BAKITA mbadili huu msamiati dhalili

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Mzungu mmoja aliwahi kunikebehi akasema sisi Waafrika kwy Kiswahili tunamuita mtu toka nchi za Magharibi Mzungu, akaniambia ebu sasa ondoa herufi z kwenye neno Mzungu alafu ulisome.

Akajinasibu kwamba Mzungu ni mungu wa weusi ndiyo maana tunawategemea kwa kila kitu hata kibovu, yakiwemo mawazo.

Bakita badilini huu msamiati dhalili kwetu. Hautufai. Kiswahili ni tajiri wa misamiati tutafutieni mwingine.

Vinginevyo tukusanye saini za watu tukaiombe Mahakama iufute toka kwenye matumizi.

Lakini mjuwe kama hamjaandaa msamiati mbadala patakuwa na ombwe endapo Mahakama itachukuwa hatua mapema.

Aidha, sina hakika aliyebuni msamiati huu ni nani hasa na kama hakupewa chochote kitu na hawa miungu mieupe ya Afrika!

Nawasilisha.
 
Nilishawahi kusema hili jambo hapa JF.

Ila sikutaka BAKITA wabadili msamiati.

Kiswahili ni lugha inayopangwa na watu, haipangwi na BAKITA.

Kuna nchinkama Ufaransa ambayo lugha inaoangwa na baraza la lugha.

Ndiyo maana kuna maneno watu wanayaanzisha mtaani, halafu yanakuja kukubalika.
 
Mzungu mmoja aliwahi kunikebehi akasema sisi Waafrika kwy Kiswahili tunamuita mtu toka nchi za Magharibi Mzungu, akaniambia ebu sasa ondoa herufi z kwenye neno Mzungu alafu ulisome.

Akajinasibu kwamba Mzungu ni mungu wa weusi ndiyo maana tunawategemea kwa kila kitu hata kibovu, yakiwemo mawazo.

Bakita badilini huu msamiati dhalili kwetu. Hautufai. Kiswahili ni tajiri wa misamiati tutafutieni mwingine.

Vinginevyo tukusanye saini za watu tukaiombe Mahakama iufute toka kwenye matumizi.

Lakini mjuwe kama hamjaandaa msamiati mbadala patakuwa na ombwe endapo Mahakama itachukuwa hatua mapema.

Aidha, sina hakika aliyebuni msamiati huu ni nani hasa na kama hakupewa chochote kitu na hawa miungu mieupe ya Afrika!

Nawasilisha.
Naunga mkono hoja,
Mzungu ndio nini, ila twaweza kubadili sie wenyewe tukitaka,

Buni jina moja
 
Nilishawahi kusema hili jambo hapa JF.

Ila sikutaka BAKITA wabadili msamiati.

Kiswahili ni lugha inayopangwa na watu, haipangwi na BAKITA.

Kuna nchinkama Ufaransa ambayo lugha inaoangwa na baraza la lugha.

Ndiyo maana kuna maneno watu wanayaanzisha mtaani, halafu yanakuja kukubalika.
Sasa BAKITA wana sheria/kanuni inayowapa mamlaka ya kumchukulia mtu hatua za kisheria kwa kosa la kubuni misamiati bila kurasimishwa na BAKITA au kubadili maana ya misamiati iliyopo.

Kuna uchafuzi mwingi wa lugha adhimu ya Kiswahili. Mifano hii hapa:-

1. Kalamu - Peni/pen.

2. Butcher. Kiswahili chake ni nini? Je, ukiandika kwa Kiswahili Bucha nyama haitanunulika? Au watu watakuja kuulizia mkaa badala ya nyama? Je, butcher/butchery ni mchinjaji? Machinjio? Duka la kuuzia nyama? Tuko sahihi tukisema Meat Shop badala ya butcher? Je, meat shop ni Kiswahili?

3. Markiti toka Market badala ya soko.

4. Skuli toka School badala ya shule.

5. Namba 4 na 5 hazijatokana na kibantu zimetokana na English ambayo siyo kibantu.

BAKITA inachelewesha Kiswahili kusambaa. Nchi zilizohitaji Walimu wa Kiswahili zinatumia vitabu vya Kiswahili vya Kiada na Ziada to DR Congo na Kenya, Tz imepigwa bao.

Watz, wajinga ndiyo waliwao.

Siku Kenya wakisema Kiswahili ni chao tunaanza kuwakatalia kama tunavyowakatalia mlima Kilimanjaro. Hata wakati mlima unapigiwa kura duniani, kura za Tz zilikuwa chache kuliko za Kenya.
 
Sasa BAKITA wana sheria/kanuni inayowapa mamlaka ya kumchukulia mtu hatua za kisheria kwa kosa la kubuni misamiati bila kurasimishwa na BAKITA au kubadili maana ya misamiati iliyopo.

Kuna uchafuzi mwingi wa lugha adhimu ya Kiswahili. Mifano hii hapa:-

1. Kalamu - Peni/pen.

2. Butcher. Kiswahili chake ni nini? Je, ukiandika kwa Kiswahili Bucha nyama haitanunulika? Au watu watakuja kuulizia mkaa badala ya nyama? Je, butcher/butchery ni mchinjaji? Machinjio? Duka la kuuzia nyama? Tuko sahihi tukisema Meat Shop badala ya butcher? Je, meat shop ni Kiswahili?

3. Markiti toka Market badala ya soko.

4. Skuli toka School badala ya shule.

5. Namba 4 na 5 hazijatokana na kibantu zimetokana na English ambayo siyo kibantu.

BAKITA inachelewesha Kiswahili kusambaa. Nchi zilizohitaji Walimu wa Kiswahili zinatumia vitabu vya Kiswahili vya Kiada na Ziada to DR Congo na Kenya, Tz imepigwa bao.

Watz, wajinga ndiyo waliwao.

Siku Kenya wakisema Kiswahili ni chao tunaanza kuwakatalia kama tunavyowakatalia mlima Kilimanjaro. Hata wakati mlima unapigiwa kura duniani, kura za Tz zilikuwa chache kuliko za Kenya.
Lugha zote zinakwenda kwa misamiati inayobuniwa na watu.

Kila mwaka utasikia Oxford wameingiza maneno mapya kwenye kamusi yao ya Kiingereza, maneno yatambulike rasmi, kwa sababu inaonekana yanatumika sana.

Kuna waingereza mpaka leo hawapendi kutumia maneno kama "boss", kwa sababu zamani hili neno lilikuwa slang, leo linatambulika kama Kiingereza rasmi. Sasa wale wahafidhina hawapendi maneno kama haya.

Wataalam walijaribu kutunga lugha zao zinazotungwa na mabaraza, kama Esperanto.

Zimekufa kutokana na kutokuwa na nguvu ya umma.

Kama neno "Mzungu" linatudhalikisha, watu wapewe elimu, wajue, watalikataa wenyewe.

Kama ni sehemu ya utamaduni wetu tu, watu wataamua wenyewe.

Hatuhitaji kushikiwa kiboko na BAKITA. Watu, wakishakuwa nanm elimu, ndio wataielekeza BAKITA.

Kuna mtu anakijua na kukipenda Kiswahili kuliko Rais Ali Hassan Mwinyi hapa?

Mzee Mwinyi kaandika kitabu "Mzee Rukhsa: Safari ya Maisha Yangu". Kitabu kina maneno mengi tu ya mtaani, hususan yaliyotumika katika uongozi wake. Kwa sababu Mwinyi, gwiji la Kiswahili, anajua kwamba maneno yale yanawakilisha moja kwa moja hata hisia ya wakati ule tu, na mengi yalianza kama maneno ya mtaani (slang), lakini yakaja kukubalika kwenye Kiswahili rasmi.

Lugha inakua, na inakuzwa na watu, si mabaraza.
 
Lugha zote zinakwenda kwa misamiati inayobuniwa na watu.

Kila mwaka utasikia Oxford wameingiza maneno mapya kwenye kamusi ya Kiingereza, maneno yatambulike rasmi, kwa sababu inaonekana yanatumika sana.

Wataalam walijaribu kutunga lugha zao zinazotungwa na mabaraza, kama Esperanto.

Zimekufa kutokana na kutokuwa na nguvu ya umma.
Kiswahili kila nchi Maziwa Makuu ina kamusi yake. Kenya computer wanaita Tarakishi. Tz hatujabuni msamiati wa neno la Kiingereza computer.

Ili tukuze Kiswahili duniani inabidi kwa kila msamiati kuwe na maana moja ya kufanana dunia nzima.

Kenya waligoma kuondoa msamiati Tarakishi waliposhauriwa ili zifanyike tafiti za kutosha kwanza.

Kwenye google Kenya ndiyo wamewahi kuweka Kiswahili badala ya BAKITA na Kiswahili cha google kina dosari nyingi.

Nadhani BAKITA kama ilivyo NIDA zinatakiwa zivunjwe

Mabaraza ya Kiswahili ya eneo la Maziwa Makuu yakikutana ni kulumbana tuu bila muafaka huku kila mmoja akivutia kwake kwa anachokiamini.
 
Mzungu mmoja aliwahi kunikebehi akasema sisi Waafrika kwy Kiswahili tunamuita mtu toka nchi za Magharibi Mzungu, akaniambia ebu sasa ondoa herufi z kwenye neno Mzungu alafu ulisome.

Akajinasibu kwamba Mzungu ni mungu wa weusi ndiyo maana tunawategemea kwa kila kitu hata kibovu, yakiwemo mawazo.

Bakita badilini huu msamiati dhalili kwetu. Hautufai. Kiswahili ni tajiri wa misamiati tutafutieni mwingine.

Vinginevyo tukusanye saini za watu tukaiombe Mahakama iufute toka kwenye matumizi.

Lakini mjuwe kama hamjaandaa msamiati mbadala patakuwa na ombwe endapo Mahakama itachukuwa hatua mapema.

Aidha, sina hakika aliyebuni msamiati huu ni nani hasa na kama hakupewa chochote kitu na hawa miungu mieupe ya Afrika!

Nawasilisha.
Nafikiri huyo mzungu ana wazimu, kwa nini iondolewe z? Ni kabila gani linaloita Mungu mzungu?
Kama ulikebehiwa, uliamua mwenyewe hiyo iwe kebehi.
 
Back
Top Bottom