Makirita Amani
JF-Expert Member
- Jun 6, 2012
- 1,914
- 3,437
Habari rafiki,
Nimekuwa nawashauri watu ambao wanataka kuingia kwenye biashara na hawajui pa kuanzia basi waingie kwenye biashara ya mtandao (network marketing).
Huu ni mfumo bora kabisa wa kibiashara ambapo mtu anajifunza mengi kuhusu biashara ikiwa ni pamoja na kunadi biashara yako, kujenga timu na kujiamini.
Lakini pia kuweni makini na hizi kampuni zinazochipukia za biashara hiinya mtandao, nyingi siyo halisi.
Nikupe vitu vitatu muhimu vya kuangalia kabla hujaamia kuingia kwenye biashara ya mtandao unayoambiwa inalipa vizuri;
1. Biashara iwe na bidhaa au huduma ambayo watu wanaihitaji na wapo tayari kulipia.
2. Uwe unalipwa kutokana na faida inayopatikana baada ya watu kununua bidhaa, na siyo ulipwe kwa kuwaingiza watu pekee.
3. Anayekuambia uingie kwenye biashara fulani ambayo yupo yeye akisema inalipa, mwambie kwanza akuoneshe ushahidi wa yeye kulipwa cash, kama hajawahi kulipwa cash ila anaambiwa tu ana hela zake zipo kwenye mfumo, kimbia haraka sana,huo ni utapeli.
Neno la mwisho kwakp rafiki, hakuna biashara rahisi, hakuna njia ya haraka ya kupata fedha ambayo haikutoi jasho la mwili au akili. Usipoteze muda wako kwa mambo ya utapeli.
Weka juhudi kwenye biashara sahihi na utafanikiwa.
#MUHIMU; Naandika kitabu kuhusu BISHARA YA MTANDAO, mambo yote muhimu mtu anayopaswa kuyajua. Kama una swali kuhusu biashara hii au una kampuni ambayo ungependa kuijua kwa undani niandikie swali lako kwenye email makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Rafiki na kocha wako,
Makirita Amani,
www.makirita.info
Nimekuwa nawashauri watu ambao wanataka kuingia kwenye biashara na hawajui pa kuanzia basi waingie kwenye biashara ya mtandao (network marketing).
Huu ni mfumo bora kabisa wa kibiashara ambapo mtu anajifunza mengi kuhusu biashara ikiwa ni pamoja na kunadi biashara yako, kujenga timu na kujiamini.
Lakini pia kuweni makini na hizi kampuni zinazochipukia za biashara hiinya mtandao, nyingi siyo halisi.
Nikupe vitu vitatu muhimu vya kuangalia kabla hujaamia kuingia kwenye biashara ya mtandao unayoambiwa inalipa vizuri;
1. Biashara iwe na bidhaa au huduma ambayo watu wanaihitaji na wapo tayari kulipia.
2. Uwe unalipwa kutokana na faida inayopatikana baada ya watu kununua bidhaa, na siyo ulipwe kwa kuwaingiza watu pekee.
3. Anayekuambia uingie kwenye biashara fulani ambayo yupo yeye akisema inalipa, mwambie kwanza akuoneshe ushahidi wa yeye kulipwa cash, kama hajawahi kulipwa cash ila anaambiwa tu ana hela zake zipo kwenye mfumo, kimbia haraka sana,huo ni utapeli.
Neno la mwisho kwakp rafiki, hakuna biashara rahisi, hakuna njia ya haraka ya kupata fedha ambayo haikutoi jasho la mwili au akili. Usipoteze muda wako kwa mambo ya utapeli.Weka juhudi kwenye biashara sahihi na utafanikiwa.
#MUHIMU; Naandika kitabu kuhusu BISHARA YA MTANDAO, mambo yote muhimu mtu anayopaswa kuyajua. Kama una swali kuhusu biashara hii au una kampuni ambayo ungependa kuijua kwa undani niandikie swali lako kwenye email makirita@kisimachamaarifa.co.tz Rafiki na kocha wako,
Makirita Amani,
www.makirita.info