Angekuwa wewe ungefanyaje?

Kwanza pesa si yako. Naye anafahamu hilo. Mweleze muende kwa wazazi na ndugu waliokupa huo mtaji watoe uamuzi. Hii itakuepusha na lawama kwake na waliokukabidhi huo mtaji. PESA SI ZAKO.
 
Dah mzee umezungumza kitu cha maana ila watu hawatakuelewa ,maisha haya kila kitu fanya kwa kiasi ,usifanye jambo ukapitiliza mpaka ukajinyima kila kitu kwa ajili ya mtu mwingine ambaye hatokuja jinyima kwa ajili yako ,utaumia sana mbeleni huko ,binaadamu sio wa kuwaaamini kabisaaaa
 

Marafiki huwa wabinafs mno tena wakikuona una roho nzuri Ndio wanatake advantage
 
Marafiki huwa wabinafs mno tena wakikuona una roho nzuri Ndio wanatake advantage
Watu wabinafsi haswa marafiki utawagundua kupeleka shida zake mbele kweny upande wake haswa kweny ishu za pamoja ..Kama hapo alitakiwa kujua kwamba ishu ya mzee wake ni yake private sio kuileta kwa rafiki yake
 
Mkuu kwanza futa neno rafiki kabisa, ili neno rafiki limeniponza mpaka leo sio chini ya ml 30 zimepotea kwenye mikono ya marafiki alafu hakuna nilichovuna zaidi ya unafiki, nilichoamua mpk sasa mm sina neno rafiki maishani mwangu alafu hao niliokuwa nawaita marafiki nilishawaambia hata nisikie yeye au ndugu yake yoyote anakufa sitatoa msaada hata kwangu mm nimewaambia sitaki msaada wao, huyo unayemwita rafiki sasa mpe hiyo hela utakuja kusimulia hapa tena atachokulipa baada ya kumpa hiyo hela, kama wadau wanavyosema hapo juu kupanga ni kuchagua mpe urafiki ufe au usimpe urafiki ufe, ila mm ningechagua kutokumpa wacha urafiki ufe nina experience mbaya sana na hawa watu tunaowaita marafiki.
 
Eti rafiki..urafiki unakufa.
Kama hizo pesa zisingekuwepo angefanyeje?
Pesa si zako kwanini umpe?
Kwani ni lazima ulipie urafiki wenu?
 
Mwambie rafiki yako kwamba huna sauti ya mwisho juu ya hzo pesa mpka ushirikishe Wazazi wako

Then rudi nyumban kwa wazee wako ongea nao swal litakuja why umemwambia una pesa utajua jinsi ya kujitetea then baada ya hapo sikilza maamuz yao

Wakikupa ruhusa ya kias gan umpe toa wasipokupa usitoe kamwambie ukwel Rafiki yako ili ajue kwamba ni nje ya.uwezo wako.
 
Kama huyo rafiki ni kama ndugu kama ulivyosema itakuwa hadi kwenu wanamfaham, itakuwa vyema kuongea na familia yako uone wanasemaje ila usijichukulie maamuzi wewe kama wewe maana baadae utakuja kujutia mambo yakibadilika sababu hela zinavunja sana urafiki hata undugu
 
Tutegemee nyuzi za majuto toka kwa mleta uzi.
Jamaa hakutakiwa kuigusia pesa yako, angekushirikisha hali ya mzee then wewe ndo ujichekeche.

Hiyo ya kusema mwanangu si una ile hela basi naiomba( aisee hiko ni kosa).

Washirikishe ndgu zako hilo tatizo, ukimpa bila kuwashirikisha. Yakitokea ya kutokea huenda ukakosa utetezi mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…