Ni muendelezo wa mikakati iliyokuwepo tokea awali, baada ya Sudan ya kusini ilikuwa wimbi la kugawanywa liilekee Misri (lilisimamishwa na mapinduzi ya kumngoa Mubaraka) sambamba na Mali,Niger (sina uhakika kuhusu Mauritania ilikuwa ingiliwe vipi).Ukiangalia hilo jimbo/eneo/taifa lililojitangazia uhuru, ni kubwa zaidi kuliko Mali. Kumbe juhudi zao za kudai uhuru hazikuanza leo na hata hao wanajeshi waliopindua, walifanya hivyo kwa sababu raisi waliempindua walimhisi ana "moyo laini" kwa "waasi", na ndio walitaka wao wawanyamazishe. Matokea yake ni hayo.
Tusubiri tuone.
Kutoka Euphrates una Iraq iliyogawanyika, kuanzia Nile una Sudan (Misri) zinazogawanyika, changanya na zako unapata jibu Mkuu!