Athari za ahadi za majukwaani

Kali _D

Senior Member
Feb 10, 2019
145
132
Nikiwa kama mwananchi mzalendo, nimetafakari sana athari tutakazozipata kutokana na ahadi zinazotolewa katika majukwaa ya siasa hasa katika kipindi hichi cha kampeni.

Baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakiahidi mambo ambayo ukiyaangalia kwa undani hayawezi kutekelezeka hata kidogo.

Tumemsikia Mgombea wa Urais Zanziba kwa tiketi ya ACT Wazalendo Maalim Seif Hamad akitoa ahadi kuwa atapandisha kima cha chini cha mishahara hadi kufikia silingi Laki 5 za kitanzania. Ikumbukwe kwamba kima cha chini cha mishahara kinapandishwa Serikalini kinaenda sambamba na kile katika sekta binafsi.

Je, Ni sekta binafsi ngapi zina uwezo wa kupandisha kwa kiasi hicho? Je, Bajeti ya serikali ya Zanziba inaakisi upandishwaji wa mishahara kwa kiwango hicho? Je, vyanzo gani vya mapato vitatumika kama sio kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa.

Pia, baadhi ya wagombea wamekuwa wakitumia majukwaa kuubeza Muungano wetu wa Tanganyika na Zanziba ambapo wamekuwa wakiuelezea kwa lengo la kupotosha ukweli na uhalisia wake.

Wazanzibar na Watanzania bara kwa ujumla tusiingie katika mtego huo kwani kwa kushirikiana kwetu tumepata Nchi ya neema Tanzania, na chokochoko zote zinazoendelea zina lengo la kuhakikisha wanawaingiza wananchi kwenye machafuko.​
 
Kweli ahadi za uongo kama za CCM hazitakiwi kabisa.
1. Milioni 50 kila kijiji ipo wapi?
2. Laptop kwa kila Mwalimu zipo wapi?
3. Tanzania ya viwanda ipo wapi?

i. Hapa Dodoma tuliahidiwa
Ujenzi wa uwanja wa michezo wa kisasa na kimataifa jiwe na Mfalme wa Morroco Chali
ii. Ujenzi wa uwanja wa ndege Msalato chali.
iii. Ujenzi wa Hospital ya uhuru kutoka fedha za uhuru day 2017 hadi leo chaliiii.
Iv. Ujenzi wa Barabara ya Mduara Ring road CHALI.

CCM ni waongo sana watanzania tusifanye makosa 28/October
 
Ni ngumu sana kupandisha mishahara wakati mfumuko wa bei haupo undercontrol. Ukipandisha mshahara na bei zina panda exponentially kufidia gepu la ongezeko.

So cha msingi ni kutazamia mbinu za kushusha mfumuko wa bei. Ukiweza hilo automatically mshahara utatosha. Hata kwa mshahara wa 300,000 na nusu watu watafanya maisha issue ni mfumuko wa bei baaaaasi.

Mataifa yetu ya dunia ya tatu bado yanapambana na hili tatizo na linawashinda kwasababu ya kukosa mipango na mikakati ya kiuchumi ya kupambana na soko la uhitaji wa bidhaa na huduma mbali mbali ambazo nyingi hutokea nje.

Unapokuwa na taifa hambalo wanainchi wake 80% ya mahitaji yao hutokea nje ya inchi then tarajia mfumuko mkubwa wa bei kwasababu pesa yote inakwenda nje na wao humu ndani hawana soko linalotegemea bidhaa tokea ndani.
 
Ni kama ilivyoyeyuka ile ahadi ya mil. 50 kila kijiji. Yaani Meko atatafunwa na dhambi hii hadi atakapoingia kaburini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom