KERO Barua ya wazi kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Alberto Msando

KERO Barua ya wazi kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Alberto Msando

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Ms Billionaire

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2020
Posts
2,466
Reaction score
4,967
HABARI YA LEO WAKUU,

Barua ya Wazi kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Bw. Alberto Msando.

Kwanza nikupongeze kwa Uteuzi wako wa kuja kuiongoza Wilaya hii ya Ubungo, tuna matumaini na wewe tena sana tu.

Nikupongeze pia kwa juhudi ulizozianzisha za kupunguza au kukomesha foleni zisizo na msingi katika wilaya hii.

Dhumuni la Barua hii ya wazi kwako, ni kuomba ututazame wakazi wa Goba Tegeta A kwa jicho la huruma. tuna barabara mbovu sana. nilishaandika malalamiko mengi sana humu kuhusu ubovu huo wa barabara lakini naona hakuna anaejigusa.

KINACHONISIKITISHA KUHUSU HII BARABARA NI JINSI AMBAVYO SCHOOL BUS ZA WATOTO ZINAPITA KWENYE CARAVAT DOGO SANA INAHATARISHA MAISHA YAO KIPINDI CHOTE. HII NJIA NI KAMA UKITOKEA MADALE ROAD UNAELEKEA KITUO CHA AFYA CHA MTAKATIFU YOHANNE, KULE KUNA SHULE ZAIDI YA NNE LAKINI NJIA NI HATARISHI. TUNAOMBA TUTENGENEZEWE HII NJIA NA WATUWEKEE CARAVAT KUBWA ILI SCHOOL BUS ZIPITE KWA USALAMA. NA KAMA INAVYOONEKANA KWENYE PICHA TUCHONGEWE HII NJIA KWASABABU KINGO ZINASOMBWA NA MAJI MARA KWA MARA HATA BARABARA IKICHONGWA.

NIMEAMBATANISHA NA MALALAMIKO YANGU YA TANGU MWAKA JANA.
NA PIA NIMEAMBATANISHA PICHA YA RAMANI YA ENEO HILO, PICHA YA CARAVAT NNALO LIZUNGUMZIA NA PICHA YA SCHOOL BUS ZA WATOTO ZINAVYOPATA ADHA.

TUNAOMBA MTUSEMEE NA KUTUSAIDIA KATIKA HILI.

NAWASILISHA

1. Wakazi wa Goba njia ya Tegeta A kwenda Madawa na Kulangwa tuna changamoto kubwa ya Barabara
2. Barabara ya Goba Tegeta A/Kulangwa bado inatia mashaka mvua zikianza school bus zinapita sehemu hatarishi
3. Changamoto ya barabara mbovu Goba Kulangwa/Tegeta a Serikali inapuuza?

1715793799418.png


1715793838808.png
1715793877788.png
1715793925903.png
barabara mbovu.jpeg
cc309ef9-7a1b-4e14-a529-651420da9b3e.jpeg

Hii video iliyotumwa nimeattach uone school bus za watoto zinavyopita. Ikitokea wameyumba kidogo tutaongelea msiba. Mara nyingi hizo kingo huwa zinasombwa na maji mvua zikinyesha. Udongo wa pembeni huwa unamomonyoka. Ni HATARI KULIKO NNAVYOWEZA KUELEZEA. Tusisubiri kuandika rip za watoto jamani haya mambo mbona yanaweza kurekebishika.​
 
Dhumuni la Barua hii ya wazi kwako, ni kuomba ututazame wakazi wa Goba Tegeta A kwa jicho la huruma. tuna barabara mbovu sana. nilishaandika malalamiko mengi sana humu kuhusu ubovu huo wa barabara lakini naona hakuna anaejigusa.
Hawezi kukusikiliza.
 
CCM mitano tena, maana wapinzani waliturudisha nyuma sana.

Sasa yapo wapi, miaka mitano imeisha Mbunge wa Jimbo bara kutoka CDM ni mmoja tu. Nilidhani kwa miaka hii 5 watamaliza matatizo yote. Kumbe hamna kitu sasa tuseme

#NO REFORM NO ELECTION #
 
Mkuu wa wilaya kazi yake ni kuhakikisha ccm inabaki madarakani, sio kazi yake kurekebisha barabara.
He will prove you wrong. sijawahi kuita kiongozi ambae sio Rais kwenye thread zangu. I believe in Msando, that`s all i can say for now.
 
Utashangaa ishu ya plate number na wake wa wabunge kupata VIP Treatment inapitishwa ila ishu muhimu kama hizi ccm haina final say kwa miaka 60+.

Kuishi Tanzania inahitaji moyo wa jiwe.
 
Back
Top Bottom