Amemfumania mchumba wake aki cheat, afanye nini?

Amemfumania mchumba wake aki cheat, afanye nini?

Huyo binti anatakiwa amuombe msamaha mchumba wake. Kwa nini amfanyie ambush saa tano usiku? Jemaa angekuwa na bastola ingekuwaje?

Kama alishindwa kumwambia kwamba amekutana na huyo msichana unategemea amwambie eti leo kuna demu anakuja au alikuja kulala kwangu ni lazima angefanya kicricri. Mi namshauri amwache co unaamua kua nae then unakuja kujutia baadae!
 
Amekuwa na mahusiano na Boyfreind then Mchumba wake kwa miaka minne na nusu. Kwa mara ya kwanza amemkamata akicheat. Anasema boyfriend wake alikuwa amuelewielewi kwa siku mbili hivi, akaamua kufanya ambushi usiku wa saa tano kwa mchumba wake. Looh!! akamkamata mpenzi wake na msichana mwingine live bila chenga. Aligundua pia mchumba wake na huyu mfumaniwa walikutana wiki moja iliyopita. Mchumba wake alimwalika mfumaniwa waspend usiku huo. Kwa hasira mdada akavunja mahusiano na jamaa mda uleule kwa hasira na kusepa.

Sasa imepita wiki mbili, jamaa anaomba msamaha na kuomba msamaha kwa second chance. Kitu ambacho kinamuumiza sana ni kwamba msichana aliyemfumania yupo tofauti sana na yeye. Mfumaniwa kwa kweli kakamilika kila idara, namba nane Yeye wa kawaida sana.

Amesema Mchumba wake amemwambia kosa
hilo amefanya kwa mara ya kwanza, mdada amekubali kuwa ni kweli anaamini ni mara ya kwanza. Mchumba wake anataka waende mbele na plan yao ya kufunga ndoa.

Nimemuongelea hapa kwa wana MMU ili mimi niprint the best advice, japo mimi nami nimesha mpa ushauri wangu ila hapa MMU funga kazi.
Madada kama wewe umevaa viatu vyake utafanya nini? Utamsamehee a cheat?





Kusamehe inaweza kuwa ni jambo zuri, lakini kuna vitu muhimu ambavyo mfumaniaji anatakiwa kuchunguza na kujiridhisha kuwa vitabaki sawa. Na mbona kamsamehe haraka hivyo? Ana uhakika gani kama alicheat mara moja tu? Ana uhakika gani kama alicheat na msichana mmoja tu? Kuna sababu gani ya kuwa na uchumba wa zaidi ya miaka 4 bila ndoa? Na afya je? Ana uhakika gani kama huyo jamaa alitumia kinga na hajaambikizwa gonjwa lolote na hasa ukizingatia nyie vijana mnatumia kila kitu kwenye mapenzi?

Ushauri binafsi, ni bora angempa muda kidogo na kufuatilia baadhi ya vitu muhimu kuliko kusamehe kwa haraka kiasi hiki! Nalazimika kuhisi kuwa kwa sababu kaambiwa kuna mpango wa ndoa, na yeye anataka ndoa, ndiyo maana kalegea mapema hivyo.
 
Ushauri wangu ni hivi: Kama huyo dada ni mwaminifu asilimia zote kwa mchumba wake basi namshauri amwache huyo mwanaume lkn Kama na yeye amewahi kupita kando hta km hakukamatwa basi amsamehe.
 
AKUMULIKAYE MCHANA, USIKU ATAKUCHOMA... safari ya cheating ikianza mapema hivyo basi binti atarajie makubwa ndani ya ndoa
 
Tukumbuke kwamba WANAWAKE WAKO WENGI SANA LAKINI SIO WOTE WANAOFAA KUITWA "MKE WA MTU"....alichokifanya huyo kaka ni tamaa tu za mwili wake zilimshinda kujizuia akajikuta kamtamani huyo dada....lakini pia tukirudi upande wa dada( mchumba) je kaka alipokuwa anataka " vituz" ulimpa bila tatizo??
Sasa kama dada anajiamini anatakiwa amsamehe kwa kujiamini kwamba yeye ndo "MWANAMKE BORA" NA SIO "BORA MWANAMKE"
Wanawake wa kisasa tunatakiwa kujiamini na hayo yaliyotokea ndo yatawafanya hao wachumba wajifunze kwamba ni wapi walikosea ili wajirekebishe na watakapoingia kwenye ndoa itakuwa ndoa imara sana....Nawatakia kila la kheri kwenye ndoa yao!!
 
Back
Top Bottom