Mwanongwa
JF-Expert Member
- Feb 15, 2023
- 866
- 805
Hii ni barua ya wazi kwako Mheshimiwa Waziri wa michezo Professor Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi kuhusiana na watendaji wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT).
Kuna sintofahamu nyingi zimejitokeza kwenye chaguzi za Vyama Vya Mipira ya Miguu Vya Mikoa kabla ya kutangazwa uchaguzi wa Shirikisho la Mpira Wa Miguu Tanzania,TFF.
Malalamiko mengi yamewasilishwa kwa Katibu Mtendaji na Msajili wa Baraza la Michezo Tanzania kuhusiana na chaguzi hizo lakini mpaka sasa "HAWATAKI" kutoa majibu au miongozo.
Mfano ni uchaguzi wa Chama Cha Mpira Wa Miguu Mkoa wa Mbeya,MREFA uligubikwa na uvunjaji mkubwa wa kanuni,sheria na taratibu.
1.Uchaguzi ulisimamiwa na kamati ya uchaguzi ya TFF badala ya kamati ya uchaguzi ya MREFA.
2.Wapiga kura waliotumika ni "BATILI" wakati wale waliokuwa "HALALI" walizuiwa na JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA kuingia ukumbini kupiga kura.
3Kifungu cha 5.2.3 cha Sera ya maendeleo ya michezo ya mwaka 1995 kilikiukwa kwani kuna mgombe alizidisha vindi vya uongozi alipitishwa na TFF na kuchaguliwa.
4.Katiba ya MREFA toleo la mwaka 2008 Ibara ya 32.4 kipengere cha muda wa madaraka kilikiukwa.
Katika uchaguzi huo ambao Msajili Msaidizi Wa Vyama Vya Michezo Mkoa wa Mbeya alihudhuri alitoa miongozo sahihi lakini Kamati ya uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania,TFF ilimpuuza na kumwambia wao wanakwenda na muda.
Wahanga wa uchaguzi huo uliyofanyika tarehe 06/04/2025 katika Ukumbi wa Royal Tughimbe jijini Mbeya tuliandika malalamiko yetu BMT kupitia ofisi ya MKUU WA MKOA MBEYA ila hadi sasa hakuna majibu.
Tunahisi kutotendewa haki na kujiuliza maswali mengi juu ya uwezo wa utendaji wa wizara yako.
Haya tunayaongea baada ya kufanya jitihada kubwa kufuatilia jambo hili BMT bila majibu hadi hii leo.
Tunajaribu kufuata taratibu zote ili kuimarisha amani maana siku ya uchaguzi tusingekuwa wavumilivu kungekuwa na uvunjifu mkubwa wa amani hasa baada ya Jeshi la Polisi kuingilia mchakato huu wa uchaguzi.
Hivyo basi ukiwa Waziri mwenye dhamana tunakuomba utoe majibu au mwongozo wa changamoto hii.
Swali tunalojiuliza huko BMT kuna mkwamo gani hadi wanashindwa kutoa majibu zaidi ya miezi kadhaa sasa.
Je wanabariki uvunjifu wa sheria za nchi na vyama?
Wadau tunakerwa na utendaji wa BMT kutokana na kuchukua muda mrefu kutoa maamuzi.
Hii inaathiri utendaji wa Wizara yako kwa ujumla. Tumekuwa na wasiwasi na uwezo wa utendaji kazi wa BMT maana mwanzo tuliamini kuwa migogoro yote ya kikatiba inatatuliwa na BMT lakini hali imekuwa tofauti na badala yake inaonekana kama wanabariki uvunjifu wa katiba unaendelea.
Tunakuomba Mheshimiwa Waziri kuingilia kati suala hili ili wadau tupate majibu.
Kuna sintofahamu nyingi zimejitokeza kwenye chaguzi za Vyama Vya Mipira ya Miguu Vya Mikoa kabla ya kutangazwa uchaguzi wa Shirikisho la Mpira Wa Miguu Tanzania,TFF.
Malalamiko mengi yamewasilishwa kwa Katibu Mtendaji na Msajili wa Baraza la Michezo Tanzania kuhusiana na chaguzi hizo lakini mpaka sasa "HAWATAKI" kutoa majibu au miongozo.
Mfano ni uchaguzi wa Chama Cha Mpira Wa Miguu Mkoa wa Mbeya,MREFA uligubikwa na uvunjaji mkubwa wa kanuni,sheria na taratibu.
1.Uchaguzi ulisimamiwa na kamati ya uchaguzi ya TFF badala ya kamati ya uchaguzi ya MREFA.
2.Wapiga kura waliotumika ni "BATILI" wakati wale waliokuwa "HALALI" walizuiwa na JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA kuingia ukumbini kupiga kura.
3Kifungu cha 5.2.3 cha Sera ya maendeleo ya michezo ya mwaka 1995 kilikiukwa kwani kuna mgombe alizidisha vindi vya uongozi alipitishwa na TFF na kuchaguliwa.
4.Katiba ya MREFA toleo la mwaka 2008 Ibara ya 32.4 kipengere cha muda wa madaraka kilikiukwa.
Katika uchaguzi huo ambao Msajili Msaidizi Wa Vyama Vya Michezo Mkoa wa Mbeya alihudhuri alitoa miongozo sahihi lakini Kamati ya uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania,TFF ilimpuuza na kumwambia wao wanakwenda na muda.
Wahanga wa uchaguzi huo uliyofanyika tarehe 06/04/2025 katika Ukumbi wa Royal Tughimbe jijini Mbeya tuliandika malalamiko yetu BMT kupitia ofisi ya MKUU WA MKOA MBEYA ila hadi sasa hakuna majibu.
Tunahisi kutotendewa haki na kujiuliza maswali mengi juu ya uwezo wa utendaji wa wizara yako.
Haya tunayaongea baada ya kufanya jitihada kubwa kufuatilia jambo hili BMT bila majibu hadi hii leo.
Tunajaribu kufuata taratibu zote ili kuimarisha amani maana siku ya uchaguzi tusingekuwa wavumilivu kungekuwa na uvunjifu mkubwa wa amani hasa baada ya Jeshi la Polisi kuingilia mchakato huu wa uchaguzi.
Hivyo basi ukiwa Waziri mwenye dhamana tunakuomba utoe majibu au mwongozo wa changamoto hii.
Swali tunalojiuliza huko BMT kuna mkwamo gani hadi wanashindwa kutoa majibu zaidi ya miezi kadhaa sasa.
Je wanabariki uvunjifu wa sheria za nchi na vyama?
Wadau tunakerwa na utendaji wa BMT kutokana na kuchukua muda mrefu kutoa maamuzi.
Hii inaathiri utendaji wa Wizara yako kwa ujumla. Tumekuwa na wasiwasi na uwezo wa utendaji kazi wa BMT maana mwanzo tuliamini kuwa migogoro yote ya kikatiba inatatuliwa na BMT lakini hali imekuwa tofauti na badala yake inaonekana kama wanabariki uvunjifu wa katiba unaendelea.
Tunakuomba Mheshimiwa Waziri kuingilia kati suala hili ili wadau tupate majibu.