PostGE2025 Balozi wa Tanzani UN-DR. Abdallah Possi azimiwa mic na hotuba yake nzito yenye maelezo ya kweli na ya kina kuhusu uchaguzi wa Tanzania2025 yakatishwa

PostGE2025 Balozi wa Tanzani UN-DR. Abdallah Possi azimiwa mic na hotuba yake nzito yenye maelezo ya kweli na ya kina kuhusu uchaguzi wa Tanzania2025 yakatishwa

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections
Hongera sana Mkuu Tila, huu ndio uzalendo wa kweli wa taifa hili na hili ni bandiko la kizalendo kuonyesha jinsi Balozi wetu alivyozimiwa mic!, japo mimi sikubaliani na wewe, kuhusu hizo dosari na changamoto ndogondogo za uchaguzi, kama kweli ni dosari na changamoto ndogondogo za uchaguzi then kwanini serikali yetu ilitumia risasi za moto?.
P
Uzalendo ni kuvaa maskafu tu, wala sio kupandisha habari za balozi wetu.
 
Duh,
Huyu mhuni, muongo, mzushi, chawa ni dr wa nini?
zingatia ukweli uliowakera mabwenyenye gentleman mpaka wakamzimia mic, hakuna haja ya kumbwelambwela na mamabo yasiyo muhimu gentleman
 
Wauaji wanajua sana kupamba story zao. Wanaweza mazingira Sawa ili jumuiya ya kimataifa wasahau waendelee kuua. Kuendelea kuwasikiliza wakipamba mauaji yao ni maumivu makubwa yasiyovumilika. Ni Sawa alivyozimiwa mic
 
Siyo kweli.
Hivyo vikao ni vikao vya watu wenye akili timamu, siyo vikao vya CCM. Watu wana mambo mengi ya kujadili, wewe ukienda kwa dhamira ya kueleza uwongo, ni sahihi kuzimiwa mic, hata kutolewa nje ya kikao. Ni sawa na mtu mnamwona kabisa ni mwanaume, halafu jitu linawapotezea muda eti liwafafanulie kuwa huyo ni mwanamke!
Fikiria ule ushetani uliofanywa na wauaji ile Oct 29, halafu jitu linakupotezea muda kukueleza kuwa hakukuwa na tatizo!! Huyo si anawafanya wote hawana akili!
Huwezi zimia mtu mic vikao vya UN,hata iwe vipi,hapo wameonesha ujinga,hivyo siyo vikao vya jumuiya,mahari etc
 
Ccm waliwashurutisha walimu waibe kura kwani nani hajui?
 
Umeshamuomba msamaha mdogo wako mchemba kwa kumuingilia mawazo yake kumsemea aliumia huku yeye hakuumia kutoshangiliwa au upo tu humu unasifia sifia ujinga?

Ameonyesha uzalendo gani huyo hata umuite mzalendo!
Hujamuelewa ujumbe uliojificha.
Kampiga kijembe. Kamdhihaki na kumpinga huyo chawa.
 
Posi, mwana aliyekuzwa wazazi wakila mema ya nchi kwa sababu ya CCM, atatetea nini zaidi ya CCM...

Mara zote amekuwa akifanya hivyo huko UN...

Yah possi mboga 8 kitambo sana,watu wa hivyo ujiona wao ndio wenye haki ya kula mema ya nchi na vizazi vyao
 
Mtu umempa nafasi ya kujieleza, halafu unamzimia mic!..hawa si ndiyo wanaohubiri freedom of expression?
Kama anaongea utumbo,imagine mtu anatetea kuuliwa kwa risasi kwa watu ambao awakua na silaha ya aina yoyote,tena wengine wameuliwa wakiwa majumbani kwao
 
Kama anaongea utumbo,imagine mtu anatetea kuuliwa kwa risasi kwa watu ambao awakua na silaha ya aina yoyote,tena wengine wameuliwa wakiwa majumbani kwao
Waliwahi zima mic vikao kama hivyo vya kuishutumu Israel mauaji ya Gaza mwaka Jana?
 
Akihutubia na kutoa majibu na ufafanuzi muhimu sana dhidi ya upotosha uliotolewa na mataifa mablimbali kuhusu matukio ya kabla ya uchaguzi mkuu, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi mkuu huru, wa wazi na wa haki uliofanyika Oct.29,2025, makamo wa rais wa kikao hicho cha baraza alionekana kukerwa na ukweli wa balozi dr. Possi na kulazimika kumzimia mic na kukatisha hotuba ya Dr.Possi iliyojaa mambo muhimu na ya msingi zaidi dunia kufahamu.

Akihutubia kikao cha 61 cha baraza la haki za binadamu, Dr.Possi ameeleza kusikitishwa na taarifa za kupotosha za upande moja za mataifa na taasisi kadhaa za kimataifa, huku kwa makisudi wakifumbia macho ukweli halisi juu ya kilichotokea Oct.29.2025.

Kiukweli, balozi Dr. Abdalah Possi ni mtu na nusu mbele ya mabwenyenye ya magharibi, ambao walikua kimya mno wakati balozi akiudadavua na kuweka wazi kweli mtupu dhidi ya uongo wao mabwenyenye, balozi Possi aliweka bayana namana serikali sikivu ya CCM chini ya Dr.Samia Suluhu Hassan, ilivyosimamia na ilivyoshughulikia dosari na changamoto ndogondogo za uchaguzi kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi.

Sikiliza hotuba hiyo ya maana na ya kihistoria, lakini pai shuhudia namna hotuba hiyo muhimy ya balozi Possi, livyokatishwa kihuni.

Mungu Ibariki Tanzania

View: https://youtu.be/NQTikDfGIIU?si=UnE3agEAaFciz8Lb

Hakumzimia maiki muda ulimalizika, sawa sawa na wabunge wanavyopewa dakika 15 bungeni kutoa hoja zao, muda ulimalizika.
 
Kama hotuba nzuri kwanini uzimiwe maiki

Maana yake ilikuwa inaboa masikioni mwao

Mbona wengine hawakuzimiwa maiki kwanini yeye tu
 
Akihutubia na kutoa majibu na ufafanuzi muhimu sana dhidi ya upotosha uliotolewa na mataifa mablimbali kuhusu matukio ya kabla ya uchaguzi mkuu, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi mkuu huru, wa wazi na wa haki uliofanyika Oct.29,2025, makamo wa rais wa kikao hicho cha baraza alionekana kukerwa na ukweli wa balozi dr. Possi na kulazimika kumzimia mic na kukatisha hotuba ya Dr.Possi iliyojaa mambo muhimu na ya msingi zaidi dunia kufahamu.

Akihutubia kikao cha 61 cha baraza la haki za binadamu, Dr.Possi ameeleza kusikitishwa na taarifa za kupotosha za upande moja za mataifa na taasisi kadhaa za kimataifa, huku kwa makisudi wakifumbia macho ukweli halisi juu ya kilichotokea Oct.29.2025.

Kiukweli, balozi Dr. Abdalah Possi ni mtu na nusu mbele ya mabwenyenye ya magharibi, ambao walikua kimya mno wakati balozi akiudadavua na kuweka wazi kweli mtupu dhidi ya uongo wao mabwenyenye, balozi Possi aliweka bayana namana serikali sikivu ya CCM chini ya Dr.Samia Suluhu Hassan, ilivyosimamia na ilivyoshughulikia dosari na changamoto ndogondogo za uchaguzi kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi.

Sikiliza hotuba hiyo ya maana na ya kihistoria, lakini pai shuhudia namna hotuba hiyo muhimy ya balozi Possi, livyokatishwa kihuni.

Mungu Ibariki Tanzania

View: https://youtu.be/NQTikDfGIIU?si=UnE3agEAaFciz8Lb

Ujue kama marekani anamiliki settlite tatu..

Maduro anafuatwa chumbanii anakuja kuamka yupo ummatekani..

AYATOLLAH KHEMENEI SUPREME LEADER ANAKUTWA NA MAUTI KWENYE PRIMISES YAKE.

NB. Mtu mstaarabu HUWA HAWAVUMILII U k*m* mayooo
 
Ulitaka wafanyweje wale wahalifu?
Dosari za uchaguzi hata zingekua kubwa ndiyo wafanye uhalifu waliofanya?..vituo vya mwendokasi viliwakosea nini,sheli za watu ziliwakosea nini,kwa nini walipora?
Wahalifu walikamatwa na Samia akatoa msamaha waachiwe ila watu wanazungumzia yale mauwaji ya polisi kwa raia.
 
Back
Top Bottom