Arusha iko tayari!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Tarehe 14/7/2013 yaani Jumapili ya kesho kutwa, kutafanyika Uchaguzi Mdogo wa Madiwani katika Kata nne za Arusha.Kampeni zimeshaisha ingawa bado 'zinaendelea'. Sasa ni kampeni zisizo rasmi. Ni mikutano ya ndani kwa ndani,nyumba kwa nyumba;kitanda kwa kitanda. Hairuhusiwi lakini inafanyika.

Kuelekea kwenye uchaguzi wa Jumapili, Tanzania inasubiri. Inataka kuona washindi wa Arusha na jinsi watakavyopatikana. Tanzania inatamani kufunikwa na kitambaa cha siasa safi na za amani. Vyama vya siasa pinzani Arusha (CHADEMA na CCM) viko tayari.

Viko tayari kushinda au kushindwa.Lakini kwa haki.Ama sivyo,haitakuwa siasa.Itakuwa vurugu.Demokrasia itabakwa.Hatutarajii hili.Tuaatarajia uchaguzi wa heri na amani. Vyama viwaache wananchi wawachague viongozi wawatakao.Kila la kheri Arusha......Mungu awe nanyi Jumapili ya tarehe 14/7/2013!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Asilimia 85 ya sisi members wa jf hapa Arusha ni Mawakala, na rasmi tumeapishwa leo!
Kwahiyo tutaripoti tokea kwenye source bila kukwepesha mazee!
Shamrashamra za wenzetu wa upande wa pili ni kubwa sn hapa mjini. Vikao vya Usiku na Mchana, na leo hii nimejuzwa kuwa anawasili rasmi mzee wa "WAPIGWE TU" ili kujazia safu ya serekali.
Tunaomba sala za kila mpenda mageuzi wa Tanzania. Tupo kwenye majaribu hujawahi ona.
 
Nawaambieni mtaona na kuskia maajabu kwenye uchaguzi wa Arusha. Mungu awe nanyi Arusha
 
Tunawaombea uchaguzi wa amani.
 

Mungu mkubwa!
 
Kila la heri wanaArusha tunawakia uchaguzi mwema wenye utulivu. Makamanda tupo wote mnaiwakilisha nchi huo uchaguzi ni kiashiria cha 2015. Kila la heri dua zetu ziko pamoja nanyi.
 

Kamanda Kama Nina kuona best wishes, CUF vipi huko?
 
Wapigwe ni nani huyo?
Mkuu ni yule mpu...mbavu aliyelia bungeni..
Ee Mola wetu nakuomba sana uepushe majaribu haya na hila za shetani mwovu masisiem,HAKI ikasimame pale Arusha!!Amina!!
 
Kuna jamaa mmoja ana ugomvi na sura yake, haiPendi na hapendi kuandamana nayo hasa sehemu watu ZA WATU wanaovutia, kwasababu hawezi kuivua, chuki anapeleka kwa watu wengine kwamba wapigwe tu
 
Mzee wa 'Liwalo na Liwe".

Mzee wa "Wapigwe tu'

ha ha haaa

Mtoto wa Mkulima ni balaa, nafikiri ipo haja kumwuliza kuhusu maudhui ya kauli zake hizi, tusijeshangaa anamaanishaga mambo tofauti kabisa na anachosema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…