VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Tarehe 14/7/2013 yaani Jumapili ya kesho kutwa, kutafanyika Uchaguzi Mdogo wa Madiwani katika Kata nne za Arusha.Kampeni zimeshaisha ingawa bado 'zinaendelea'. Sasa ni kampeni zisizo rasmi. Ni mikutano ya ndani kwa ndani,nyumba kwa nyumba;kitanda kwa kitanda. Hairuhusiwi lakini inafanyika.
Kuelekea kwenye uchaguzi wa Jumapili, Tanzania inasubiri. Inataka kuona washindi wa Arusha na jinsi watakavyopatikana. Tanzania inatamani kufunikwa na kitambaa cha siasa safi na za amani. Vyama vya siasa pinzani Arusha (CHADEMA na CCM) viko tayari.
Viko tayari kushinda au kushindwa.Lakini kwa haki.Ama sivyo,haitakuwa siasa.Itakuwa vurugu.Demokrasia itabakwa.Hatutarajii hili.Tuaatarajia uchaguzi wa heri na amani. Vyama viwaache wananchi wawachague viongozi wawatakao.Kila la kheri Arusha......Mungu awe nanyi Jumapili ya tarehe 14/7/2013!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Kuelekea kwenye uchaguzi wa Jumapili, Tanzania inasubiri. Inataka kuona washindi wa Arusha na jinsi watakavyopatikana. Tanzania inatamani kufunikwa na kitambaa cha siasa safi na za amani. Vyama vya siasa pinzani Arusha (CHADEMA na CCM) viko tayari.
Viko tayari kushinda au kushindwa.Lakini kwa haki.Ama sivyo,haitakuwa siasa.Itakuwa vurugu.Demokrasia itabakwa.Hatutarajii hili.Tuaatarajia uchaguzi wa heri na amani. Vyama viwaache wananchi wawachague viongozi wawatakao.Kila la kheri Arusha......Mungu awe nanyi Jumapili ya tarehe 14/7/2013!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam