ABRAHAM LINCOLN
Member
- Dec 23, 2011
- 28
- 10
Ndugu Mjengwa,
Ushauri wako kwa CCM hii ya makuadi wa soko huria na wapenda kusifiwa hata wanapokuwa hawana walilolifanya linalostahili kusifiwa si sahihi kwa maoni yangu. CCM ya leo wala haistahili kupewa ushauri wako wa eti: "CCM ya sasa inapaswa kupanga mikakati ya kuendelea kuongoza dola huku ikishirikiana hata na wapinzani. Ingawa hata huo ni mtihani mgumu wenye kukihitaji chama hicho kuwa na watu makini zaidi badala ya waendekeza fitina na majungu.
" Hii CCM ya leo ni CCM ya viongozi wanaofikiria kujilimbikizia mali kupita kiasi kwa kutumia mgongo wa kushika dola pekee au na wapinzania walio walafi kama wao na ambao watakubali kutawaliwa na CCM milele. Ushauri unatoa ni hatari kwani si ushauri wa kidemokrasia. Wananchi ndio wanapaswa kupanga nani awatawale si eti "CCM ya sasa inapaswa kupanga mikakati ya kuendelea kuongoza dola huku ikishirikiana hata na wapinzani."
Yale yale yaliyopangwa gizani Zanzibar na watu wawili ya kugawana madaraka viongozi chama tawala na cha upinzani na kuzalisha vyeo lukuki vya umakamu wa Rais na gharama zake zinabebwa na watu masikini...Kwani cheo cha Waziri Kiongozi na Naibu Waziri Kiongozi vingekuwa na ubaya gani? Leo Tanzania ina Rais 2 na Makamu wa Rais wa 3 na ikianzishwa serikali ya Tanganyika basi tunaweza tukajikuta tunao labda wa Rais 3 na Makamu wa Rais 5 eti? Natumaini huo sio mmoja wa "mikakati ya kuendelea kuongoza dola huku ikishirikiana hata na wapinzani"!!!!
Hapana!!! CCM kinaitaji kuondolewa madarakani haraka iwezekanavyo kama walivyoonyesha njia watu wa Arumeru. Kikae upinzani nachenyewe na pale wakifurunda Chadema basi Watanzania wawapunzishe na wao na wawarudishe CCM. Huo ndi mfumo wa vyama vingi, Ndugu Mjengwa!. Wanasiasa wanakuwa wanyenyekevu kwa wapinga kura kwa vile wanajua watapunzishwa mara moja wakizembea katika uongozi. CCM iliyoongozwa na kauli za Mheshimiwa Mkapa na Mbunge Lusinde kule Arumeru ilistahili kubwagwa na kuangukia pua na wapiga kura makini maana ilijaa majigambo ya kijinga na kauli za kipuuzi za watu waliolewa madaraka kutokana na chama chao kutawala kwa nusu karne.Tusaidiane
Mjengwa. Mimi siku hiyo CCM itakapoondolewa madarakani na kuwa chama cha upinzani nitafufua uanachama wangu wa chama hiki kilichokuwa chenye mwelekeo wa kijamaa na kizalendo enzi za Mwalimu Nyerere pamoja na mapungufu yake ya enzi hizo katika nyanja za haki za binadamu na uhuru wa vyombo vya habari. Tanzania inaitaji vyama vikuu viwili makini na vya kizalendo, kimoja chenye kuegemea ujamaa ( CCM) na kingine kuegemea ubepari ( Chadema), lakini vyote vya vikiogozwa na watu wanyenyekevu walio tayari kuwa kwenye upinzani kura za wananchi zikiitaji hivyo.
Source: Mwl. Lwaitama
Ushauri wako kwa CCM hii ya makuadi wa soko huria na wapenda kusifiwa hata wanapokuwa hawana walilolifanya linalostahili kusifiwa si sahihi kwa maoni yangu. CCM ya leo wala haistahili kupewa ushauri wako wa eti: "CCM ya sasa inapaswa kupanga mikakati ya kuendelea kuongoza dola huku ikishirikiana hata na wapinzani. Ingawa hata huo ni mtihani mgumu wenye kukihitaji chama hicho kuwa na watu makini zaidi badala ya waendekeza fitina na majungu.
" Hii CCM ya leo ni CCM ya viongozi wanaofikiria kujilimbikizia mali kupita kiasi kwa kutumia mgongo wa kushika dola pekee au na wapinzania walio walafi kama wao na ambao watakubali kutawaliwa na CCM milele. Ushauri unatoa ni hatari kwani si ushauri wa kidemokrasia. Wananchi ndio wanapaswa kupanga nani awatawale si eti "CCM ya sasa inapaswa kupanga mikakati ya kuendelea kuongoza dola huku ikishirikiana hata na wapinzani."
Yale yale yaliyopangwa gizani Zanzibar na watu wawili ya kugawana madaraka viongozi chama tawala na cha upinzani na kuzalisha vyeo lukuki vya umakamu wa Rais na gharama zake zinabebwa na watu masikini...Kwani cheo cha Waziri Kiongozi na Naibu Waziri Kiongozi vingekuwa na ubaya gani? Leo Tanzania ina Rais 2 na Makamu wa Rais wa 3 na ikianzishwa serikali ya Tanganyika basi tunaweza tukajikuta tunao labda wa Rais 3 na Makamu wa Rais 5 eti? Natumaini huo sio mmoja wa "mikakati ya kuendelea kuongoza dola huku ikishirikiana hata na wapinzani"!!!!
Hapana!!! CCM kinaitaji kuondolewa madarakani haraka iwezekanavyo kama walivyoonyesha njia watu wa Arumeru. Kikae upinzani nachenyewe na pale wakifurunda Chadema basi Watanzania wawapunzishe na wao na wawarudishe CCM. Huo ndi mfumo wa vyama vingi, Ndugu Mjengwa!. Wanasiasa wanakuwa wanyenyekevu kwa wapinga kura kwa vile wanajua watapunzishwa mara moja wakizembea katika uongozi. CCM iliyoongozwa na kauli za Mheshimiwa Mkapa na Mbunge Lusinde kule Arumeru ilistahili kubwagwa na kuangukia pua na wapiga kura makini maana ilijaa majigambo ya kijinga na kauli za kipuuzi za watu waliolewa madaraka kutokana na chama chao kutawala kwa nusu karne.Tusaidiane
Mjengwa. Mimi siku hiyo CCM itakapoondolewa madarakani na kuwa chama cha upinzani nitafufua uanachama wangu wa chama hiki kilichokuwa chenye mwelekeo wa kijamaa na kizalendo enzi za Mwalimu Nyerere pamoja na mapungufu yake ya enzi hizo katika nyanja za haki za binadamu na uhuru wa vyombo vya habari. Tanzania inaitaji vyama vikuu viwili makini na vya kizalendo, kimoja chenye kuegemea ujamaa ( CCM) na kingine kuegemea ubepari ( Chadema), lakini vyote vya vikiogozwa na watu wanyenyekevu walio tayari kuwa kwenye upinzani kura za wananchi zikiitaji hivyo.
Source: Mwl. Lwaitama