Baada ya tarehe 25 October, Tusilaumiane!

Baada ya tarehe 25 October, Tusilaumiane!

fredrickjanga

Member
Joined
Aug 13, 2015
Posts
23
Reaction score
22
Naanza kuwatahadharisha watanzania wote, baada ya uchaguzi mkuu tusilaumiane:

Nimeona wasanii sasa hivi wanajikomba CCM, baada ya uchaguzi ndio watagundua kwamba serikali bado haiwajali, Tusilaumiane!

Naona bado kuna wakinamama wenye shida za kutupwa, bado wanasema CCM ni nzuri, baada ya uchaguzi, ndio wataanza tena kulalamika, Tusilaumiane!

Naona kuna baadhi ya vijana wanapewa vifedha na kujisahau, baada ya uchaguzi, ndio watakumbuka kumbe hawana ajira, Tusilaumiane!

Naona watanzania wengi tumekuwa tukilalamika maisha magumu, baada ya uchaguzi, maisha yatabadilika kutokana na chaguo lako, ukichagua
CCM, Tusilaumiane!

Chagua mabadiliko, vinginevyo, TUSILAUMIANE!!!!
 
Chadema imeshauzwa...

Ni mwendelezo wa kambi ya mgombea wa CCM, asiye na ugomvi na chama bali uchu wa madaraka...

Chadema mwaka huu haina mgombea, isubiri 2025 labda...
 
fredrickjanga
Mabadiliko yapi? Hata CCM wanafanya mabadiliko na walishaanza mapema kabla yetu. Walitupa kule mafisadi wakiongozwa na Lowassa. Wakachagua wenye maadili. Sisi hayo mabadiliko tuliyafanya baadae kwa kuwatupia virago viongozi waadilifu kina Dr Slaa na kuleta mafisadi.

Kwa hiyo unazidi kutuambia tuchague mabadiliko ya style hii au? Viongozi waliopambana na mafisadi miaka nenda rudi tumewatupa na kukumbatia wachafu na makapi. Haya ndio unayoyataka?
 
Last edited by a moderator:
Mabadiliko kwa kupitia chama hiki alichokinunua Lowasa? CHADEMA au kipi. Manake tunaambiwa mitandaoni jamaa alitoa hela ndefu.
Hii hii Saccos au?

Usidharau wananchi kiasi hicho. Umebugi meeeen!
 
Umeanadika maneno ya busara na hekima sana. Mimi nlishawambia ndugu zangu vijijini nkigundua unaishabikia ccm na kuipigia kura. Usinililie shida. Mfano lowasa kashasema atafanya awezalo elimu iwe bure mpaka chuo na matibabu apunguze gharama. Nimewambia ukichagua ccm na kilaza magufuli. Mtu asiniombe hela ya ada au michango ya madawati.
 
kwa utaratibu huu huu tusije shikana uchawi, eti kwa nini tulikuwa na ubadilishaji gia angani.
 
Na pia UKAWA na uroho wao wameamua kujitoa akili na kuwaalika mafisadi yaliyokubuhu eti ndio yapeperushe bendera ya urais. Tusianze kulaumiana eti tumeibiwa kura, oh sijui tumefungwa goli la mkono na maccm.
 
fredrickjanga
Mabadiliko yapi? Hata CCM wanafanya mabadiliko na walishaanza mapema kabla yetu. Walitupa kule mafisadi wakiongozwa na Lowassa. Wakachagua wenye maadili. Sisi hayo mabadiliko tuliyafanya baadae kwa kuwatupia virago viongozi waadilifu kina Dr Slaa na kuleta mafisadi.

Kwa hiyo unazidi kutuambia tuchague mabadiliko ya style hii au? Viongozi waliopambana na mafisadi miaka nenda rudi tumewatupa na kukumbatia wachafu na makapi. Haya ndio unayoyataka?
Mkuu ainisha ushiriki wa mzee Slaa na kwenye ujio wa Lowasa.
 
Last edited by a moderator:
Naanza kuwatahadharisha watanzania wote, baada ya uchaguzi mkuu tusilaumiane:

Nimeona wasanii sasa hivi wanajikomba CCM, baada ya uchaguzi ndio watagundua kwamba serikali bado haiwajali, Tusilaumiane!

Naona bado kuna wakinamama wenye shida za kutupwa, bado wanasema CCM ni nzuri, baada ya uchaguzi, ndio wataanza tena kulalamika, Tusilaumiane!

Naona kuna baadhi ya vijana wanapewa vifedha na kujisahau, baada ya uchaguzi, ndio watakumbuka kumbe hawana ajira, Tusilaumiane!

Naona watanzania wengi tumekuwa tukilalamika maisha magumu, baada ya uchaguzi, maisha yatabadilika kutokana na chaguo lako, ukichagua
CCM, Tusilaumiane!

Chagua mabadiliko, vinginevyo, TUSILAUMIANE!!!!

Hao mabadiliko ndio wataleta nini?
KARNE YA 21 HAMNA WA KUMDANGANYA, WE ACHA TU WATU WAPIME MBAYA YUPI ANA KANAFUUPO!
 
Muomba kura kanisani atawadanganya nyie tu wafata mkumbo ila sio watu wanao-reason vizuri. Katoka CCM karukia CDM, its still the same person, hata kama akiwa nyuma ya chama still anahold power kubwa tu, ona burundi jamaa alivogoma kutoka hata chama chake kilishindwa kumwambia chochote, that's the power of the president. You can't give that much power kwa mtu asiyejitambua
 
fredrickjanga
Mabadiliko yapi? Hata CCM wanafanya mabadiliko na walishaanza mapema kabla yetu. Walitupa kule mafisadi wakiongozwa na Lowassa. Wakachagua wenye maadili. Sisi hayo mabadiliko tuliyafanya baadae kwa kuwatupia virago viongozi waadilifu kina Dr Slaa na kuleta mafisadi.

Kwa hiyo unazidi kutuambia tuchague mabadiliko ya style hii au? Viongozi waliopambana na mafisadi miaka nenda rudi tumewatupa na kukumbatia wachafu na makapi. Haya ndio unayoyataka?

Miongoni mwa watu wenye utapia mlo wa kufikir na wewe umo? CCM imetupa mafisadi tangu lini? Juz tu hapa hata mwaka haujafika mafisadi wa ESCROW wanarandaranda tu mitaani, ufisadi wa bn300/-na usheee, eti leo unakuja na hadaa za kwenue khanga CCM imetupa mafisadi, are serious? Watu wamenunua mabehewa fake, Boat fake, watu wamelisababishia hasara Taifa, kuna issue ya radar, EPA,IPTL,Nyumba kuuzwa katka ile ijulikanayo kama political Enterpreneurship na kadhia kazaa za kifisadi. Ngoja uchaguz uishe kama hatutasikia ufisadi mwingine wa CCM ili kugharimia kampeni.

Mchangiaj Babel ni mpotoshaji sana. Mafisadi wote bado wako CCM.
 
Last edited by a moderator:
Hao wasanii kila siku wanaililia serikali imeshindwa kusimamia kazi zao....
Kweli tusilaumiane
 
Mimi mmoja wa wanaoichukia ccm kuzidi chochote duniani, lakini kubadili ccm kwa ajili ya lowassa, hilo sikuabaliani hata kiama, bora ccm warudi tu,
Wapuuzi kina mbowe wametuuza mwaka huu tungeshinda kwa nguvu zetu bila kuazima hiyo mizoga ya ccm isiyo na usafi wala uadilifu, eti Leo ndio imekuwa tumaini letu, ujinga kabisa, mbwa waliotukamua miaka mbwa waliotutafuna miaka leo ndio walinzi wa mageti yetu, upumbavu kabisa
 
Naona huu umevamiwa na watu wa Lumumba. Unanuka kinyesi
 
Mimi kwenye familia yangu ni mwendo wa mabadiliko tu hadi raha.
Ila kuna watu nawaangalia tu,ngoja October ipite.
 
Naanza kuwatahadharisha watanzania wote, baada ya uchaguzi mkuu tusilaumiane:

Nimeona wasanii sasa hivi wanajikomba CCM, baada ya uchaguzi ndio watagundua kwamba serikali bado haiwajali, Tusilaumiane!

Naona bado kuna wakinamama wenye shida za kutupwa, bado wanasema CCM ni nzuri, baada ya uchaguzi, ndio wataanza tena kulalamika, Tusilaumiane!

Naona kuna baadhi ya vijana wanapewa vifedha na kujisahau, baada ya uchaguzi, ndio watakumbuka kumbe hawana ajira, Tusilaumiane!

Naona watanzania wengi tumekuwa tukilalamika maisha magumu, baada ya uchaguzi, maisha yatabadilika kutokana na chaguo lako, ukichagua
CCM, Tusilaumiane!

Chagua mabadiliko, vinginevyo, TUSILAUMIANE!!!!
Tusichague vigeugeu. Mtu alikuwa kiongozi w toka uhuru.Leo anaambiwa uongozi basi anatukana watu.Hizi ni tabia za vigeugeu na si mabadiliko ya tija
 
Back
Top Bottom