Balozi Mulamula Kugombea Nafasi ya Katibu Mkuu wa CommonWealth

Balozi Mulamula Kugombea Nafasi ya Katibu Mkuu wa CommonWealth

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
79,084
Reaction score
84,976
Nafasi anayogombea Mulamula ndio nafasi ambayo Membe aliomba na kuchinjiwa baharini na Mwendazake 🤪🤪.

Rais Samia hana kinyongo so ameamua kumbeba Balozi Mulamula..

---
RAIS Samia Suluhu Hassan ameridhia Balozi Liberata Mulamula kugombea nafasi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola akiamini kuwa kutokana na uzoefu wake mkubwa katika masuala ya diplomasia atakuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha uhusiano wa Tanzania na jumuiya hiyo.

Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa aliliambia HabariLEO kuwa kuchaguliwa kwa Balozi Mulamula ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Afrika Mashariki kutakuwa na manufaa makubwa kwa kuwa atasaidia baadhi ya ajenda za Tanzania kuzingatiwa ndani ya jumuiya.

“Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imepitisha jina lake na inamuunga mkono kwa sababu inaamini juu ya uwezo wake, ataiwakilisha nchi vizuri, atakuwa balozi mzuri kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla,” alisema.

Msigwa aliwaomba wajumbe watakaohusika katika kumpitisha Balozi Mulamula kumpa kura za kutosha kwa sababu atatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya jumuiya hiyo na dunia kwa ujumla.

Imeandaliwa na Selemani Nzaro

Habari Leo​

 
Wasira hajakosea ccm Ina watu wenye nongwa ,fitina na majungu
Jumuiya hii inayoongozwa na Ufalme dhalimu na wakibeberu ambao umewahi kutokea katika karne hizi za karibuni, siyo ya kupewa kipaumbele na mpenda haki, mzalendo, na Mwafrika yeyote yule.

Sina nongwa, wala jungu na huyu bibie Balozi, ni haki yake, ila naye asome nyakati, Ufalme wa Uingereza ume wanyanyasa sana Wananchi wa Jumuiya hii. Hivi majuzi tu baada ya uchunguzi(wala sijui ulikuwa na jukumu lipi)Umebaini .....kitu ambacho kilikuwa dhahiri halafu kinabaini tena?......umebaini.... na ninanukuu...."Kulingana na wanahistoria wafalme 12 wa Uingereza walidhamini, kuunga mkono au kufaidika na ushiriki wa Uingereza katika utumwa, Kutoka Elizabeth I hadi William IV, tena kwa kipindi cha miaka 270!!" ... walikuwa na uhusiano na biashara hiyo.
Mpaka leo hii hawataki kabisa kukubali udhalimu wao na wanaendeleza haya "Ukoloni mamboleo" kupitia Jumuiya hii.

Tunapigiana kelele kuhusiana na Katiba yetu wakati ni Lazima narudia ni Lazima Mfalme wa Uingereza akubali na kuridhia mchakato mzima wa Kuwa na Katiba mpya! Sasa kwanini tusijitoe, tupate Katiba isiyo na Vishinikizo, halafu turidhie maungano na Jumuiya hii?
 
Nafasi anayogombea Mulamula ndio nafasi ambayo Membe aliomba na kuchinjiwa baharini na Mwendazake 🤪🤪.

Rais Samia hana kinyongo so ameamua kumbeba Balozi Mulamula..


Kwa kipindi nimemfahamu sijawahi kuvutiwa na utendaji wake, zaidi zaidi huwa nakerwa na mbwembwe zake na kuchekacheka bila sababu za msingi
 
Nitawaadithia wajukuu zangu kuhusu wale ninaowaita vibaraka wa mabeberu, kwa sababu huo ndio Ukweli. Kuwemo ndani ya Jumuiya ya Madola ni kukubali Udhalimu wa Ufalme wa Kingereza pamoja na Ukoloni mamboleo unaotoka ndani ya dhamira kuu ya Jumuiya hiyo.....ni karaaaha.
Kwenda kuwakilisha au kuuwakilisha ni kujidharau.l na Kujidhalilisha.
 
Nafasi anayogombea Mulamula ndio nafasi ambayo Membe aliomba na kuchinjiwa baharini na Mwendazake 🤪🤪.

Rais Samia hana kinyongo so ameamua kumbeba Balozi Mulamula..



Wasira hajakosea ccm Ina watu wenye nongwa ,fitina na majungu

Ana uwezo mdogo hafai ungesema Tax ningekuelewa anaweza! Mulamula anachekachaka tu hawezi

Kwa kipindi nimemfahamu sijawahi kuvutiwa na utendaji wake, zaidi zaidi huwa nakerwa na mbwembwe zake na kuchekacheka bila sababu za msingi
Wasira hajakosea ccm Ina watu wenye nongwa ,fitina na majungu
Hakika hajakosea kuna watu wananongwa
 
Usijifanye unashangaa Choisi jibu hoja kinachokushangaza

haha na pacha wako wa kujibishana.....😉
😆😆😆 what an introduction.
 
huu ndio ulikiwa wakati muafaka kujiondoa katia hii Jumuiya. Anaenda kutafuta nini huko? Hakuna kitu chochote kilichokuwa common zaidi ya kujidhalilisha kwa, na kuwakilisha ubeberu kwa wananchi wetu.

Aluta Continua
Wapumbavu hawajifichi siku hizi, hujitokeza wenyewe. Yote majitu yenye akili kama SYLLOGIST! ni masalia ya Magufuli.

Go Go Mulamula hiki kizazi kisichojua English na kinachopenda kujifungia Kolomije au Chato tulikizika Machi, 2021
 
Wapumbavu hawajifichi siku hizi, hujitokeza wenyewe. Yote majitu yenye akili kama SYLLOGIST! ni masalia ya Magufuli.
Ipo siku utapona kwa Usongo na Huzuni. Wataalamu wanasema umefikia stage ya makasiriko, ni mwendo pia wa kawaida kwa mfiwa, ila utafika.
GoGo Mulamula hiki kizazi kidichojua English na kinachopenda kujifungia Kolomije au Chato tulikizika Machi, 2021
Balozi wetu huyi ninamuheshimu sana tu, ni gwiji wa Diplomasia na ninaelewa hivyo.....Hana haja ya kuwa kibaraka wa ukoloni mamboleo. Ni hilo tu. Usihadae na kutaka kuaminisha ninamuekea kigingi.
 
Ipo siku utapona kwa Usongo na Huzuni. Wataalamu wanasema umefikia stage ya makasiriko, ni mwendo pia wa kawaida kwa mfiwa, ila utafika.

Balozi wetu huyi ninamuheshimu sana tu, ni gwiji wa Diplomasia na ninaelewa hivyo.....Hana haja ya kuwa kibaraka wa ukoloni mamboleo. Ni hilo tu. Usihadae na kutaka kuaminisha ninamuekea kigingi.
Kibaraka wa ukoloni mamboleo ndiyo kitu gani?
 
Kumbe membe alichinjiliwa mbali, safi sana 💪
Namtakia heri na mafanikio balozi Mulamula ✌️
 
Back
Top Bottom