Baba aua mwanae kisa kuchelewa kutembea, atupwa jela miaka 15

Baba aua mwanae kisa kuchelewa kutembea, atupwa jela miaka 15

Beira Boy

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2016
Posts
23,961
Reaction score
42,166
Aman iwe watumishi wa MUNGU katika KRISTO YESU

Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Geita, imemuhukumu kifungo cha miaka 15 jela, Imani Salehe (23) baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mtoto wake mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu.

Hukumu hiyo imetolewa Aprili 30, 2025 na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Calvin Mhina, baada ya mshtakiwa kukiri kosa la kumuua mtoto wake Monica Imani, bila kukusudia.

Kesi hiyo iliwasilishwa kwa ajili ya kusomewa hoja za awali, lakini Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Kabula Benjamin ameiomba Mahakama kubadilisha hati ya mashitaka kutoka kuua kwa kukusudia na kuwa kuua bila kukusudia, kinyume na Kifungu cha 195 na 198 cha Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

Akiwasilisha maelezo ya kosa, Wakili Kabula amesema tukio hilo lilitokea Septemba 17, 2024 huko Chato, mkoani Geita, Salehe alimuua mtoto wake Monica kwa kumyonga shingoni, kwa madai kwamba mtoto huyo alikuwa amechelewa kutembea, jambo lililomkwaza baba yake.

 
dah jamaa ni chizi fresh,,,ila mtoto nae mzembe kweli mwaka na nusu Bado anajivuta kama nyoka,mm nimetembea nikiwa na miezi 8 tu.
 
Baba alikuwa ana haraka sana ,Kwan alikuwa anataka mtt awahi kutembea kwenda wapii maninaa zakee yy ...na Kwa nn wamempaa adhabu ndogo hvyo kwann asingenyongwa km alivyomnyonga mtt aiseeee....mm mwanangu wakiume katembea akiwa na miaka miwili na hakuwa na shda yyt na ckuwa hata na wsws wwt ule...

Haki nimelia Sanaa 😭
 
Huyo Imani hakua baba alikua bazazi, mwaka na nusu unaua kwa kua mtoto hajaanza kutembea? Kuna watoto wengine wanafika hata miaka miwili ndiyo watembee. Au Amani ali vuta bangi akalewa akawa anamtuma mtoto akimbie kumletea kiberiti baada kuona mtoto Monica haelewi lugha akaona mtoto kamgomea akamnyongelea mbali.
 
Yote hiyo ni umaskini hamna kingine, ukichunguza utakua amani kipato chake hakizidi elfu tano kwa siku na analea familia
 
Aman iwe watumishi wa MUNGU katika KRISTO YESU

Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Geita, imemuhukumu kifungo cha miaka 15 jela, Imani Salehe (23) baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mtoto wake mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu.

Hukumu hiyo imetolewa Aprili 30, 2025 na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Calvin Mhina, baada ya mshtakiwa kukiri kosa la kumuua mtoto wake Monica Imani, bila kukusudia.

Kesi hiyo iliwasilishwa kwa ajili ya kusomewa hoja za awali, lakini Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Kabula Benjamin ameiomba Mahakama kubadilisha hati ya mashitaka kutoka kuua kwa kukusudia na kuwa kuua bila kukusudia, kinyume na Kifungu cha 195 na 198 cha Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

Akiwasilisha maelezo ya kosa, Wakili Kabula amesema tukio hilo lilitokea Septemba 17, 2024 huko Chato, mkoani Geita, Salehe alimuua mtoto wake Monica kwa kumyonga shingoni, kwa madai kwamba mtoto huyo alikuwa amechelewa kutembea, jambo lililomkwaza baba yake.

Hapo usikute kuna udini ...mtoto anaitwa monica na ni mtoto wa salehe🙄🙄🙄🙄
 
Tatizo la Afya ya akili linazidi kuongezeka siku hadi siku.
 
changamoto za afya ya akili ni nyingi sana huko kanda ya ziwa , nadhani pia na ushirikina unausika sana hapo.
 
Back
Top Bottom