Amani ya Nchi na Uchaguzi

Amani ya Nchi na Uchaguzi

mtwana

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
428
Reaction score
141
Habari Zenu wana Ukumbi,

Baada ya salamu

Napenda kuwasihi sana Watanzania wenzangu kuwa tunaelekea katika kipindi cha uchaguzi. Tujitokezeni kwa wingi ktk Kampeni na tudumishe amani mda wote na ikibidi kampeni zetu ziwe za kistaarabu. Matusi sio silaha ya kumuangusha mpinzani wako, ila sera zako za ukweli ndio zitakazoweza kumuangusha mpinzani wako

Ama katika suala la kuchagua usishawishiwe na mtu yoyote kwa kukulaghai (kukupa rushwa) maana rushwa ni adui wa haki, fanya chaguo ambalo unahisi nini moyo wako unakwambia na sio unachagua ati kwa kuwa fulani amekwambia uchague

Zaidi tumuombe sana Aliyetuumba atudumishie amani katika nchi yetu tuzidi kupendana na isiwe siasa ikaja kutufarakanisha

Asante
 
Mtaona jinsi jiwe na CCM watakavyo jiharibia wao wenyewe ndio mtajua kweli nguvu ya wananchi ni kubwa kuliko ya majeshi tuliyonayo.
 
Baada tu ya kifo cha Baba wa Taifa, rushwa ikageuka kuwa ni halali ndani ya chama tawala. Kuna wakati ilifikia kiwango na kuipa jina la "takrima". Kwa sasa inafumbiwa macho kwa kundi fulani la wateule wachache wenye kukubalika mbele ya macho ya Mwenyekiti, ambao hata wakionekana wakijipitisha majimboni na kugawa rushwa kwa uwazi hakuna wa kuwagusa.

Hawa ambao unasikia wanakamatwa na TAKUKURU ni "rejects" ambao wapo ktk orodha ya kukatwa majina yao, hata kama wataongoza ktk kura za maoni. Ebu fikiria mtu kama Polepole ambaye ndiye mwenye kushikilia fungu la kufanya "bargaining & purchasing" kwa njia ya ghiliba ili kuweza kuwanasa waunga juhudi, huyu pia ndiye eti mwenye kuhubiri kuwa anaichukia rushwa.

Rushwa na CCM ni kama maisha ya samaki ndani ya maji. Ustawi wa chama hiki na mchakato wa upangaji wa safu yake ya viongozi toka taifa mpaka matawini kwa sehemu kubwa hutegemea rushwa ya fedha, ngono zembe, uzinzi, upendeleo wa fursa za kimaslahi na hata ushirikina. Bahati mbaya ni kwamba, hiki kitu wapiga kura wengi hawana fursa wala njia ya kupata taarifa sahihi juu ya hao ya viongozi waliojitokeza na wanaopigiwa debe.
 
Back
Top Bottom