Anataka nimuoe na mtoto wake


mnazaaje kabla ya ndoa,,,kuishi na mwanamke ambaye amezalishwa,na,jitu jingine kikwetu jamii inakutenga.
 
kuwa makini sana...kama kujikanganya ni mapema yote hiii kuwa makini...sio unadandia treni kwa mbele
 
Mimi napita tu, haya mambo magumu sana naona wazungu kidogo wenzetu wameyamudu.
 
Labda kikubwa zaidi kwa wasomaji hasa mabinti kuna lolote wanalojifunza kwenye mada hizi au bussiness as usual?
 
Kaka bila kupindisha maneno huyu dada humpendi. Tena humpendi kabisaaaa wala usizuge hapa eti unampenda. Ungekuwa unampenda usingeona shida kumlea mtoto wake hata km babaake yupo hai. Muache dada wa watu mapema ili aumie then azoee hayo maumivu aendelee na maisha yake. Kuwa na mtoto sio sababu ya kumpa mwanamke masharti ya ndoa aise... usijilazimishe kufanya kitu ambacho hautakuwa na amani maisha yako yote. Mtoto yupo na ataendelea kuwepo.
 
mnazaaje kabla ya ndoa,,,kuishi na mwanamke ambaye amezalishwa,na,jitu jingine kikwetu jamii inakutenga.

Maisha ya mwanadamu yana na mapito mengi ikiwa ni pamoja na kuzaa kabla au nje ya ndoa; kutengwa ni sehemu ya maisha pia. Ni kawaida kwa binadamu kujihesabia haki na kuhukumu wengine, kwa hiyo jamii yako takatifu kuwatenga wanawake waliozaa kabla ya ndoa ni sawa tu. Aliyetengwa naye akijitenga ndo inakuwa tatizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…