapa kweli? Mwaka juzi tena wakati wa kampeni bendera hii ilikuwa inapeperushwa hapa hapa.Ilikuwa tarehe 10.10.2010 wakati Jakaya alipokuwa anafanya kampeni hapa Songea bendera hii ikawa inapepea.Au ndo tuseme kuna tawi hapa linaendeshwa kwenye majengo haya ya serikali?Kama nikiambiwa ni sahihi basi CDM nasi tutafanya mpango tuwe na tawi hapa.