Baadhi ya Wanawake Acheni Roho Mbaya

Baadhi ya Wanawake Acheni Roho Mbaya

Payer

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2014
Posts
824
Reaction score
189
Habari ya mchana wana MMU na JF kwa ujumla, mimi sijambo kabisa na imani yangu kwenu ni kuwa hamjambo na kama kuna mgonjwa basi namuombea heri.

Juzi nimekutana na kisa kimoja, mkwe wa mke ni mgonjwa na kwa kuwa kijijini huduma za afya sio bora sana basi ikabidi aletwe jijini kwa matibabu zaidi. Aliyemleta ni mdogo wa jamaa aliye na huyo mwanamke aliyezua kizaazaa.

Mgonjwa alipofikishwa mjini alipelekwa nyumbani kwa kaka mtu ili atibiwe akiwa hapo, cha ajabu mama mwenye nyumba akachukia sana na kusema maneno mengi ya kuwa kwa nini uyo mdogo wako asingeenda naye kwake?

Kiuhalisia kwa mdogo nafasi haitoshi, mmoja wa watoto wa kiume wa mama mlalamikaji alimuhoji mama yake akisema siku nikioa ukaletwa kwangu unaumwa ili utibiwe mke wangu akafanya unayofanya leo, utajisikiaje? Mama akanywea na maisha yakaendelea.

Swali, kwanini wanawake mko hivyo? Hamna utu ndani yenu au ni roho mbaya iliyopitiliza?
 
Please dont generalize!!! Sema kwanini baadhi ya wanawake wako hivyo?? Ni tabia ya mtu tu binafsi anakuwa hapendi wageni wa mume waje kwake,pia hata baadhi ya wanaume wako hvyo hawapendi ndugu wa mke wafike kwake.
 
Please dont generalize!!! Sema kwanini baadhi ya wanawake wako hivyo?? Ni tabia ya mtu tu binafsi anakuwa hapendi wageni wa mume waje kwake,pia hata baadhi ya wanaume wako hvyo hawapendi ndugu wa mke wafike kwake.

Umesomeka vyema. Ni baadhi
 
Nampenda sana mkewangu..ila akileta habari za namna hii....atakuwa amejipatia 'one way/ non-return ticket' to her parents.
 
Hbr ya mchana wana MMU na JF kwa ujumla...
Mimi sijambo kabisa na Imani yangu kwenu ni kuwa hamjambo.
Kama kuna mgonjwa basi namuombea heri.
Juzi nimekutana na kisa kimoja, mkwe wa Mke ni mgonjwa na kwa kuwa kijijini huduma za afya sio bora sana basi ikabidi aletwe jijini kwa matibabu zaidi.
Aliyemleta ni mdogo wa jamaa aliye na huyo mwanamke aliyezua kizaazaa....
Mgonjwa alipofikishwa mjini alipelekwa nyumbani kwa kaka mtu ili atibiwe akiwa hapo, cha ajabu mama mwenye nyumba akachukia sana na kusema maneno mengi ikiwemo " kwa nini uyo mdogo wako asinge enda naye kwake?"
Kiuhalisia kwa mdogo nafasi haitoshi.
Mmoja wa watoto wa kiume wa mama mlalamikaji alimuhoji mama yake akisema "siku nikioa ukaletwa kwangu unaumwa ili utibiwe Mke wangu akafanya unayofanya Leo, utajisikiaje?" Mama akanywea na maisha yakaendelea.
Swali: kwanini wanawake mko ivo? Hamna utu ndani yenu au ni roho mbaya iliyopitiliza??
Huyo mwanamke sio wote,wengine wamelelewa wakaleleka............
 
huyu mume alikuwa wapi aache hadi mama yake mzazi amuulize mka mwana kwann unafanya hivyo

mwanaume atakuwa hana kauli n maisha yao ya ndoa siyo

mwaanamke kuongea hayo maneno hana tabia njema arudi kwao akufundwe
 
Please dont generalize!!! Sema kwanini baadhi ya wanawake wako hivyo?? Ni tabia ya mtu tu binafsi anakuwa hapendi wageni wa mume waje kwake,pia hata baadhi ya wanaume wako hvyo hawapendi ndugu wa mke wafike kwake.

Katika title amesema "baadhi"
 
ICHANA ni hatari sana haya maisha
 
Last edited by a moderator:
Nampenda sana mkewangu..ila akileta habari za namna hii....atakuwa amejipatia 'one way/ non-return ticket' to her parents.

Mnasemaga tu hapa, mnakuwaga mazuzu sana, yani mtu anakunyanyasia ndugu zako, anadharau wazazi wako unamuangalia tu.
Sijui ndo mnatishiwaga papuchi....
 
Last edited by a moderator:
Kim nana, papuchi uko nayo daily inakuogopeahaje? Nadhani meingine anakaa kimya kuepusha ugomvi
 
Last edited by a moderator:
Watu wanajisahau sana mtu akishavuta hewa basi anajiona yeye ndio yeye jamani hujafa hujaumbika.
 
Kim nana, papuchi uko nayo daily inakuogopeahaje? Nadhani meingine anakaa kimya kuepusha ugomvi

Labda mnaogopa kuambiwa "usiku utaona".
Ila wanaume ndo wanalea hizo tabia.
 
Last edited by a moderator:
Habari ya mchana wana MMU na JF kwa ujumla, mimi sijambo kabisa na imani yangu kwenu ni kuwa hamjambo na kama kuna mgonjwa basi namuombea heri.

Juzi nimekutana na kisa kimoja, mkwe wa mke ni mgonjwa na kwa kuwa kijijini huduma za afya sio bora sana basi ikabidi aletwe jijini kwa matibabu zaidi. Aliyemleta ni mdogo wa jamaa aliye na huyo mwanamke aliyezua kizaazaa.

Mgonjwa alipofikishwa mjini alipelekwa nyumbani kwa kaka mtu ili atibiwe akiwa hapo, cha ajabu mama mwenye nyumba akachukia sana na kusema maneno mengi ya kuwa kwa nini uyo mdogo wako asingeenda naye kwake?

Kiuhalisia kwa mdogo nafasi haitoshi, mmoja wa watoto wa kiume wa mama mlalamikaji alimuhoji mama yake akisema siku nikioa ukaletwa kwangu unaumwa ili utibiwe mke wangu akafanya unayofanya leo, utajisikiaje? Mama akanywea na maisha yakaendelea.

Swali, kwanini wanawake mko hivyo? Hamna utu ndani yenu au ni roho mbaya iliyopitiliza?

Kawashtaki ustawi wa jamii,watakusaidia naamini.
 
Back
Top Bottom