Askari wa usalama barabarani Kimara Bucha

Askari wa usalama barabarani Kimara Bucha

Joined
Jun 13, 2015
Posts
8
Reaction score
22
Habari wandugu,

Napenda kuwapa tahadhari juu ya kikundi cha askari wa usalama barabarani wanaopenda kukaa maeneo ya Kimara Kona ama Kimara Bucha. Askari hawa ni wahuni na wanabambikia watu kesi kila mara, na muda mwingine ukibishana nao wanakukariri gari yako na kuchukua number ya leseni yako wanakua wanakuandikia faini ilihali huna kosa wala hujakubaliana na kosa tajwa kama sheria inavyoelekeza.
 
Mhh kile kikundi cha boko haramu pale Kimara buchasiyo cha kispoti, ukiwa na gari na ukaamua kupita pale lazima wakule kichwa!! nikisubiri mwendo kasi pale bandani huwa nawachora tu wanavyowafyeka.
 
Wale Askari ni shidaaa miaka 2 nyuma nlipambana nao karibia kila siku nikiwa na misele ya town . Hawanaga huruma wale.
 
Wapigeni picha za kutosha muwaweke hapa ili tuwajadili, kuna wengine hawajapata shida kitaa wametoka kwa wazazi, wakapitia kwa mashemeji, wakawa ma askari. Inabidi turekebishe modura assendi yao..
 
Enzi hizo nina usafiri washanikamata sana,hawafai kabisa.
 
Mhh kile kikundi cha boko haramu pale Kimara buchasiyo cha kispoti, ukiwa na gari na ukaamua kupita pale lazima wakule kichwa!! nikisubiri mwendo kasi pale bandani huwa nawachora tu wanavyowafyeka.
Nilimshuhudia mmoja akipokea mlungula wa 10'000
 
Wale askari ni wapumbavu.. tunafanya mpango wa kuweka kamera pale wanapo oza kochi.


Wale wanaokaa kona wakijificha kwenye bajaji siku hizi hawapo ila wamehamia hapa rombo.

Kila daladala inayopita wanachukua 3000.

Kila gari la mzigo hasa magari madogo ambayo yanachukua bidhaa kama nyanya .. ndizi etc wanachukua 5000.

Magari binafsi wanakubambia makosa mengi ili utoe 10000 au 20000 bila kuandikiwa.

Cha ajabu ni askari hao hao kila siku wana kaa hapo.


Mbona huku mbagala hakuna mambo ya kiboya hayo..
 
Umesema yote rafiki yangu...yani huo ndo mtindo kwa wale wapuuzi! Lile genge lao kwakweli linatakiwa liangaliwe sivyo ni kumtafuta mmoja mmoja jioni anafanyiziwa maana wamekua kero kwakweli
Wale askari ni wapumbavu.. tunafanya mpango wa kuweka kamera pale wanapo oza kochi.


Wale wanaokaa kona wakijificha kwenye bajaji siku hizi hawapo ila wamehamia hapa rombo.

Kila daladala inayopita wanachukua 3000.

Kila gari la mzigo hasa magari madogo ambayo yanachukua bidhaa kama nyanya .. ndizi etc wanachukua 5000.

Magari binafsi wanakubambia makosa mengi ili utoe 10000 au 20000 bila kuandikiwa.

Cha ajabu ni askari hao hao kila siku wana kaa hapo.


Mbona huku mbagala hakuna mambo ya kiboya hayo..
 
Umesema yote rafiki yangu...yani huo ndo mtindo kwa wale wapuuzi! Lile genge lao kwakweli linatakiwa liangaliwe sivyo ni kumtafuta mmoja mmoja jioni anafanyiziwa maana wamekua kero kwakweli
Hahaahaa "kumtafuta mmoja mmoja jioni anafanyiziwa"

Umenikumbusha mbali sana mkuu, haya maisha acheni kabisa, watu kama hao, dah.... Aiseee
 
Back
Top Bottom