Bei ya mshikaki coco beach

Sio Coco tu mahali pengi Dar wahudumu wezi sana na nadhani wanaambiwa kufanya hivyo na mabosi wao. Rose Garden ndio balaa.

Ni kweli rose garden jana wamenipiga buku baada ya kuagiza makange
 
Umenikumbusha kisa kimoja kilitokea mwaka 2002 Arusha. Jamaa zangu fulani toka Dar walikwenda Arusha kikazi. Ilipofika jioni wakaenda sehemu na kuagiza mishikaki wakaambiwa hapa hatuuzi mishikaki ila unasema unataka nyama sehemu ipi au ya shilingi ngapi. Basi kwa wakati huo wakaagiza nyama ya shilingi 2000/=. Baada ya muda walipoletewa (walikuwa watatu) wakamwambia yule mhudumu kuwa atakuwa amekosea maana wao wameagiza nyama ya 2000/= tu!! Akawaambia ndiyo hii, jamaa waliangaliana hawakuamini macho yao, maana nyama ilikuwa ni nyingi balaa!!! Wakaambiwa nyie mmezoea njaa Dar hii AR bana!!!
 
Wenye mahotel wanajua kwamba wahudu wao ni wezi wkubwa na hilo ni ajabu na aibu sana hasa hapa Tz kila sehemu unaibiwa sana ni ajabu serikali haichukui hatua
 
Sio Coco tu mahali pengi Dar wahudumu wezi sana na nadhani wanaambiwa kufanya hivyo na mabosi wao. Rose Garden ndio balaa.

rose garden ndo balaaa....wezi kwli upande wa chakulaa....ile dawa yao ni kuwaambia wakuletee risit ya TRA,na sio walioindika wao
 

Hayo yaliwah kunikuta mimi irnga nilipo agiza chips balaaa cjps za buku 2 ni kama za buku 20dar
 
Poleni basi futeni hayo mapovu ya mate kisa....mmetapeliwa buku tano
 

kwahio ukiingia supermarket ukaona chocolate ukaitamani una njaa????ndugu kuna kula kwa njaa na kula kwa hamu tu.... vitu kama chocolate,mshikaki mmoja/miwili ni hamu tu.....
 
Duu umeongea kama vile tulikuwa wote maana story ni hiyo hiyo na ilikuwa Florida Bar. Nakumbuka actually walisema samahani sisi tuliagiza ya 2000 mbona unatuletea hii wakiwa na maana mbona nyingi mno, mchoma nyama akawambia sahamani nyingine inakuja sinia ni dogo kutosheleza yote nyingine itakuja baada. Jamaa walibaki vinywa wazi. Tulikula mpaka nyingine nikafunga na kuondoka nayo nyumbani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…