Barua ya SFO hii hapa: Je, Chenge na PCCB wamedanganya?

Mkuu superman mie naungana na wewe na watanzania wengine kwa ujumla kupinga huyu mtu kuwa spika na tuwe na kauli moja kwa mbunge yoyote yule ambae atampa kura huyu mtu basi 2015 tumuwajibishe .

Thread ifunguliwe leo hii ya kuwaonya wabunge kuhusu kumpigia kura chenge kwani mpango ushapangwa kwamba huyu mtu ndio hawe spika hili kwenda kuzima ma skendo ya rushwa yote.

inauma sana kwamba nchi yetu viongozi wanaofanya maovu ndio wanazawadiwa nafasi za juu zaidi kila kukicha.
 
Hosea is just another joke,sijui kwanini bado ana kazi ile? huyu si ndio alidanganya watanzania kuhusu Richmond na kutoa report Richmond ni safi,huyu Chenge hana business yeyote inayojulikana na ni mtumishi wa serikali sasa hizo billions alizipata wapi? ****** like Hosea hawezi hata kuuliza swali kama hilo....hawa wanachezea watu akili tuu na kuona kila mtu mjinga.
 
wana jf;

mwanasheria wa zamani wa serikali ya jmt andrew chenge na takukuru wote kwa nyakati tofauti wamedai kuwa chenge hakuhusika katika kashfa ya rada.

lakini tuhuma na ushahidi uliopo katika barua ya sfo kwenda kwa mwanasheria mkuu wa jmt ya tarehe 21 march 2008 inaonyesha kuwa chenge, bado anao mkono katika tuhuma hizi nzito. Na bado anawajibika kuwajibu wa tanzania alipata wapi usd 1.5 million badala ya kuja na majibu mepesi kwa maswali magumu kuwa "hivyo ni visent vyangu na nina haki ya kikatiba kutokueleza nilikozipata"

ninachoshindwa kuelewa ni wanasiasa wa tanzania na watendaji wao; je wanatufanya watanzania hamnazo au mazezeta sana? Je, kwa barua hii na tuhuma zilizoelekezwa kwake ana majibu gani ya kutupa hata kama anadai sfo wamem- clear. Hizo usd 1.5 million alizitoa wapi? Na huyu ndiye sasa anataka awe spika wa bunge letu.

ole wao wabunge wakimchagua 2015 si mbali, mtakutana na hukumu ya moto!

je pccb na chenge wamedanganya? Ni kweli sfo hawajamhusisha chenge na tuhuma hizi?

naona kizunguzungu bado!





sources:

1. http://hawleyfeinstein.files.wordpress.com/2010/02/sfo-tanzania-request.pdf
2. http://hawleyfeinstein.files.wordpress.com/2010/03/tanzania-bae-allegations1.pdf
3. The guardian tanzania, "moment of shame", 7/2/10
4. bae's secret $12m payout in african deal | world news | the guardian

nimekukubali mkuu!
 
Wadanganyika lazima tukome mwaka huu, si ndio hao tulioamua kuwapa 'kula' sasa hebu fikiria, badala ya kupambana na ufisadi jambo ambalo limekuwa gumzo kubwa kabisa katika mchakato mzima wa uchaguzi wa awamu hii, strategy yao ya kwanza ni kusafisha mafisadi wote na kuwarudishia tena ulaji ili waendelee kutu ??#@)... hapo ndio tutajua kama JK ana uwezo wa kufanya maamuzi magumu, sifa mojawapo ya kiongozi mahiri.
 
Uongozi wa serikali ya Tanzania ni dhaifu sana, sana. Ukimchukua mgonjwa wa akili pale muhimbili, wodi ya vichaa, na kumweka pale IKULU ya Tanzania atafanya mambo makumbwa ya kimaendeleo kuliko hawa watawala waliopo.

Wanasimama na sababu za kijinga, ati kuna watanzania wakitikiswa nchi na usalama wa taifa utatikisika.

Kikwete acha maneno maneno kemea rushwa, chukua hatua.
 
Kua aliyewahi kuseama "Tawala zote kubwa zilizo anguka duniani, zilikutwa na maswahibu hayo kutoka na kutokuwa na umakini wa kujua kuwa ardhi waliyo isimamia imeanza kutingishika na kumeguka"

Ninapoona wezi wanatakaswa kuwa safi....naona usemi huu unakaribia kutimia mbele ya macho yetu kwa chama mtawala, hasa nitakapo shuhudia Chenge bib Chenge akiapishwa kuwa Spika wa bunge letu!!!
 
Uongozi wa serikali ya Tanzania ni dhaifu sana, sana. Ukimchukua mgonjwa wa akili pale muhimbili, wodi ya vichaa, na kumweka pale IKULU ya Tanzania atafanya mambo makumbwa ya kimaendeleo kuliko hawa watawala waliopo.

Wanasimama na sababu za kijinga, ati kuna watanzania wakitikiswa nchi na usalama wa taifa utatikisika.

Kikwete acha maneno maneno kemea rushwa, chukua hatua.
Mnanishangaza washikaji kutegemea kikwete kumtaka kuchukua hatua wakati mwenyewe ameiba kura kuingia ikulu. Kwa sasa wana jamvi tu brainstorm ni tuwasaidie vipi wananchi hasa wa vijijini wafahamu ubaya wa ccm kuwasababishia umaskini mkubwa kiasi hicho na wafahamu thamani ya kura yao. kwenye uchaguzi uliopita imeonekana kwenye maeneo yenye umaskini mkubwa ndo kikwete kapata kura nyingi now i am very much worried about this
 
Kwanini hii isitumwe kwa dg wa takukuru kama kuna mtu ana e mail yao maana si wamesema mwenye kujua wala rushwa awasilishe kwao?

Mkuu nakuhakikishia Dr Hossea na TAKUKURU yake wanafahamu yote hayo na hizo barua wanazo ila kama walivyomsafisha Lowassa na Rostam kwenye sakata la Richmond ndivyo hivyo wanafanya kwa Chenge kwa nia kumfanya awe Spika kwa madai kwamba hana hatia vyombo vya habari tu vilikuwa vinachoche bila kujua ukweli wa sakata. JK kama alikuwa na roho ya kumnadi Mramba atashindwa nini pamoja na mafisadi kumtakasa ili awe spika kama Anna Makinda watamwona hataweza.

Kumbuka nia ya CCM, JK na Mafisadi ni kujipanga kwa 2015 kwa kupunguza kelele za wabunge wa upinzani ambazo zinakuwa na 'negative impact' kwa CCM, halafu pia kipindi hiki cha mwisho cha JK atafanya mambo mengi ya hovyo ya kupendelea watu, wizi wa hela na kuharibu uchumi na hata timiza hata nusu ya ahadi zake, hivyo lazima kuhakikisha bunge halipati nafasi ya kujadili mambo hayo na hayatawafikia wananchi wengi
 
Pamoja na haya yote , CCM wakiongozwa na lowassa na rostam wametuletea huyu tahira wakidhani kwamba watu millioni arobaini bado wanaamuliwa na wezi

nina hamu ya kuona wabunge wetu wanajifunza karate ili wakatoane meno bungeni

Chenge, i will drive to dodoma kukutoa meno if need be
 
Siku yaja, tutafukua makuburi yao kuwachapa viboko na kuchunguza bongo zao. Huu ni uhuni wa wazi, sijui kwanini Serikali ya UK inaendelea kuipa TZ misaada kama TAKUKURU wameshindwa kumaliza hiki ambacho SFO wamekifanya. Nimesoma paragraphs mbili ambazo huhitaji hata kuwa na 'interrogation skills' kupata ukweli:

It appears that in breach of Tanzanian law, the Public Leadership Code of Ethics Act 1995 ("Ethics Act"), Chenge has not disclosed assets held in Jersey on the appropriate register. Under the Ethics Acts 1995, Chenge as Attorney General fell within the category of persons obliged to disclosed his worldwide assets annually, on a public register. The SFO has been informed by the PCCB that Chenge has failed to declare any assets on the relevant register
The material obtained fromthe authorities in Jersey also shows that a payment of $600,000 was made from the Franton account controlled by Chenge to an account in the name of Langley Investments Limited ("Langley") in May 1998. That account was controlled by Mr. Idriss Rashidi ("Rashidi")
SFO wametafuna haya majinga yanatuambia yamechunguza wakakosa link; anyway basi mtuambie Chenge na Rashidi walifanya biashara gani mwaka 1998 mpaka kulipana kiasi hicho cha pesa!

Sisi mabwege kweli, kila kitu kiko wazi na SFO wameweka wazi kuwa kuna link, hawa ni watu waliokuwa coordinators wakuu kwenye manunuzi ya radar. Wameonyesha details za transactions zote bado haya majinga yanakuja na majibu rahisi yakiona sisi ni mabwege mtozeni! Tutafukua kaburi la Hosea hata kama hatakuwepo ili tuchunguze UBONGO wake.
 
Chenge mwacheni aweke tu jina lake. Ili Sita ambamize kisawasawa na apte kufahamu kuwa wabunge wanamdharau sana. Tunakuomba Rais na wenzio wa CC msikate jina la Sita. Sita ndiye chaguo letu. Usiruhusu umakamba kwa kukata jina la mtu anayekubalika na wengi. JK I gave you my vote kwa sababu naamini unauchukia ufisadi kama vile Sita anavyouchukia ufisadi. Basi mpeni Sita Uspika.
 
Huyu Chenge anautumiaje uanasheria wake ?
Mtu yeyote mwenye akili ya kawaida ya kuzaliwa hata bila kuona ndani ya darasa alipaswa kuona kuwa HAFAI MBELE YA JAMII YA WATANZANIA na nitatoa sababu:
1. Aliwahi kushika nafasi nyeti na muhimu serikalini ya kuhakikisha maadili, utawala wa kisheria na utawala bora vinazingatiwa.Badala ya kuwa mfano bora, akawa wa kwanza kukiuka misingi ya haya mambo tena mbele ya nyuso za watanzania!..Huwezi ukawa Attorney General unayetegemewa kuwa mshauri mkuu wa mambo ya kisheria kwa serikali na badala yake ukawa wa kwanza kuihujimu serikali hiyo hiyo kwa kuweka mbele maslahi binafsi!

2. Pamoja na dhana ya kuwa huna kosa hadi uthibitishwe na mahakama kuwa una hatia , the mere fact kwamba umeshindwa kujizuia kuingia kwenye utata na mizozo ya kisheria kunaacha maswali mengi sana kuhusu uadilifu na uhalali wa kushika tena nafasi za umma. Kwani kuna Watanzania wangapi "wasafi mbele ya macho ya Watanzania",wenye elimu, maarifa na wajihi na uwezo wa kushika hiyo nafasi ya Uspika?

3.Kwani ni wewe tu Chenge unayestahiki/stahili nafasi zote za juu katika nchi hii? Umeshapita ubunge kwanini usiridhike?

TAFADHALI CHENGE..GIVE TANZANIANS A BREAK!
 
Back
Top Bottom