ecolizer baba
Member
- Sep 29, 2010
- 88
- 310
Azam Tv hiki mnachofanya hakivumiliki.
Wananchi tulianza kuwaamini sana kwa huduma zenu za matangazo ya televisheni. Taarifa zenu za habari na hasa Campaigns zilikuwa balanced kwa vyama vyote vikubwa vya siasa na hasa CHADEMA/UKAWA kwa upande mmoja na CCM kwa upande mwingine zilikuwa balanced bila bias yoyote.
Lakini kwa takribani wiki mbili zilizopita tunaona tofauti kubwa sana na hasa kwa upande wa mgombea urais wa,CHADEMA/UKAWA Mh. Edward Lowassa. Taarifa za mikutano yake hamzioneshi vizuri siku hizi na hata kama mtaonesha huwa camera zenu zinawakwepa umati wa wahudhuriaje ambao huwa ni wengi na badala yake mnaishia kuonesha high table tu.
Na kwa siku ya leo ndio mmetia fora kabisa. Licha ya kuacha kuonyesha mikutano ya Lowassa huko kanda ya ziwa lakini pia mmetunyima kusikia alichosema Mh. Freeman Aikael Mbowe juu ya Msiba wa M/kiti mwenza wa UKAWA Dr. Emmanuel Makaidi. Wakati mtangazaji anatangaza hiyo habari sauti ilikuwa inatoka lakini Mh. Mbowe alipoonyeshwa akitoa tamko la UKAWA kuhusu kifo cha Mh. Makaidi sauti ikakata. Ilipoisha habari ya Mbowe sauti ikarudi. Kwa kweli wana-UKAWA wameumia sana kwa hiki mlichotufanyia leo. Na hata hamkuomba radhi.!!!
Am sure Ndg. Tido Mhando ni mtu ambaye ni smart sana na huenda hajui hiki kinachotokea. Huenda anahujumiwa na mafundi mitambo na watangazaji wa Azam.
Azam tv kumbukeni kuwa mna wateja toka vyama vyote na wote wanalipa gharama sawa kila mwezi. Hivyo acheni kutakatisha tamaa wateja wenu. Kama imekuwa ikitokea kwa,bahati mbaya basi ni busara muwe mnaomba radhi.
MODS NAOMBENI MSIUFUTE UZI HUU KWANI TUNA HAKI YA KUONYESHA MASIKITIKO YETU KWA JF IS WHERE WE DARE TO TALK OPENLY.
Wananchi tulianza kuwaamini sana kwa huduma zenu za matangazo ya televisheni. Taarifa zenu za habari na hasa Campaigns zilikuwa balanced kwa vyama vyote vikubwa vya siasa na hasa CHADEMA/UKAWA kwa upande mmoja na CCM kwa upande mwingine zilikuwa balanced bila bias yoyote.
Lakini kwa takribani wiki mbili zilizopita tunaona tofauti kubwa sana na hasa kwa upande wa mgombea urais wa,CHADEMA/UKAWA Mh. Edward Lowassa. Taarifa za mikutano yake hamzioneshi vizuri siku hizi na hata kama mtaonesha huwa camera zenu zinawakwepa umati wa wahudhuriaje ambao huwa ni wengi na badala yake mnaishia kuonesha high table tu.
Na kwa siku ya leo ndio mmetia fora kabisa. Licha ya kuacha kuonyesha mikutano ya Lowassa huko kanda ya ziwa lakini pia mmetunyima kusikia alichosema Mh. Freeman Aikael Mbowe juu ya Msiba wa M/kiti mwenza wa UKAWA Dr. Emmanuel Makaidi. Wakati mtangazaji anatangaza hiyo habari sauti ilikuwa inatoka lakini Mh. Mbowe alipoonyeshwa akitoa tamko la UKAWA kuhusu kifo cha Mh. Makaidi sauti ikakata. Ilipoisha habari ya Mbowe sauti ikarudi. Kwa kweli wana-UKAWA wameumia sana kwa hiki mlichotufanyia leo. Na hata hamkuomba radhi.!!!
Am sure Ndg. Tido Mhando ni mtu ambaye ni smart sana na huenda hajui hiki kinachotokea. Huenda anahujumiwa na mafundi mitambo na watangazaji wa Azam.
Azam tv kumbukeni kuwa mna wateja toka vyama vyote na wote wanalipa gharama sawa kila mwezi. Hivyo acheni kutakatisha tamaa wateja wenu. Kama imekuwa ikitokea kwa,bahati mbaya basi ni busara muwe mnaomba radhi.
MODS NAOMBENI MSIUFUTE UZI HUU KWANI TUNA HAKI YA KUONYESHA MASIKITIKO YETU KWA JF IS WHERE WE DARE TO TALK OPENLY.