Lakasa chika7
JF-Expert Member
- Jan 7, 2017
- 510
- 1,337
inakre sana aisee. watu wapo kivyam vyama sana. nahisi kuna vikundi vinapewa pesa ili waje wapigie debe vyama vyaoJf ushabiki umezidi uki ikosoa UKAWA bas wewe CCM , uki ikosoa CCM bas wewe UKAWA, tumekuwa sio great thinkers tumekuwa grat Partisans. Inakera sana
Jana niliandika mada kuhusu kushake kwa diplomasia ya Tanzania kimataifa. Ulikuwa ni ushauri tu kwa viongozi wetu ambao kimsingi siyo watawala kwakuwa tume/wamechaguliwa.
nilipata kebehi KUTOKA kwa vijana ccm..Mara wazee wa kata tatu, baada ya kipigo cha kata 19,wengine wakaniita nyumbu sijui., mwingne akaniambia mshauri mbowe achana na Magufuli wetu. Wengine eti mkalipie kodi jengo lenu.
Wiki moja imepita niliwahi pia kuandika ukimya wa viongozi wa chadema/ juu ya Ben saanane pamoja na shutuma za kubenea. Aisee, napo nilioga shutuma nyingi sambamba na kejeli kutoka kwa chadema. Mara Lumumba huyu, Mara propanga wa Lumumba, Mara buku kazini. Wengine wakaniita kilaza wa Lumumba. Mara bendela fata upepo.
Jukwaa hili tunaliharibu sana. Binafsi nilijiunga 2010 siyo kwa akaunti hii kipind kile Jamii forum kulikuwa MTU akiibua hoja anajibiwa kwa hoja. But Leo tunajiabisha sana na kama siyo wasomi vile. Let's discuss issues- pinga kwa hoja, kubali kwa hoja.
Tukumbuke sisi ndo vijana wa Leo..wengine tuna watoto/ wengine tutapata pia. Tunabishana na kusuguana kwa ushabiki. Kizazi chetu kitakuwaje. Tuwe vibrant.
Ushabiki wa kisiasa usitutoe kwenye agenda ya maendeleo. Wananchi na wanajamii forum tunataka maendeleo, siasa safi na utu wa mtanzania uheshimiwe.Forum ya kisiasa isiwe km kijiwe cha celebrity forum!
Tukiruhusu kutumika na wanasiasa tutaipoteza Tanzania. Tuwe vibrant na mawazo huru. Anakutumia anakupa shilingi ngapi na mwambie akupe na life insurance basi.
Shukrani.
aisee umeandika ukweli mtupu. asante sanaI real I appreciate your thread.
Hilo ndilo tatizo tunalokutana nalo hapa JF maana watu wanashindwa kujadili mada wanajadili watu au kutoa ligha chafu bila sababu, ila nimegundua tatizo siyo ushabiki tu ila background matters a lot. Pia kuna watu wamekubali kuingiziwa chuki binafsi zisizo kuwa na tija...kuna mtu kafundishwa kumchukia Lowassa na mwengine kafundishwa kumchukia Magufuli kwa hiyo determinations zao zimekuwa finyu sana kujadili mambo makubwa yanayohusu nchi. We are heading a very wrong direction as a nation
we nawe uchama huo
safi sana mzeeWatu wanasahau kwamba Tanzania ni muhimu kuliko ma vyama ......
Vyama vilikuwepo vingi vimepita toka enzi Tanzania haijapata Uhuru kama ASP,TANU na vingine .....
Lakini Tanzania imebaki tena ikiwa ndani moja..............
Tubishane kwa hoja za kukosoa kwa maendeleo au tutaniane kwa kwenye jukwaa usika sio kuleta unafiki kwenye mambo ya msingi..........
Kuna mambo tunatakiwa tuungane kama nchi na kuna mambo inatakiwa tubishabe kwa kujenga hoja kama nchi...............
ushauri mzuri sana Junior Zito..Nasikia kaka yupo nje ya nchi kweli haya..joking?Shida tunaingia na ID feki ndo maana watu walo huru kutukana wanavyotaka ila tungekuwa tunaingia na real identities i hope watu wangekuwa na staha ili kulinda heshima na credibility zao kwenye jamii.
Afu pia mada nyingi ni za kichama humu ndio zinaharibu hivi tungeweka mada za kisiasa lakini zina direct impact kwa maendeleo kma elimu bure ,uongozi,miswada ya bungeni kule,uchumi n.k i guess watu wangeweka uchama pembeni ili warushe madini ya kisomi shida inakuja unapoleta story ya mbowe au magufuli hapo lazma watu wagawanyike maana inagusa interest za vyama.
SOLUTION: Tulete mada za MASUALA sio vyama au political personalities
tunatumika kabsa,,alafu ni kote, ccm wanawatumia watu, chadema nao vilevileSafi hizi ndo issue za kujadili. Unajua huwa nafika mahala sielewi sijui nani kawaloga.. mtu anashabikia siasa kama anavyoshabikia soccer.. bila kujua analeta ushabiki kwenye maisha.. siasa ina nguvu, siasa ni maisha. inauwezo wa kumpa nguvu aliyeishia la tatu kutunga sheria na ikamunyima mwenye degree hata mbili.. tusilete jokes na maisha.. hao tunaowashabikia wengi wao wanatutumia kama ngazi za kupandia..