Bei ya simu used Zanzibar

mbaya wao

Member
Joined
Jul 6, 2022
Posts
33
Reaction score
40
Wakuu naomba kujua uhalisia wa bei za simu used Zanzbar, maana nikiangalia kwenye page mbalimbali insta bei yake ndogo Sana mfano Samsung s10+ kwa laki nne. Nilipouliza page moja utaratibu wameniambia et nalipia halafu natumiwa risiti na kwenda kupokelea mzigo airport. Nahisi Kama ni matapeli.

Naomba kujua hawa watu sio matapeli, mfano wa insta page mobile_phones_uk
Na kwanini wanauza Bei ya chini wanazichukua wapi kwa njia gani?
 
Nitafute mimi nipo Zenji tujenge maisha
 
Ukiona page ya kuuza kitu insta imeandikwa wako Kenya au Zanzibar hahaha usinunue utapigwa urudi hapa kulia kulia

Ukitaka kuthibitisha hilo wapigie simu waambie kesho nakuja kununua mwenyewe watakwambia hatuko Unguja tuko Pemba.

Ukiwaambia Pemba na ndg nielekeze nimtume hapo chap sahiz utapigwa block au kuzungushwa weeee
 
Ni Tanzania tu Vitu vikali vikali simu, laptop, Gaming console etc vinapatikana ndanindani huko Tanzania na Dar havipo. Eti ps5 bei rahisi kuliko Usa inapatikana Pemba. Ukiona hivyo mkuu kimbia. Otherwise tafuta rafiki anayeishi huko akutane na muuzaji.
 
Yaweza kuwa niliwahi nunua s7 edge zanzbar 240000 sema niliifuata mwenyewe
 
Kuna page 1 insta ya iPhone wanauza bei chini ukiwapigia au kuchart nao wapo busy waambie nipo Nairobi ofisi zenu zipo wapi nije wanakublock hata kuchart hawataki KUWA MAKINI USIJE KUWA FURSA
 
utaibiwa kaka ww kama unataka simu nzuri na ni bora ww nicheck tu nitakuuzia kwa bei simple kidogo ila
Siyo kwa s10 plus kwa 400K u ataka ulie??
 
Matapeli wa Dar kimbia mkuu
 
Hao jamaa ni matapeli jaribu kuwapigia uone km watapokea cmu yko,wengi wamepigwa kwa sababu yakuona bei zao ziko chini
 
Kuna rafki alipigwa laki 3 alikubali kulipia iphone mpya ipo igunga Tabora, nilimuonya sana ila akalipia kimya kimya kujidai yeye mjanja na kweli walimuonyesha risiti na nyaraka ya kusafirisha kumbe huwa wanazitengeneza wenyewe kwa utapeli......

Huko Zanzibar na Kenya hata usijaribu
 
Zenji simunused ni bei rahisi kweli
S7 edge 250k unaipata tena in good condition
S10 inatembea humohumo kwenye 400k na ushee na nimeona seller wengi wakizisafirisha with a guarantee ya kubadilishiwa kama imezingua
Ila tahadhari za wadau zizingatiwe kwani matapeli hutembelea mazingira halisi
 
page moja insta inaitwa vunjabeisimu_zanzbar wana Bei ndogo hata kiwandani hakuna hiyo Bei, Yan Samsung S20 laki nne, dah huku moyo unataka huku unasita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…