Gembe
JF-Expert Member
- Sep 25, 2007
- 2,483
- 159
Mheshimiwa Waziri mkuu,
Awali ya yote naomba kukupongeza kwa hatua yako ya kuzungumzia suala la DECI,na kuonehsa jinsi suala hilolilivyo la kihalifu,Umefanya vyema sana kwa kuwa kwa baadaye litakuwa tatizo la serikali pindi wannachi watakapoanza kudai pesa zao.Pia ningependa kukopongeza kwa juhudi zako za kuokoa pesa za wananchi zinazopotea katika stendi ya ubungo
ambao ni uhalifu mwingine ambao unamhusu kada wa chama chako ambaye hana uwezo wa kuona mandishi madogo mpaka ulipoweka miwani yako
Mhe waziri mkuu kwa tafsiri ya karibu kabisa uhalifu ni uvunjaji wa sheria kwa kuiba kwa njia mbalimbali,aidha kwa mtandao,au uvamizi na mara zote hatua kali huchukuliwa kwa watu wanaotenda uhalifu.
Baada ya kusema hayo naomba nianze na maelezo yangu ya awali.Ni jambo lililozooleka sana kwa watu kupanga njama na kufanikisha wizi wa mabilioni ya pesa kwa njia zisizo kihalali,chukulia mfano wa suala la wizi wa Pesa Za EPA,KAGODA,IMPORT SUPPORT,RDC na wizi wa mabilioni ya pesa unaotekea katika wizara na ofisi nyingi za serikali.Kwa tafsiri yako huu wote ni uhalifu tena wa wa muda mrefu na inawezekana unaujua vyema sana kutokana na wewekufanya kazi katika wizara ya tawala za mikoa na serikali za Mitaa
Mhe. Pinda kwa maoni yangu kabla ya kuanza na DECI ,ama hatua ambazo umepanga kuzichukua kwa watu wa DECI ningeomba uanze na wahalifu hawa ambo wako karibu yako na unafanya nao kazi kila siku.Hawa ndiyo wanochochoea uhalifu mwingine sababu watu wanaona maovu yanatokea na wanatafuta mbinu za kujitafutia Pesa.Na kwa kuwa wanacci wana maisha magumu,wamekata tamaa na umasikini wa muda mrefu wanatumbikia katika shimo hili la waharamia wnaofanya biashara haramu
CHIMBUKO LA DECI
Mhe waziri mkuu utakumbuka moja ya kauli mbinu iliyotumiwa kumnadi Rais kikwete ni kuwapa watanzania maisha bora kwa kutumia chachandu ya Tanzania yenye neema inawezekana.Kauli mbinu hii ilichochoea wananchi kumpa mwenyekiti wetu wa CCM kura nyingina kusema kweli wakati huo kwa kweli 'zilitosha'.
Wananchi 430,276 kwa mujibu wa takwimu za DECI ndiyo wnachama wa DECI,hawa ndiyo wale watu waliokata tamaa ya kukosa maisha bora na wnaona ni bora na DECI kuliko serikali,DECI imewapatia maisha bora walimu,mapolisi,wanajeshi na waumini wa madhehebu mbali mbali!maisha bora wakliyoyakosa kwa muda mrefu na hawa ndiyo hawakufaidika na yale 'mabilioni'
Mhe waziri mkuu,ukiangalia historia ya mabenki yetu ya ndani na vyombo ambavyo hukopesha pesa kama Bayport,FINCA na PRIDE ni kuwa ,yanatoza riba za juu sana ambazo hata kam mwananchi akikopa pesa na kuzifanyia biahsara hawezi kufaidika na hiyo pesa sababu pesa yote itaishia katika matumizi ya kawaida tu na kulipa deni.
Benki nyingi na vyombo vya kifedha hukopesha kwa riba ya asilimia 19 hadi 22 kwa watu wa maisha ya chini,hivyo kuwa wia vigumu wanachi wengine kurudisha pesa hizo,suala hili linachangia watu wengi kutafuta pesa za haraka na ikitokea kitu kama DECI wanachi wanakuwa wa kwanza kuchangamkia.Wanachi wamezwe kutambua kuwa "hauwezi kula kwanza mpaka uliwe"na ndiyo mana wako DECI.
Kimsingi DECI ni utapeli na naungana nwa ewe katika hilo,sababu biahsara yoyote ambayo inaingiza faida zaidi ya asilimia 40 ni kamali,hivyo unaweza kuliwa ama kula kwa faida itakayoaanishwa na wamiliki wa hiyo kamali.
HATUA ZA KUCHUKUA KUHUSIANA NA DECI
1.Hatua ya kwanza ni serikali kukaa na watu wa DECI na kuzungumza nao kujua pesa za wanachama ziko wapi na nia yenu kama serikali kuhusiana na mchezo huo.
2.Nyie kama Serikali muangalie uwezekna wa kuiweka pesa hiyo katika mizunguko ya kibenki na kuona ni faida gani halisi inaweza kupatikana kama pesa hiyo ya wanchi ikiwekwa kwa mfumo wa FIxed deposit inaweza kupatika.Faida hiyo ndiyo mwashauri DECI waitoe kwa wanachi,inawezekan kama ukiwekza benki Billioni 13 unapata 10% kwa mwaka basi igawiwe kwa wananchi kama faida kwa pesa zao.
3.Kama ni vigumu kwa hilo basi Serikali iwashauri wananchi kuwa pesa yao itaingizwa katika benki mojawapo inayomilikiwa
na serikali na wawe kama wamenunu a HISA.
4.Kama ikishindikana kabisa,Funga DECI na wananchi warudishiwe Pesa zao kama walivyopanda!
HITIMISHO
Mhe waziri mkuu,naamini sasa umetambua ni kwa kiasi gani watanzania wengi walivyo na masiah duni ukiangalia kwa undani zaidi ya asilimia 30% ya watanzania hawajui kesho watakula nini na pia hawajui nchi inakwenda wapi na hili ni Tatizo.Mie nina uhakika leo ukiuliza swali kwa waziri mmojawapo ni nini mipango ya wizara yake kwa mwak 2011 hatakuwa hajui.
Tatizo hili ni la muda mrefu na ni bomu ambalo tunalitengeneza wenywe,embu kwa kuanzia hapa naomba muandae Program ya muda mrefu ya kuondoa umasikini na tuachane na Mkurabita,Mkumbita na TASAF sababu zimeshindwa kubadili chochote.Tujifunze mbinu kutoka nchi zingine kama Gambia na Noth Korea na hata nchi nyingine zenye misingi mizuri ya kimaendeleo.
Mie nina imani kubwa kama tukitumia watalaam Wazalendo,wenye uchungu na nchi hii basi mpango mkakati wa kiuchumi utalisaidia taifa hili kuondokana na umasikini wa muda mrefu.Tuachane na wataala wa Serikali wa muda mrefu waliozoea "copy and Paste".Tuangaze vijana wasomi waliopo katika sekta mbalimbali na kuwatumia katika kuimarisha uchumi wa nchi hii kwa mipango mizuri.
Mheshimiwa Waziri mkuu,naomba sasa kuhitimisha kwa kukuomba uanze kushghulikia wahalifu wakubwa waliokuzunguka na nikipata nafasi nitakuletea barua ofisini kwako.
Mhe. Pinda tuache kulalamika kila siku,wananchi wanalamika na nyie pia?tuwasaidie watanzania wenzetu sasa na tuache kupiga porojo kwa kuunda tume kila siku zisizo na tija wala mafanikio.
YES I have said "TANZANIA YENYE NEEMA INAWEZEKANA KAMA UKIONDOA WAHALIFU WALIOKUZUNGUKA"
wako Mwenye upeo na mwenye upendo wa Nchi yangu,
GEMBE
Awali ya yote naomba kukupongeza kwa hatua yako ya kuzungumzia suala la DECI,na kuonehsa jinsi suala hilolilivyo la kihalifu,Umefanya vyema sana kwa kuwa kwa baadaye litakuwa tatizo la serikali pindi wannachi watakapoanza kudai pesa zao.Pia ningependa kukopongeza kwa juhudi zako za kuokoa pesa za wananchi zinazopotea katika stendi ya ubungo
ambao ni uhalifu mwingine ambao unamhusu kada wa chama chako ambaye hana uwezo wa kuona mandishi madogo mpaka ulipoweka miwani yako
Mhe waziri mkuu kwa tafsiri ya karibu kabisa uhalifu ni uvunjaji wa sheria kwa kuiba kwa njia mbalimbali,aidha kwa mtandao,au uvamizi na mara zote hatua kali huchukuliwa kwa watu wanaotenda uhalifu.
Baada ya kusema hayo naomba nianze na maelezo yangu ya awali.Ni jambo lililozooleka sana kwa watu kupanga njama na kufanikisha wizi wa mabilioni ya pesa kwa njia zisizo kihalali,chukulia mfano wa suala la wizi wa Pesa Za EPA,KAGODA,IMPORT SUPPORT,RDC na wizi wa mabilioni ya pesa unaotekea katika wizara na ofisi nyingi za serikali.Kwa tafsiri yako huu wote ni uhalifu tena wa wa muda mrefu na inawezekana unaujua vyema sana kutokana na wewekufanya kazi katika wizara ya tawala za mikoa na serikali za Mitaa
Mhe. Pinda kwa maoni yangu kabla ya kuanza na DECI ,ama hatua ambazo umepanga kuzichukua kwa watu wa DECI ningeomba uanze na wahalifu hawa ambo wako karibu yako na unafanya nao kazi kila siku.Hawa ndiyo wanochochoea uhalifu mwingine sababu watu wanaona maovu yanatokea na wanatafuta mbinu za kujitafutia Pesa.Na kwa kuwa wanacci wana maisha magumu,wamekata tamaa na umasikini wa muda mrefu wanatumbikia katika shimo hili la waharamia wnaofanya biashara haramu
CHIMBUKO LA DECI
Mhe waziri mkuu utakumbuka moja ya kauli mbinu iliyotumiwa kumnadi Rais kikwete ni kuwapa watanzania maisha bora kwa kutumia chachandu ya Tanzania yenye neema inawezekana.Kauli mbinu hii ilichochoea wananchi kumpa mwenyekiti wetu wa CCM kura nyingina kusema kweli wakati huo kwa kweli 'zilitosha'.
Wananchi 430,276 kwa mujibu wa takwimu za DECI ndiyo wnachama wa DECI,hawa ndiyo wale watu waliokata tamaa ya kukosa maisha bora na wnaona ni bora na DECI kuliko serikali,DECI imewapatia maisha bora walimu,mapolisi,wanajeshi na waumini wa madhehebu mbali mbali!maisha bora wakliyoyakosa kwa muda mrefu na hawa ndiyo hawakufaidika na yale 'mabilioni'
Mhe waziri mkuu,ukiangalia historia ya mabenki yetu ya ndani na vyombo ambavyo hukopesha pesa kama Bayport,FINCA na PRIDE ni kuwa ,yanatoza riba za juu sana ambazo hata kam mwananchi akikopa pesa na kuzifanyia biahsara hawezi kufaidika na hiyo pesa sababu pesa yote itaishia katika matumizi ya kawaida tu na kulipa deni.
Benki nyingi na vyombo vya kifedha hukopesha kwa riba ya asilimia 19 hadi 22 kwa watu wa maisha ya chini,hivyo kuwa wia vigumu wanachi wengine kurudisha pesa hizo,suala hili linachangia watu wengi kutafuta pesa za haraka na ikitokea kitu kama DECI wanachi wanakuwa wa kwanza kuchangamkia.Wanachi wamezwe kutambua kuwa "hauwezi kula kwanza mpaka uliwe"na ndiyo mana wako DECI.
Kimsingi DECI ni utapeli na naungana nwa ewe katika hilo,sababu biahsara yoyote ambayo inaingiza faida zaidi ya asilimia 40 ni kamali,hivyo unaweza kuliwa ama kula kwa faida itakayoaanishwa na wamiliki wa hiyo kamali.
HATUA ZA KUCHUKUA KUHUSIANA NA DECI
1.Hatua ya kwanza ni serikali kukaa na watu wa DECI na kuzungumza nao kujua pesa za wanachama ziko wapi na nia yenu kama serikali kuhusiana na mchezo huo.
2.Nyie kama Serikali muangalie uwezekna wa kuiweka pesa hiyo katika mizunguko ya kibenki na kuona ni faida gani halisi inaweza kupatikana kama pesa hiyo ya wanchi ikiwekwa kwa mfumo wa FIxed deposit inaweza kupatika.Faida hiyo ndiyo mwashauri DECI waitoe kwa wanachi,inawezekan kama ukiwekza benki Billioni 13 unapata 10% kwa mwaka basi igawiwe kwa wananchi kama faida kwa pesa zao.
3.Kama ni vigumu kwa hilo basi Serikali iwashauri wananchi kuwa pesa yao itaingizwa katika benki mojawapo inayomilikiwa
na serikali na wawe kama wamenunu a HISA.
4.Kama ikishindikana kabisa,Funga DECI na wananchi warudishiwe Pesa zao kama walivyopanda!
HITIMISHO
Mhe waziri mkuu,naamini sasa umetambua ni kwa kiasi gani watanzania wengi walivyo na masiah duni ukiangalia kwa undani zaidi ya asilimia 30% ya watanzania hawajui kesho watakula nini na pia hawajui nchi inakwenda wapi na hili ni Tatizo.Mie nina uhakika leo ukiuliza swali kwa waziri mmojawapo ni nini mipango ya wizara yake kwa mwak 2011 hatakuwa hajui.
Tatizo hili ni la muda mrefu na ni bomu ambalo tunalitengeneza wenywe,embu kwa kuanzia hapa naomba muandae Program ya muda mrefu ya kuondoa umasikini na tuachane na Mkurabita,Mkumbita na TASAF sababu zimeshindwa kubadili chochote.Tujifunze mbinu kutoka nchi zingine kama Gambia na Noth Korea na hata nchi nyingine zenye misingi mizuri ya kimaendeleo.
Mie nina imani kubwa kama tukitumia watalaam Wazalendo,wenye uchungu na nchi hii basi mpango mkakati wa kiuchumi utalisaidia taifa hili kuondokana na umasikini wa muda mrefu.Tuachane na wataala wa Serikali wa muda mrefu waliozoea "copy and Paste".Tuangaze vijana wasomi waliopo katika sekta mbalimbali na kuwatumia katika kuimarisha uchumi wa nchi hii kwa mipango mizuri.
Mheshimiwa Waziri mkuu,naomba sasa kuhitimisha kwa kukuomba uanze kushghulikia wahalifu wakubwa waliokuzunguka na nikipata nafasi nitakuletea barua ofisini kwako.
Mhe. Pinda tuache kulalamika kila siku,wananchi wanalamika na nyie pia?tuwasaidie watanzania wenzetu sasa na tuache kupiga porojo kwa kuunda tume kila siku zisizo na tija wala mafanikio.
YES I have said "TANZANIA YENYE NEEMA INAWEZEKANA KAMA UKIONDOA WAHALIFU WALIOKUZUNGUKA"
wako Mwenye upeo na mwenye upendo wa Nchi yangu,
GEMBE
Last edited: