Askari Polisi wavamia mgodi wa Tanzanite na kupokonya madini kwa kutembeza kichapo

waziri2020

Senior Member
May 31, 2019
190
451
Askari polisi katika mji mdogo wa Mererani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wanadaiwa kuvamia mgodi wa Kitalu B, unaomolikiwa na mfanyabiashara, Joel Saitoti na kutembeza kichapo kwa wafanyakazi na kisha kuwapora madini zaidi ya kilo nne waliokuwa wamezalisha .

Akiongea kwa uchungu Meneja wa mgodi huo ,Martin Msigwa kutoka kampuni ya Gem and Rock Venture alisema kuwa askari polisi walivamia mgodi wao wakiwa na watu zaidi ya 30 na kuwashambulia kwa kipigo na kisha kuwapora madini kinyume cha sheria.

Alifafanua Kuwa sakata hilo ,lililotokea machi 13 mwaka huu,wakati wanaendelea na uzalishaji wa madini hayo ambapo askari hao wakiwa ameambatana na wachimbaji wengine waliwavamia na kuanza kuwapiga wafanyakazi wa kampuni hiyo wakilazimisha watoe madini waliokuwa wamezalisha zaidi ya kilo nne.

Alisema kabla ya askari hao kufika, alikuja mkaguzi wa baruti, Ezekiel Isaac ambaye alifanikiwa kuvunja geti la Mtobozano akipitia mgodi wa Franone Mining na kuingia kitalu B inayomilikiwa na kampuni ya Gem and rock bila kufuata taratibu .

"Baada ya kufika walikuta shughuli za uzalishaji zikiendelea na kutaka wapatiwe madini wakilazimisha yapitie mgodi wa Kitalu C,lakini vijana wetu waligoma kuachia madini hayo wakidai sio utaratibu wa kawaida kwakuwa mkaguzi wa baruti alikuwa mwenyewe alishirikiana na wafanyakazi wa Franone ,bila kuwepo askari polisi,jeshi la wananchi (JWTZ) na usalama wa taifa kama ilivyozoeleka"

Naye meneja msaidizi wa mgodi huo,Enock Nanyaro alidai kuwa kabla ya tukio hilo Machi 10 mwaka huu majira ya saa 10 jioni alipokea barua iliyotumwa kupitia mtandani wa WhatsApp kutoka kwa afisa mkaguzi wa baruti Ezekiel Isaac kwenda kwa meneja Nanyaro ikiitaka kampuni hiyo kusimamisha uzalishaji katika Kitalu B ili kupisha uchunguzi baada ya kuwepo malalamiko ya kuwepo kwa hewa chafu inayotokana na mlipuko wa baruti.

Nanyaro alisema kuwa uongozi wa mgodi huo uliamua kujibu barua hiyo kwa njia hiyo hiyo ya whatsup wakimweleza Mkaguzi huyo kuwa umbali waliopo ni zaidi ya mita 580 kutoka mgodi wa Franone kwa hiyo sio kweli kwamba moshi wa baruti unawafikia.

"Tunashangaa kuona kampuni ya Franone wakilalamika kuhusu moshi wa baruti wakati wapo umbali mkubwa na sisi kama ni hivyo kwanini migodi mingine ya jirani kama mgodi wa Deo Minja ,Sunday na Papaking hawalalamiki"???

Naye Wilbart Mosses mfanyakazi wa mgodi huo wa Gem and Rock Ventures amesikitishwa kuona mkuu wa usalama Mererani (DCO) kutoa amri kwa askari aliokuwa ameongozana nao kuanza kuwashambulia kwa kipigo kikali na kupokonywa madini yetu ambayo ndio ujira wetu na kuondoka nayo.

Mosses alimwomba rais Samia suluhu Hasan kuingilia kati sakata hilo ili kupata haki yao ya msingi kwani wamechoka kuonewa mara kwa mara pindi wanapoanza uzalishaji wa madini.


Endd...

Pichani mmoja ya mwanaapolo aliyeambulia kichapo cha polisi akionesha majeraha mgongoni

Wengine ni viongozi wa mgodi huo na baadhi ya wanaapolo waliopewa kichapoView attachment 2555395View attachment 2555398
 
Ukifuatilia vizuri hii habari utakuta Majungu ni mengi kwa hao askari wetu ila kwa kuwa viumbe wa kupakwa mavi na hawana pa kujitetea wacha wayaoge malipo yao mbinguni ndipo haki yao ilipo.
 
Nadhani baada ya kupokea barua ile mngepaswa kushughulikia hilo jambo kabla ya kuendelea na kazi za uchimbaji. Kitendo cha kupokea barua na kujibu tu kisha kuendelea na shughuli za kila siku ni aina fulani ya dharau ndio maana wakaja na hiyo ambushi.
Na inavyoonekana sio mara ya kwanza kupewa hayo malalamiko, labda ungeweka hao hiyo barua mliyopewa ili tuone mlichiambiwa.
But anyway, kitendo cha polisi kutembeza kipigo hadi kwa wafanyakazi wa chini sio sawa, nadhani wangedili na wamiliki na viongozi wa kampuni. Kwanza hata hiyo barua yenyewe hawakupewa hao vibarua
 
Sakata la vurugu zilizoibuka ndani ya Mgodi wa Tanzanite wa kampuni ya Gem and Rock Venture unaomilikiwa mfanyabiashara maarufu, Joel Saitoti ,limechukua sura mpya mara baada ya meneja wa mgodi huo, kuibuka na kudai kuwa Ezekiel Isack akiwa na watu zaidi ya 30 waliwavamia na kuwashambulia kwa kipigo na kisha kunyang'anya madini kinyume cha sheria.

Akitoa ufafanuzi wa sakata hilo, lililotokea machi 13 mwaka huu, meneja wa mgodi huo Martin Msigwa alidai kuwa siku ya tukio wakiwa wanaendelea na uzalishaji wa madini hayo askari hao wakiwa ameambatana na wachimbaji waliwavamia na kuanza kuwapiga wafanyakazi wa kampuni hiyo wakilazimisha watoe madini waliokuwa wamezalisha zaidi ya kilo nne.

Alisema kabla ya askari hao kufika, alikuja mkaguzi wa baruti, Ezekiel Isaac ambaye alifanikiwa kuvunja geti la Mtobozano akipitia mgodi wa Franone Mining na kuingia kitalu B inayomilikiwa na kampuni ya Gem and rock bila kufuata taratibu .

"Baada ya kufika walikuta shughuli za uzalishaji zikiendelea na kutaka wapatiwe madini wakilazimisha yapitie mgodi wa Kitalu C,lakini vijana wetu waligoma kuachia madini hayo wakidai sio utaratibu wa kawaida kwakuwa mkaguzi wa baruti alikuwa mwenyewe alishirikiana na wafanyakazi wa Franone ,bila kuwepo askari polisi,jeshi la wananchi (JWTZ) na usalama wa taifa kama ilivyozoeleka"

Naye meneja msaidizi wa mgodi huo,Enock Nanyaro alidai kuwa kabla ya tukio hilo Machi 10 mwaka huu majira ya saa 10 jioni alipokea barua iliyotumwa kupitia mtandani wa WhatsApp kutoka kwa afisa mkaguzi wa baruti Ezekiel Isaac kwenda kwa meneja Nanyaro ikiitaka kampuni hiyo kusimamisha uzalishaji katika Kitalu B ili kupisha uchunguzi baada ya kuwepo malalamiko ya kuwepo kwa hewa chafu inayotokana na mlipuko wa baruti.

Nanyaro alisema kuwa uongozi wa mgodi huo uliamua kujibu barua hiyo kwa njia hiyo hiyo ya whatsup wakimweleza Mkaguzi huyo kuwa umbali waliopo ni zaidi ya mita 580 kutoka mgodi wa Franone kwa hiyo sio kweli kwamba moshi wa baruti unawafikia.

"Tunashangaa kuona kampuni ya Franone wakilalamika kuhusu moshi wa baruti wakati wapo umbali mkubwa na sisi kama ni hivyo kwanini migodi mingine ya jirani kama mgodi wa Deo Minja ,Sunday na Papaking hawalalamiki"???

Naye Wilbart Mosses mfanyakazi wa mgodi huo wa Gem and Rock Ventures amesikitishwa kuona mkuu wa usalama Mererani (DCO) kutoa amri kwa askari aliokuwa ameongozana nao kuanza kuwashambulia kwa kipigo kikali na kupokonywa madini yetu ambayo ndio ujira wetu na kuondoka nayo.

Mosses alimwomba rais Samia suluhu Hasan kuingilia kati sakata hilo ili kupata haki yao ya msingi kwani wamechoka kuonewa mara kwa mara pindi wanapoanza uzalishaji wa madini.

IMG-20230317-WA0012.jpg
 
Sakata la vurugu zilizoibuka ndani ya Mgodi wa Tanzanite wa kampuni ya Gem and Rock Venture unaomilikiwa mfanyabiashara maarufu, Joel Saitoti ,limechukua sura mpya mara baada ya meneja wa mgodi huo, kuibuka na kudai kuwa Ezekiel Isack akiwa na watu zaidi ya 30 waliwavamia na kuwashambulia kwa kipigo na kisha kunyang'anya madini kinyume cha sheria.

Akitoa ufafanuzi wa sakata hilo, lililotokea machi 13 mwaka huu, meneja wa mgodi huo Martin Msigwa alidai kuwa siku ya tukio wakiwa wanaendelea na uzalishaji wa madini hayo askari hao wakiwa ameambatana na wachimbaji waliwavamia na kuanza kuwapiga wafanyakazi wa kampuni hiyo wakilazimisha watoe madini waliokuwa wamezalisha zaidi ya kilo nne.

Alisema kabla ya askari hao kufika, alikuja mkaguzi wa baruti, Ezekiel Isaac ambaye alifanikiwa kuvunja geti la Mtobozano akipitia mgodi wa Franone Mining na kuingia kitalu B inayomilikiwa na kampuni ya Gem and rock bila kufuata taratibu .

"Baada ya kufika walikuta shughuli za uzalishaji zikiendelea na kutaka wapatiwe madini wakilazimisha yapitie mgodi wa Kitalu C,lakini vijana wetu waligoma kuachia madini hayo wakidai sio utaratibu wa kawaida kwakuwa mkaguzi wa baruti alikuwa mwenyewe alishirikiana na wafanyakazi wa Franone ,bila kuwepo askari polisi,jeshi la wananchi (JWTZ) na usalama wa taifa kama ilivyozoeleka"

Naye meneja msaidizi wa mgodi huo,Enock Nanyaro alidai kuwa kabla ya tukio hilo Machi 10 mwaka huu majira ya saa 10 jioni alipokea barua iliyotumwa kupitia mtandani wa WhatsApp kutoka kwa afisa mkaguzi wa baruti Ezekiel Isaac kwenda kwa meneja Nanyaro ikiitaka kampuni hiyo kusimamisha uzalishaji katika Kitalu B ili kupisha uchunguzi baada ya kuwepo malalamiko ya kuwepo kwa hewa chafu inayotokana na mlipuko wa baruti.

Nanyaro alisema kuwa uongozi wa mgodi huo uliamua kujibu barua hiyo kwa njia hiyo hiyo ya whatsup wakimweleza Mkaguzi huyo kuwa umbali waliopo ni zaidi ya mita 580 kutoka mgodi wa Franone kwa hiyo sio kweli kwamba moshi wa baruti unawafikia.

"Tunashangaa kuona kampuni ya Franone wakilalamika kuhusu moshi wa baruti wakati wapo umbali mkubwa na sisi kama ni hivyo kwanini migodi mingine ya jirani kama mgodi wa Deo Minja ,Sunday na Papaking hawalalamiki"???

Naye Wilbart Mosses mfanyakazi wa mgodi huo wa Gem and Rock Ventures amesikitishwa kuona mkuu wa usalama Mererani (DCO) kutoa amri kwa askari aliokuwa ameongozana nao kuanza kuwashambulia kwa kipigo kikali na kupokonywa madini yetu ambayo ndio ujira wetu na kuondoka nayo.

Mosses alimwomba rais Samia suluhu Hasan kuingilia kati sakata hilo ili kupata haki yao ya msingi kwani wamechoka kuonewa mara kwa mara pindi wanapoanza uzalishaji wa madini.

View attachment 2555513
Saitoti hamiliki mgodi ila anahudumia mgodi wa gem n rock...sheria inasemaje ukipewa barua ya kusimamisha baruti,
 
Duh,

4kg mnafanya nayo nin kwenye nchi ya kijamaa hii, huku hutakiwi uwe na mali, unatakiwa uwe mnyonge...

Sijui lini mtawaelewa wahindi.
 
Hao walifanyiwa umafia baada ya janja janja zao kubainika.
Walete record zao za nyuma tuone kama walikuwa wanapata makilo mengi hivyo.
Muhuni hastahili heshima
 
Nadhani baada ya kupokea barua ile mngepaswa kushughulikia hilo jambo kabla ya kuendelea na kazi za uchimbaji. Kitendo cha kupokea barua na kujibu tu kisha kuendelea na shughuli za kila siku ni aina fulani ya dharau ndio maana wakaja na hiyo ambushi.
Na inavyoonekana sio mara ya kwanza kupewa hayo malalamiko, labda ungeweka hao hiyo barua mliyopewa ili tuone mlichiambiwa.
But anyway, kitendo cha polisi kutembeza kipigo hadi kwa wafanyakazi wa chini sio sawa, nadhani wangedili na wamiliki na viongozi wa kampuni. Kwanza hata hiyo barua yenyewe hawakupewa hao vibarua
Ndo waibe
 
Back
Top Bottom