SAGAI GALGANO
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 43,707
- 60,766
Nitafute nikuliwazeKama kichwa cha habari kinavyosema hapo juu.
Huyu kaka tumekuwa na mahusiano kwa zaidi ya mwaka na miezi 8 kwa jina lake ni Frank, kwa wale mliofuatilia nyuzi zangu za nyuma Frank ndiyo huyo mchaga ambae hayuko romantic. Kama nilivyowaambia mwanzo hatujawahi kukulana mpaka mwezi uliyopita ndiyo tulifanikiwa kukulana.
Nikiwa nimetimiza miaka 25 mwezi uliopita niliona siyo mbaya kumtunuku ninayemwita mpenzi wangu Frank. Hata yeye alifurahi maana ndiyo mwanaume wa kwanza kunikula (kanibikiri), akaniahidi ahadi kedekede. Basi ndiyo hivyo kaniingiza kwenye ulimwengu wa mapenzi.
Sasa ndugu zangu mimi ndiyo bikira yangu ishaenda na maji na mwanaume kanichunia. Baada ya tendo alionesha kunijali kama wiki mbili hivi baada ya hapo akasafiri kwenda mahali fulani ndiyo mambo yakarudi kama mwanzo, hanitafuti mpaka nimuanze. Mara ya mwisho nilimtumia sms kumuuliza kama amesharudi akaninyamazia hakunijibu
Tangu hapo sikumtafuta, baada ya kama wiki moja akanitumia sms kunijulia hali nami sikumjibu na wala sikuifungua mpaka hivi leo ninavyoongea ni wiki ya 3 sijamjibu wala kumsemesha. Nilikuwa na view status zake naye ana view zangu ila baadaye nikaona kimya, sioni status zake wala sioni akiview zangu.
Leo sasa nikaona niifungue sms yake niangalie dp nakutana na kivuli, ikabidi nimuulize sister wangu kwamba anaona status za Frank akajibu ndiyo, nikamwambia na dp, aka screenshot akanitumia nikajua tu hapa nimeblockiwa!
Jamani kusema kweli pamoja na kukaliana kimya sikuwai kuumia kama leo baada ya kujua kumbe kaniblock. Ina maana huyu jamaa kaamua anibikiri afu anibwage? Nyie kumbe huyu jamaa nimempenda ukweli nilifikiri masikhara, ila ndio hivyo tena.
Sijutii kutolewa bikira, kinachooniuma ni kujua kwamba hanipendi.
Ni hayo tu naombeni mniliwaze.