WE ARE ANONYMOUS
JF-Expert Member
- Mar 23, 2015
- 217
- 284
Jamaa yangu anaomba ushauri na nimeshindwa nimshauri nini nimeona niilete kwenu wana JF:
Tiririkeni wana JF tumshauri huyu muungwana.
NIMEMPATIA HUU:
Firstly; Huyo bwana amjali mkewe na kumpatia haki yake ya ndoa kwa ukamilifu. Yeye ndiye amekubaliwa na kuoana na huyo mwanamke, sasa wasiwasi wake ni wa nini?
Secondly; Amwamini mkewe. Wivu mwingine uliojengwa juu ya hisia tu pasipo justifications mara nyingi ni hatari na hauna maana sana. Anachotakiwa kuelewa ni kwamba huyo mwanake hakumuoa akiwa bikira, ni lazima alishaonjwa na wanaume wengine huko nyuma. Muhimu ni kuwa yeye sasa ndiye mume wa mke huyo, ajiamini tu. Mke au mume hachungwi kama ng'ombe, otherwise kwa mtindo wa maisha wanayoishi ya kutoaminiana, they will not last for too long!
Thirdly; Why don't they talk? Kwa nini kila mmoja asiwe wazi kwa mwenzake? Kwa nini wanaviziana?.......Kwa maelezo yako haya, hii ni observation yangu kuwa, hawa wanandoa wamekosa kitu muhimu sana, MAWASILIANO.
Mahusiano/ndoa nyingi zinakufa/vunjika kwa sababu ya kukosekana kwa mawasiliano miongoni mwa wenzi. Wazungumze na mume kama ana wasiwasi fulani dhidi ya mwenzi (mke) wake. Trust me, kama approach ya mazungumzo hayo itakuwa ya kiungwana yenye lengo la kujenga, mume atapata mengi sana toka kwa mkewe vivyohivyo mke naye. From there, kila mmoja atamwelewa mwenzake kwa maana ya strengths and weaknesses zake na likes and dislikes zake na kwa hiyo kuchukuliana na kuaminiana kutaongezeka, furaha na amani ndani ya nyumba itaongezeka maradufu na watu wote nje ya wao wenyewe hawatakuwa threats tena ukiwemo wewe ambaye jamaa anakuhisi una mahusiano yaliyovuka mpaka na mke wake.
Njia anayotumia mwanamume ya kutoa maelekezo tu pasipo mazungumzo na mkewe ya "sitaki ukaribu na flani" au sitaki hiki au kile, siyo sahihi na kiukweli hai imairishi mahusiano bali inayadhoofisha na itafika wakati haitafanya kazi tena na mwisho wa siku ndoa hiyo itakufa!
Hebu tujaribu kufikiri ni kwa nini huyu mama anafikia hatua ya kuamua kutafuta ushauri nje ya mume wake? Ni kwa nini huyu mama anatunza text messages ktk simu yake anazofikiri ni za kumfariji hata nwisho wake mume wake akazinasa?..
Ni kwa sababu something is missing in her relationship (i.e her husband) and she thought, the option is to look it somewhere outside, kwa jamaa yake wa zamani japo huyu bwana kasema hajawahi kuwa na mhasuniano ya kingono. Lakini ktk hili ni lazima tujue kuwa, tendo la ndoa linalofanyika kwa ukamilifu, ni sehemu tu ya mambo mengi yanayoimarisha mahusiano/ndoa. Mengine ni kama kujali hisia za mwenzako, upendo nk.
Ni kwa muktadha huu kwamba, huyu bwana wala hana sababu ya kuvunja uhusiano na rafiki yake ktk mazingira haya na kwa sbb tu eti anahisi mkewe anatembea na rafiki yake huyo kwa kusoma txt msg za simu ya mkewe na kusikia ya watu wa nje wasemavyo, bali ajichunguze yeye mwenyewe na atagundua kosa na udhaifu wake.
Trust me, mkewe akiwa anapata vyote anavyostahili toka kwa mumewe (na hapa si maanishi material things kwa sbb hivyo vipo tu na wanavyo), namaanisha mapenzi, upendo, heshima, kujali hisia za mwenzake na mengine yanayofanana na hayo, hayo mengine yatajifuta yenyewe naturally!!
NA KUMWAMBIA, MKE WA MTU NI SUMU, JAPO ANASEMA ALISHAACHA MAZOEA NA HUYO MKE WA JAMAA KITAMBO SANA, SEMA HIZI ISHU ZIMETOKEA JUZI KATI, KWAMBA MKE WA HUYO JAMAA ALIMCALL AKAMWAMBIA SINCE HICHO KIPINDI ASOME SMS AMEKUWA AKIMUULIZA SANA ABOUT YEYE NA AMEAMBIWA WASHAWAI KUWA PAMOJA, JAMAA ANASEMA HATA MESSAGE ZA HUYO MWANAMKE NOW HAJIBU NI MWEZI WA PILI HUU LABDA AWE AMEMPA SALAAM TU KWAMBA MNAENDELEAJE ATAMJIBU IN SHORT.
Tiririkeni wana JF tumshauri huyu muungwana.