DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Waziri wa Maji na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Pangani Mkoani Tanga Mhe. Jumaa Aweso amesema dhamira ya Dkt . Samia Suluhu Hassan ya kutoa maji ziwa Viktoria ili kuhudumia wananchi wa Mkoa wa Shinyanga yalikuwa maamuzi sahihi na ya kupongezwa kutokana na namna ambavyo mradi huo wa maji umekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi.
Waziri Aweso akizungumza na maelfu ya wananchi wa Maganzo, Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga leo Jumamosi Oktoba 11, 2025 wakati wa mkutano wa kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema mradi huo umesaidia Mji wa Maganzo kupata maji kwa asilimia 80 kutoka Ziwa Viktoria huku eneo la Vijijini wakipata maji kwa asilimia 62.5, tofauti na miaka minne nyumba ambapo upatikanaji wa maji ulikuwa chini ya asilimia 40.
"Moja ya sehemu ambapo palikuwa na ukame wa maji ni hapa Kishapu. Hali ya upatikanaji wa maji ilikuwa chini ya asilimia 40 na changamoto ya Kishapu hata ukichimba visima maji haupati. Dhamira ya kuyatoa maji Ziwa Viktoria na kuyaleta Shinyanga yalikuwa maamuzi sahihi. Tumeifanya kazi na Kishapu sasa wanapata maji kwa zaidi ya asilimia 62 Vijijini na Mjini asilimia 80" Amesema Waziri Aweso.
Katika hatua nyingine Mwanasiasa huyo amebainisha kuwa zaidi ya Shilingi Bilioni 27 zitatumika kwaajili ya kuhudumia maeneo ambayo bado hayajafikiwa na huduma ya maji kwenye Vijiji vya Bubiki, Mondo na Sekebugolo, akisema Dkt. Samia ndiyo faraja yao na atahakikisha maji yanawafikia wananchi hao punde baada ya kuwa amepewa ridhaa ya kuunda serikali kupitia uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.
https://www.instagram.com/p/DPqkh5CAq00/comments/
Waziri Aweso akizungumza na maelfu ya wananchi wa Maganzo, Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga leo Jumamosi Oktoba 11, 2025 wakati wa mkutano wa kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema mradi huo umesaidia Mji wa Maganzo kupata maji kwa asilimia 80 kutoka Ziwa Viktoria huku eneo la Vijijini wakipata maji kwa asilimia 62.5, tofauti na miaka minne nyumba ambapo upatikanaji wa maji ulikuwa chini ya asilimia 40.
"Moja ya sehemu ambapo palikuwa na ukame wa maji ni hapa Kishapu. Hali ya upatikanaji wa maji ilikuwa chini ya asilimia 40 na changamoto ya Kishapu hata ukichimba visima maji haupati. Dhamira ya kuyatoa maji Ziwa Viktoria na kuyaleta Shinyanga yalikuwa maamuzi sahihi. Tumeifanya kazi na Kishapu sasa wanapata maji kwa zaidi ya asilimia 62 Vijijini na Mjini asilimia 80" Amesema Waziri Aweso.
Katika hatua nyingine Mwanasiasa huyo amebainisha kuwa zaidi ya Shilingi Bilioni 27 zitatumika kwaajili ya kuhudumia maeneo ambayo bado hayajafikiwa na huduma ya maji kwenye Vijiji vya Bubiki, Mondo na Sekebugolo, akisema Dkt. Samia ndiyo faraja yao na atahakikisha maji yanawafikia wananchi hao punde baada ya kuwa amepewa ridhaa ya kuunda serikali kupitia uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.
https://www.instagram.com/p/DPqkh5CAq00/comments/