Asali Asali !!!!!

Asali Asali !!!!!

Endemic

Member
Joined
Jul 25, 2013
Posts
7
Reaction score
0
hallow, jaman mwenzenu nauza asali mbichi kwa dum la lita ishirini laki na ishirini, kwa mwenye mahitaj namba zangu ni 0785734279
 
nyuki wakali?
nyuki wapole?
nyuki wadogo?
nyuki chakula?.....fafanua
 
Mkuu ni ile orijino au hii ya kuchakachuliwa maana hapa daslam mchezo wa asali mzito sana aisee....
 
Wakuu ebu nisaidieni maswali yangu hapa chini;

1. Hivi asali wa nyuki wadogo na wakubwa wana tofauti gani?

2. Nasikia huwa watu wanasema asali mbichi, hii ikoje? Aina nyingine ukiondoa asali mbichi zinaitwaje?
 
Ndugu;

1. Asali mbichi ni ile asali ambayo imerinwa moja kwa moja kutoka mzingani na kuchujwa tayari kwa matumizi, ndo asali ya kawaida(fresh);

Asali iliyoiva(pikwa) hii ni asali ambayo baada ya kurinwa huwa wanaipika/au kuichemsha, sasa sijajua wanaipikaje, lakini wanasababu za kuipika ambazo sijazijua vizuri, yamkini kutakuwa na matumizi yanayohitaji ichemshwe aghalabu katika kuihifadhi!


2. Nyuki wakubwa ndo hawa nyuki wa kawaida,

Nyuki wadogo ni vidudu fulani vidogo vidogo mithili ya mbu, navyo vina asali fulani hutengeneza na mara nyingi hukaa mapangoni, asali yao ni angavu kama maji na ladha yake ni tofauti na nyuki wakubwa, hupatikana kwa uchache maana ni vidudu vidogo sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom