Askofu Dr Benson Bagonza: Hatuna duka linalouza hekima ukiwa mwizi ujifunze na kukimbia

You better write in Swahili coz you're so silly in English!!
Kilikuja na pepo za kaskazi na kusi.
Mavy yamenibana nisamehe naachia na kuporomosha bonge la ushuz mbrrrrrrrrr mbrrrrrr mbrrrr.

Na mbusi hapa kaning'ata nalia meheeee meheee mheee

Hachomoki mutu hapa maamae!
 
Kinachonikera wakati twiga na dhahabu zilipokuwa zinaondoka mbona mlikuwa hamlalami, vikapu vimepungua mafungu ya kumi. Tumieni hizo Chache ndo za halali
 
Tangu sadaka zipungue makanisani!madili ya msamaha kwa mgongo wa kanisa!biashara ya madawa ya kulevya kuyumba. .....wanaweweseka kila siku!mwishowe watajiita sir God! JPM shikilia hapohapo!usiachie baba!hapo hapo!
Jamani Kwani Askofu kasema anamsema JPM? Vije mwajishuku?
Hehehehee
 
Hatuna duka linalouza hekima. Hakuna mganga wa kienyeji toka Sumbawanga anayeweza kuzindika hekima. Hatuna daktari wa kufanya operesheni kuingiza hekima kichwani. Hakuna muujiza wa maombezi kuingiza hekima vinywani na kwenye bongo zetu.

Uzoefu (experience), haina mbadala. Twazingatia:

-Ukiwa mwongo, usiwe msahaulifu.

- Ukijifunza wizi, jifunze na kukimbia.

- Ukikosa uaminifu, jifunze uangalifu.

- Usibadili aibu kuwa hasira.

-Asojua ubaya wa makalio, huyageuza mto wa kulalia.

- Waweza kuwadharau siafu, lakini huwezi kuwakalia.

- Nyumba yenye njaa, haikosi kelele.

Mungu wetu ni msingi wa demokrasia. Aliumba wenye nguvu na wanyonge, wajinga na werevu, watawala na watawaliwa. Uhuru wa mihimili ni utashi wa muumba ili amani iwepo. Mungu akikupa nguvu anakunyima hekima ili ushauriwe; akikuumba mfupi, anakupa akili za kutumia warefu wakuchumie maembe. Dunia ya wafupi tu ni taabu. Ya warefu tu ni balaa. Ya wababe tu, mnyonge ndiye kiongozi.

Maisha yakiwa magumu, wote tunageuka wana falsafa. Tunda letu limepotea, humu ndani hapakaliki. Aliyekula na aliyekosa, wote wanalia.

Tuwahi nyumbani, ofisini hapakaliki na mitaani mafuriko.
Haya maneno yamejaa mwanga tena yamaana sana
 
Kinachonikera wakati twiga na dhahabu zilipokuwa zinaondoka mbona mlikuwa hamlalami, vikapu vimepungua mafungu ya kumi. Tumieni hizo Chache ndo za halali
Wewe ndio ulikaa kimya!
Wale wale walioiba twiga ndio hao hao wanaosema kuna mwizi.

Imekua kama vibaka wanaomkwapulia mtu simu yake halafu wanapoteza watu maboya kwa kupiga kelele za mwizi kwa mpita njia au kumnyooshea lidole yule yule waliye mwibia.Lengo ni kuwachanganya watu huku wao wakitokomea zao.

Jiulize tu wakati twiga wanaibiwa ni wakina nani walikua madarakani yaani watawala kuanzia maDC ,maRC ,mawaziri n.k.
Jibu ni rahisi ni hao hao na wakosoaji waliposema waliitwa wenye chuki na wapotoshaji. Walipewa majibu mepesi mepesi kama ilivyo desturi.

Kuikosoa serikali yoyote sio jambo rahisi na la kukurupuka.
Kama watu wanavyopotosha.
Askofu kusimama na kutoa maoni juu ya watawala sio jambo jepesi.
Ni rahisi kujipendekeza kwa watawala na kupata faida kuliko kuwakosoa na kupata hasara.
 
Na wala siyo ajabu kusikia ingawaje halipendwi kusemwa waziwazi linavungwavungwa tu kuwa katika machafuko na hatimaye mauaji nchini Rwanda, viongozi wa IMANI walishiriki pakubwa kuleta chokochoko kama hivi.
 
Back
Top Bottom