Azam Media ajirini, CEO kutoka nje ya nchi

Azam Media ajirini, CEO kutoka nje ya nchi

fimboyaukwaju

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2020
Posts
5,608
Reaction score
7,167
Matangazo yenu yana ubora mdogo sana, ukilinganisha na uwekezaji mkubwa sana mlioufanya.

Matatizo makubwa ni haya:

1.Sauti ni tatizo kubwa sana. Kila taarifa ya habari ni lazima ina shida ya sauti

2.Kuandika maandishi yanayoambana na habari hapo ndio kituko cha ajabu

3.Mpangilio wa watangazaji wanavyo kaa ama kusimama wanapotangaza vipindi kadhaa ni tatizo.

4.Uvaaji wa nguo wa watangazaji wenu ni kituko.

Hayo ni matatizo ya miaka nenda miaka rudi yapo tu. Njia pekee ni kuleta mtendaji mkuu kutoka nje ya nchi

Soma Pia: Azam TV kwenye application sio poa
 
Nje ya mada/mada mchepuko, nimechanganya media, dishi ni la Star Times, king'amuzi ni cha Azam, chaneli za star times zinaonekana kwenye screen ya tv na zinazofunguka ni tatu TBC1, safari channel na st.guide. Je nikilipia Star times chaneli zao nitakuwa nazifungua sambamba na chaneli za azam kwenye screen moja? Nadhani hii itanipunguzia kuwa na madishi mawili/matatu na tv mbili au tatu ndani kwangu kwa kuwa media zitakuwa zinasomana kwenye tv moja bila HDM2/ HDM3
 
Halafu azam Media mniambie hapa vile ving'amuzi vyenu vya antenna vina shida gani? Niko Mkoani huku mbali na nyumbani, nikasema ninunue ili niangalie ligi ya Bongo!

Aisee mpaka najuta. Kila baada ya dakika chache, picha zina staki! Kwa upuuzi wenu huu ni bora nikaangalie tu mpira kwenye vibanda umiza. Siji kulipia tena.
 
Back
Top Bottom