franckkimm
JF-Expert Member
- Aug 25, 2016
- 442
- 860
- Thread starter
- #21
Hata kipindi kakolanya yupo Simba, akipewa nafasi ya kucheza Badoo mashabiki wanalalamika, saivi yupo Singida ndio wanaona Bonge la kipaNdio ninesema mna ujuaji hali yakuwa hata mpira hamujui hivi yale magoli unaweza kumlaumu kipa kwa lipi?
Tuanze na goli alilo fungwa siku ya mechi ya power Dynamos huko zambia, kwanza mshambulia aliye funga hilo goli movement yake aliyo kuwa anaifanya akiwa na mpira haikuonesha dalili yeyote iwapo yule jamaa alikuwa anajiandaa kushut, kwa sababa mbele yake kulikuwa na mabeki zaidi 3 wa Simba walikuwa mbele yake na pia alikuwa mbali sana na goli .Inamaana alifanya maamuzi ya kushut baada ya kuona mabeki wa simba walio kuwa wamenzunguka wanamkaba kwa macho ,kitu ambacho kipa hakukitegemea maana aliamini mabeki walikuwa na uwezo wa kumbrock yule mfungaji wa goli. Alafu kingine lile shuti lilikuwa kali japo lilikuja liambaa ambaa kwa chini alafu ule mpira ulikuwa unandunda ndunda kwa chini , hilo goli badala ya kumlaumu kipa, una takiwa kuwalaumu mabeki kwa kushindwa kutimiza majukumu yao na umsifu mfungaji wa lile goli maana alifanya maamuzi magumu na katika wakati usio tegemewa.
Goli alilo fungwa hapa dar sasa hilo ndo kabisa haitaji hata chembe ya lawama maana mchezaji aliye funga lile goli alitoka na mpira karibia na katikati ya uwanja akamove nao kwa zaidi ya sekunde 45 wachezaji wa simba wanamuangalia tu akasoge mpaka nje kidogo ya box wachezaji wa simba wanamuanalia tu, akasegea mpaka katikati ya mabeki 4 wa simba akashot sasa hapo kipa aunamlaumu kwa lipi zaidi ya kuleta ujuaji usio na maana?
Nyinyi ndo mnamlaumu kipa ya taifa staz kwa kufungwa bao la mbali na Hakim Zieych hali ya kuwa magoli ya aina hiyo amekuwa akiyafunga kwenye mechi nyingi tena dhidi ya magoli kipa bora duniani.
Ila huyu kocha si kasema hata angalia jinaa Bali uwezo wa mchezaji tusubiri tuone.
Tatizo hii Simba yetu changamoto kubwa baadhi ya wachezaji wao ni wakubwa kuliko timu, hayo Mambo yashapitwa na wakati, huchezi vizuri benchi mwingine apatiwe nafasi