Asante Mungu Kwakunipa Ajira


Mashaallah hongera zako mkuu, mimi huu mwaka wa NNE nasotea ajira lakini ngoma bad ni Tatu bila
 

Hongera sana, naomba nikupe na haya maandiko

Kumbukumbu 8:12-18

12 Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake;
13 na makundi yako ya ng'ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;
14 basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa;
15 aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu,
16 aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako; apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea mema mwisho wako.
17 Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo.
18 Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
 

Asante na nashukuru kwa kunipa ushauri kupitia neno.
 
umeomba kazi umepata kazi so fanya kazi usione kazi kuifanya hiyo kazi ila acha kazi uone kazi kupata kazi.... congulatration mkuu
 
Umeanza mwaka mpya na Bwana (Yesu)
 
Hongera ndugu yangu Mungu akubariki kwani hilo tatizo halikuwa lako pekee,ubarikiwe sana.
 

Usisahau kuishukuru na Sekretariat ya ajira!
 
Hongera ndugu na usisahau kutoa fungu la kumi kwa Mungu la mshahara wako wa kwanza

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 

Pole sana mdau,sasa ni rasmi kwamba umekua MTUMWA..

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
muwe mnashauri na njia mlizotumia kupata hizo kazi ili iwasaidie ambao bado wanasota mtaani
 
Hongera sana usisahau kutoa zaka na pia usianze kudharau washkaji wa kitaa kwa kuwa sasa umekuwa matawi ya juu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…