Apple Inayumba Ingawa Bado Ni Kigogo

Apple Inayumba Ingawa Bado Ni Kigogo

ManiTek TV

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2011
Posts
410
Reaction score
159
Apple inayumba Ingawa Bado ni Kigogo



Apple wametangaza mambo mawili makubwa, awali wametangaza matokeo ya mapato katika robo ya kwanza ya mwaka 2013. Pili wametangaza mkutano rasmi wa watengenezaji wa programu za iOS na Mac OSX unaojulikana kama World Wide Developers Conference (WWDC). Kwa kawaida Apple inapotoa matangazo kama haya huwa ni wakati ambao kampuni hiyo huonyesha uwezo wake mkubwa kama moja kati ya kampuni kigogo katika teknolojia Duniani, lakini safari hii kuna hali ya mchanganyiko, yapo yenye kuonyesha umwamba wa Apple na pia yapo mambo ambayo ni ya kuvunja moyo.


Tim Cook katika tangazo la mkutano wa WWDC ambao utaanza tarehe 10 mwezi Juni na kumalizika tarehe 14 mwezi huo huo, akiripotiwa na Engadget Distro, ameweka wazi kuwa wadau wasitarajie bidhaa yoyote mpya na badala yake Apple watatoa bidhaa mpya katika kipindi cha mwezi wa tisa. Wengi miongoni mwa wanateknolojia walitarajia kuwa Apple wangetoa iWatch, iPhone mpya, iPad Mini 2 au iPad 5, hivyo tangazo hili sio tu limevunja moyo bali pia limezima kila aina ya tetesi na uvumi unaohusiana na bidhaa mpya zinazotarajiwa kutolewa na Apple mwezi Juni.


Pia tangazo hili maana yake Apple wameipa Samsung Galaxy S4 nafasi kubwa ya kutamba katika mauzo kwa karibu miezi mitano mpaka sita. Iwapo Apple watatoa iPhone 5S basi itakuwa ni vigumu kuyafikia mauzo ya Galaxy S4 ingawa uwezekano wa kuyafikia mauzo kwa iPhone 6 ni mkubwa. Tofauti ya 5S na 6 ni kwamba 6 itafanyiwa mabadiliko makubwa wakati 5S ni simu ile ile yaani iPhone 5 lakini itaongezwa kasi tu. Hatuelewi ni kwa nini Apple huipa nafasi kama hii Samsung wakati katika tableti Apple walifanya mkakati mzuri wa kuzuia mauzo ya Microsoft Surface kwa kutoa iPad With Retina Display muda mchache kabla ya kutoka kwa tableti hiyo, iPad hii ilitolewa kinyume na ratiba ya kawaida ya Apple hivyo ni wazi ililenga kwenye upinzani wa kibiashara badala ya mauzo ya kawaida. Pia Apple walitoa iPad Mini kuhimili mauzo ya utitiri wa tableti ndogo za Android kama vile Nexus 7, Amazon Kindle Fire na Samsung Galaxy Tab 2 - 7.0.


Kwa mujibu wa jarida la Engadget Distro; akijibu maswali, Afisa Mtendaji Mkuu wa Apple Tim Cook pia ameeleza wateja wasitarajie iPhone kubwa zaidi mwaka huu kwa vile unapoongeza ukubwa wa simu basi hupelekea kupoteza ubora wa skrini na apps pia haziwezi kufanya kazi na skrini hiyo mpaka pale watengenezaji watakapozifanyia marekebisho. Katika suala la ubora wa skrini hatuelewi ni kwa nini Cook ametoa madai kama haya, hii ni kutokana na ukweli kwamba tayari kuna simu kama vile Sony Xperia Z ambayo ina skrini kubwa na bora kuliko ile ya iPhone 5.


Lakini Cook yuko sahihi katika suala la apps kutofanya kazi kwa usahihi katika ukubwa mpya wa skrini, kwani mpaka sasa kuna maelfu ya apps ambazo bado huonyesha weusi juu na chini ya sehemu ya skrini katika iPhone 5 kwa vile watengenezaji wake hawakufanya marekebisho au uboreshwaji waliotakiwa kuufanya. Hii ina maana kwamba apps ambazo zinafanya kazi kwa ufanisi na iPhone 5 ni chache ukilinganisha na zile zinazofanya kazi na iPhone zenye skrini ya inchi 3.5 yaani iPhone 4S kurudi nyuma.


Hata hivyo kwa upande wa iPad Mini hali haikuwa hivyo kwani iPad hiyo imepewa rizolushani sawa na zile za iPad 2, hivyo watengeneza apps hawakuhitaji kufanya chochote ili apps zao zifanye kazi kwa usahihi katika iPad Mini. Hivyo hii maana yake ni kwamba ingawa iPad Mini ni ndogo kuliko iPad 2 lakini Mini ina skrini bora kuliko iPad 2. Hili kulitekeleza kwa upande wa iPhone ni gumu, kwani ukiongeza ukubwa na kuacha rizolushani zile zile ndio ubora wa skrini hupotea na si rahisi kuipa skrini ya ukubwa wa inchi 5 kwa mfano rizolushani sawa na za iPad kama ilivyofanyika kwenye iPad Mini. Hii pia maana yake ni kwamba iPad Mini kuwa na kioo cha retina itakuwa ni jambo gumu kidogo, ingawa linawezekana


Kwa upande wa ripoti za fedha Apple imetangaza faida ya Dola bilioni tisa na nusu, sambamba na hili Apple pia imeuza iPhone milioni thelathini na saba na laki nne (milioni 37.4) na iPad karibu milioni ishirini. Wakati mauzo ya iPad na iPhone ni yenye kuridhisha na kuonyesha Apple bado ni kigogo, faida kubwa iliyopatikana bado ni pigo kwa Apple kwani ikilinganishwa na kipindi kama hichi mwaka jana faida ya kampuni hiyo imeteremka. Hata hivyo faida ya bilioni tisa maana yake Apple si kampuni ambayo inaweza kuelezewa kwamba inaanguka bali ni kampuni ambayo inashindwa kuyafikia mafanikio yake ya miaka iliyopita.

Chanzo: gajetek habari
 
Nilifurahi sana walipochemka kwenye map tusubiri iphone 6 labda wataboresha unles otherwise warudi kutumia google map kama default map
 
wakichemsha ,wakiboogie sina shaka...Apple ,HTC, Samsung....wote......nakula nao keki!:twitch:
 
Dah!! Hyo faida kujafikiwa na kina techno na g tide n ndoto ya kimweli
 
Dah!! Hyo faida kujafikiwa na kina techno na g tide n ndoto ya kimweli

kweli aisee ngoja nifanye uchunguzi,maana tecno nao wamelisongesha hasa ukiacha utitiri zile t20,t340 na zingine ambazo ni za android.
 
Kushuka kwa faida kidogo tu kumewatia wasiwasi, kweli binadamu hatosheki


Sent from my EyePhone
 
Apple wasipokuwa makini watalajie anguko kubwa, bado ile gape ya Steve Jobs haijapata mtu wa kuiziba.
Samsung na HTC wanakuja kwa kasi sana.
 
Apple wasipokuwa makini watalajie anguko kubwa, bado ile gape ya Steve Jobs haijapata mtu wa kuiziba.
Samsung na HTC wanakuja kwa kasi sana.

actually apple share zake ndo zinashuka thamani na profit imeshuka kidogo lakini revenue na wingi wa mauzo ya simu yameongezeka sana.

Samsung ni tishio kwa apple

lakini huyo htc upo wrong vibaya mno htc ana karibia mwaka na nusu sasa profit na revenue zinashuka mwenzako anaenda kufilisika we unampamba atampita apple.

Apple ameuza iphone 47.8 million na ipad 22.9 milion kama device milion 70 wameuza zenye ios (sjaeka ipod).

Revenue ilikua ni 54.5 billion

twende htc sasa wao revenue yao ni 1.42 bilion

angalia difference yake na apple 54.5 against 1.42 yani hata havifananishiki

kuhusu idadi ya simu walizouza htc hawajafikisha milion 9 against milion 47 za apple

nashangaa why watu wanawa over rate sana htc
 
Apple wasipokuwa makini watalajie anguko kubwa, bado ile gape ya Steve Jobs haijapata mtu wa kuiziba.
Samsung na HTC wanakuja kwa kasi sana.

Watu wanaongozwa na emotional na hawatembelei website zinatoa technology news mara kwa mara,
 
kweli aisee ngoja nifanye uchunguzi,maana tecno nao wamelisongesha hasa ukiacha utitiri zile t20,t340 na zingine ambazo ni za android.

mh Mkuu Umenkumbusha Kitu!! juz Nlikua Mbeya Mwanjelwa !!! kutembelea Maduka Ya Simu Na Kutana Na Michina (simu Na Tablets) Za Androids!! simu Ni 80 Tuu!! dah Nmecheka Sana Tablets Skuulza Beiii!!
 
apple wamenimaliza akili kabisa ila sony jamani nao wanasimu nzuri pia Samsung apps za android ziko poa ila sijapenda umbo la simu zao kabisa zimekaa ki kike kike sana sorry to say that
 
BEI ZA DISPLAY (VIOO).
.
SAMSUNG (S) SERIES.
.
. TSH .
.
Samsung s3
Kioo 80,000. - SUPER AMOLED.
.
Samsung s4
Kioo 70,000. -TFT.
kioo 110,000.- SUPER AMOLED.
.
Samsung s5
Kioo 95,000.-TFT.
kioo 170,000.-SUPER AMOLED.
.
Samsung s6
Kioo 180,000.-SUPER AMOLED.
.
Samsung s6 Edge
Kioo-190,000-SUPER AMOLED.
.
Samsung s6 Edge Plus
Kioo-270,000.-SUPER AMOLED
.
Samsung s7
Kioo 190,000.-SUPER AMOLED.
.
Samsung s7 Edge
Kioo-300,000-SUPER AMOLED.
.
Samsung s8
Kioo-380,000.-SUPER AMOLED .
.
Samsung s8 plus
Kioo-400,000-SUPER AMOLED.
.
Samsung s9
Kioo-400,000-SUPER AMOLED.
.
Samsung s9 Plus
Kioo-420,000-SUPER AMOLED.
.
. ********VIOO NI MPAKA UWEKE ORDER ALAF NDO NIAGIZE INATUMIA WEEK 2 MPAKA KUPATA KIOO CHAKO*************
.
.
PIA VIOO VYA SIM NYENGINE
TUNAAGIZA ...........iPhone,Huawei,Lenovo,Oppo,....Vivo,Xiaomi,Infinix n.k

ℕ𝔹; 𝕍𝕀𝕆𝕆 ℕ𝕀 𝕆ℝ𝕀𝔾𝕀ℕ𝔸𝕃, ℕ𝔸 𝕎𝔸ℝℝ𝔸ℕ𝕋𝕐 𝕐𝔸 𝕄𝕀𝔼ℤ𝕀 𝕄𝕀𝔼ℤ𝕀 𝟞

Tupigie/tutumie ujumbe mfupi (SMS). 0784757203.
#0784757203 .
LOCATION.
Kijichi, Mbagala kuu, Temeke, Dar es Salaam, Tanzania.
 
Back
Top Bottom